Saturday, May 31, 2008

WIKI HII

Youth Christian organization fellowship, which conduct prayer as youth Christian prayer network
Mtandao huu wa maombi ya vijana walio dhamilia kudhihilisha Nguvu za Mungu duniani

Hata ikawa mwisho wa siku saba neno la bwana likanijia kusema mwanadam nimekuweka kuwa mlinzi juu ya nyumba ya izraeli [eze 3:16 ]
Mambo ya kuombea

v Ombea watumishi wa Mungu ambao mungu anawatumia juu ya Taifa , Mungu awape mafunuo juu ya Taifa utulivu na unyenyekevu mkubwa, kataa roho za kujiona bora kuliko wengine , ombea familia zao , ndoa zao ,mafanikio ya kiuchumi, hata kama wametenda dhambi omba toba juu yao , hawa ni maaskofu , wachungaji ,na wainjilsti,
v Ombea huduma ya mana ,mtumishi Mwakasege, ombea huduma ya agape,mtumishi fenandusi, ombea huduma ya mama lwakatale, Nabii mwingila,pastor hiza ,newlife oustrich under egon falk,huduma ya ukwata, huduma ya new life band, new life ministry , scripture union na huduma zingine nyingi Mungu ametumia huduma hizi kuvuna maelfu ya watu zikabidhi mikononi mwa Mungu

Kwa sara zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatiu [ waefeso 6:18]

Basi kabla ya mambo yote nataka dua na sala na maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote [1timoth 2:1]
· Msogeze mbele za Mungu huyu dada aitwae mary ni mwanafunzi anaye soma kwa mateso makali kwa sababu ya kuathilika na ukimwi omba uponyaji na rehema za Mungu juu ya maisha yake anaishi mkoani Tanga fanya dua sara na maombi kwa ajili yake
· Msogeze mbele za Mungu huyu kaka aitwaye hebron anasoma chuo cha usafilishaji Dar Mungu afungue mrango wa ada kabla ya tar16 january si chini ya 2laki kw semister ya kwanza
· Ombea ndoa za watu walio okoka , kataa vurugu,mikosi ,omba hali nzuri za kiuchumi,kataa Roho ya matengano, panda upendo mpya , panda amani, utulivu, na hofu ya Mungu kwenye ndoa hizo
· Ombea vijana walioingia kwenye uchumba,Mungu awafanikishe, watunze utakatifu, mmoja asiwe jeraha kwa mwingine, omba safari njema mpaka siku ya ndoa,kataa mahusiano yanayosababisha vijana wengi watoke kwenye mpango wa Mungu
· Ombea mabinti waliojiingiza kwenye ukahaba tu kwa sababu ya kukosa msaada yaani ni yatima , au mafukara , hana msaada wowote , au vijana wakiume waliojiingiza kwenye uvutaji wa bangi , madawa ya kulevya, upolaji, ujambazi, na mambo mengineyo ambayo si ya haki mbele za Mungu, hawakupenda kufanya haya ila ni kwa sababu tu ya kukosa msaada wakafikili njia rahisi ni hiyo omba rehema za Mungu juu yao·

Kwa kusudi hili mwana wa Mungu alidhihilishwa apate kuzivunja kazi za ibilisi [1yoh 3:8b]
kataa Roho za mauti juu ya nchi na juu ya afrika mashaliki ikiwa ni pamoja na makafara, roho za ajali , miripuko ya magonjwa,umwagaji wa Damu na matambiko yanayoendelezwa na baadhi ya makabila nchini kitu ambacho kinapelekea laana juu ya nchi amuru hizo kazi za adui kuvunjika
kumbuka na huu ndio ujasiri tulio nao kwake ya kuwa tukiomba kitu sawa sawa na mapenzi yake atusikia [2 yoh 5;14]

Baada ya maombi haya unaweza kutuambia nini Mungu kafanya ukiwa na ushuhuda mistari ya kututia Moyo, au vitu fulai umevipata toka kwaMungu, ombea huduma hii mikoa yote ya Tanzania na Afrika mashariki, ombea waombaji wote wa huduma hii kumbuka kumuombea coordinator Tuntufye Andrew.

TAMASHA LA INJILI KWA NAMNA YA PEKEE ARUSHA

Kuwashirikisha Christina Shusho, Frola Mbasha, Jackson Bent pamoja na Kwaya nyingine.

Waimbaji wa muziki wa injili Christina shusho na Frola mbasha toka Dar es Salaam wanatarajiwa
kuhudhuria katika tamasha la injili linaloandaliwa na IRPAYAN O’ NGERA ORGANIZATION ambalo ni shirika la dini linalohudumia watoto yatima mkoani Arusha.

Akizungumza na afu hii ya MAONI NA SALA, Muandaaji wa Tamasha hilo Bw.Jemsi Losioky alisema kuwa tamasha hilo litakuwa maalum kwa ajili ya kuwasaidia watoto wanaoishi kwa matumaini wa kituo hicho.

Tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika jumapili ya tarehe 8/06/2008 kuanzia saa nane mchana katika Hotel ya Gorden Rose jijini Arusha litapambwa na wakali wa injili hapa nchini ambaye ni Frola Mbasha na Christina Shusho kutoka Dar es Salaam.

Wengine ni Jackson Bent wa Arusha, Marther J. mushi, Sauti ya Nyikani Band wote kutoka Kilimanjaro pamoja na waimbaji wengine ambao hawakutajwa kwa sasa.

Tiketi za tamasha hilo kwa sasa zinapatikana kituo cha Radio ya Kikristo ya Safina FM iliyoko Arsuaha, Kimahama Bookshop pamoja na Golden Roze Hoteli (Arcade Comference Centre)

Tamasha hili linategemewa kuwa ni la aina yake kutokana na matamasha ya aina hii kutofanyika mara kwa mara.

Kwa mawasiliano zaidi 0754202623 au 0715 629562

Friday, May 30, 2008

UNAVYOWEZA KUEPUKA LAANA NA VIFUNGO VYA NGUVU ZA GIZA

Ndugu yangu mpendwa ambaye Mungu amekupa neema ya kuweza kufuatilia mafundisho haya, ninakusalimu katika jina la Bwana wetu Yesu kristo, ninacho amini ni kuwa Roho mtakatifu ana kitu cha kufanya na maisha yako mara utakapokuwa ukiendelea kuufuatilia ujumbe huu, na pia utaweza kuwa msaada katika kuwavusha wengine ambao wamefungwa na ibilisi kwa namna moja au nyingine, yamkini hata pasipo ya wao kujua wako chini ya vifungo.
Ndugu msomaji unayefuatilia mafundisho haya si watu wengi leo wanaamini habari hizi za Laana, vifungo vya nguvu za giza, ikiwa ni pamoja na mambo ya uchawi na ushirikina, lakini pamoja na hayo yote bado ni wazi kabisa kuwa maelfu ya watu wamekuwa wakiishi maisha ya taabu na manyanyaso makali ya adui, sababu ikiwa ni Roho za giza zilizo wafunga na zinazofuatilia maisha ya wengi leo.

Na hii ndio sababu ya Yesu kuja duniani na kuitwa mkombozi, tena sehemu nyingine amejulikana kama mkombozi wa wanyonge, ikiwa na maana pia kuwa ni mkombozi wa walioonewa, walio kata tamaa, na wanaosumbuliwa na mateso ya ibilisi, wanaoishi maisha ya taabu na dhiki pamoja na maumivu yanayosababisha mateso makali, huzuni na vilio maishani, kumbuka hili ni la muhimu kwako kuwa Yesu hakuishia tu kutuokoa na dhambi zetu, isipokuwa pia alijishugulisha na kila jambo lililohusu maisha yetu, Afya zetu,mafanikio yetu,ikiwa ni pamoja na Roho zetu.
Na ndio sababu ukisoma katika ule waraka wa tatu ambao Paulo alikuwa akimuandikia Yohana {3 Yoh 1:2} anasema "Mpenzi naomba ufanikiwe katika mambo yote na kuwa na afya yako kama vile Roho yako ifanikiwavyo"
Ndugu yangu mpendwa, ni wazi kuwa watu wengi leo wamefanikiwa sana katika mambo ya Rohoni lakini si katika Afya zao, wala katika maisha, na imefikia hatua kana kwamba tumefikiria kuwa Bwana Yesu alikuja kushugulikia Roho zetu tu, kitu ambacho si kweli, Mtume Paulo alitamani kama ingeeleweka kuwa Bwana Yesu hakuishia tu Rohoni isipokuwa pia alijishugulisha kwenye biashara, Ofisini, shambani, kwenye mifugo, masomoni,na kwingineko kote kufanikiwe.
Ndio sababu ukiusoma huu mstari kwenye tafsiri mojawapo ya kingereza utakuta lile neno ufanikiwe katika mambo yote limeandikwa hivi "you may prosper in every things" sasa neno "prosper’ ukiliangalia tafsiri yake "to prosper is to be successful and become rich" yaani kuwa unayefanikiwa na hatimaye kuwa Tajiri, tafsiri nyingine "to prosper is to grow and develop in healthy way" yaani ni kuendelea kukuwa na kuwa na Afya iliyo salama .
Sasa hii ndio iliyo msukuma mtume Paulo kuandika kwenye huu waraka kuwa ninapojitaabisha kuomba, au ninapojitaabisha kufunga , kuutafuta uso wa Mungu kwa ajili yenu siku zote malengo Yangu na shauku yangu, na kiu yangu huwa inakuwa ni juu yenu kwamba Mungu awafanikishe kwenye mambo yote, sasa utakuta baada ya neno mambo yote anasema na kuwa na afya yako nini maana yake, kitu alichotamani waelewe ni kuwa Mungu asingeishia tu kuwafanikisha katika mambo yote isipokuwa baada ya kufanikiwa katika maeneo mengine bado Afya zao pia ziwe Salama.
Na anaposema kama Roho yako ifanikiwavyo maana yake ni kuwa Rohoni kulikuwa na mafanikio tayari, ambayo hakuyatilia shaka hayo, na ndio sababu ikawa Rahisi kutoa mfano kwamba vivyo hivyo mnavyoendelea kufanikiwa Rohoni, ndio vivyo hivyo natamani mfanikiwe katika mambo yote, ikiwa ni pamoja na Afya zenu.

Ndugu yangu mpendwa unaye fuatilia mafundisho haya ni vizuri ukatambua hili kuwa inawezekana kabisa wewe kama mtoto wa Mungu kufanikiwa kimaisha, kuwa na Afya iliyo salama na ukiendelea kumuishia Mungu siku zote za maisha yako hatimaye kuurithi uzima wa milele.
Na ndio sababu basi "tunaokolewa roho zetu, nafsi zetu, na miili yetu" Hii ndiyo iliyomlazimu Bwana Yesu kushuka kuzimu na kumpokonya shetani funguo za mauti ili aje atutangazie ushindi katika mambo yote tena hata dhidi ya mauti. Hivyo basi kilicho mfanya Bwana Yesu aje Duniani ni kutuokoa, na kutukomboa.
Ndugu msomaji kama Yesu alikuja kutuokoa au kutukomboa, hii ina maana kuna mahali tulikuwa mateka, au kunasehemu tulikuwa tumefungwa, na ndio sababu watu wengi leo wanaishi maisha ya taabu, vilio, kutofanikiwa ikiwa ni pamoja na manyanyaso ya Ibilisi sababu kubwa ikiwa ni vifungo na manyanyaso ya adui kitu kilichomfanya Bwana Yesu aingilie kati pale msalabani.
Hivyo basi ni muhimu ukalielewa hili kuwa Biblia inaposema Yesu alikuja kutuokoa ina maana kuwa kuna mahali ambako tusingeweza kujikwamua wenyewe kama nguvu ya Bwana Yesu haikuingilia kati.
Na Bwana Yesu aliidhihilisha hii yeye mwenyewe alipokifungua kitabu cha nabii Isaya maana alizungumza maneno ya matumaini kwa ajili ya kuwafungua watu waliofungwa na kuwaweka huru wanaoteswa na kuonewa na nguvu za ibilisi. .
{Isaya 61:1-2 } "Roho ya Bwana Mungu i juu yangu Kwa sababu Bwana amenitia mafuta niwahubiri wanyenyekevu habari njema; amenituma Ili kuwaganga walio vunjika moyo, kuwatangazia mateka uhuru wao, na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao; kutangaza mwaka wa Bwana uliokubaliwa na siku ya kisasi cha Mungu wetu; kuwafariji wote waliao."
Ni muhimu ukafahamu kuwa Biblia inapozungumzia habari ya kuwatangazia mateka uhuru wao hii ina maana kuwa kuna maelfu ya watu wametekwa na ibilisi kiasi ambacho hawawezi kuponyoka huko kabisa mpaka imetokea nguvu fulani kubwa zaidi ya kuwatoa huko, ambayo si nyingeneyo yoyote isipokuwa ya Bwana Yesu


Jambo muhimu,
Ningependa ufahamu kwamba pamoja na kuwa roho za giza zinasababisha; magonjwa, vilio, mauti, kutokufanikiwa, mateso makali na mengineyo mengi
Roho hizi pia zinasababisha watu waishi maisha ya dhambi, na wengi wao huja kupata ujasiri wa kuacha mambo mabaya waliyokuwa wakifanya hapo awali tu baada ya maombi ya ukombozi, na ndio sababu kuna roho kama za uzinzi,uasherati na ushirikina na zinazofanana na hizi, amabazo kama mtu anazo huwa hawezi kuacha tabia hiyo kwa kushauriwa, kuwekewa kikao cha ndugu na ukoo, kupewa adhabu kali, au kwa kuwekewa ulinzi mkali, hizi njia zote haziwezi kusaidia kwa sababu kuna Roho iko ndani yake ambayo ndiyo inayo mshurutisha mtu huyu kufanya hayo anayo yafanya.
Nilipata kusikia habali za kaka ambaye alikuwa anatozwa faini mpaka laki tano kwa sababu ametembea na wanafunzi wa sekondari, na jinsi ambavyo faini hiyo bado haikuweza kusaidia. Pamoja na kuwa ni pesa kubwa, sasa unafikiri ni kwa nini faini kubwa namna hii haikuweza kusaidia, sababu ni kuwa kilicho hitaji kushugulikiwa ni ile roho tu ya adui iliyokuweko kule ndani ya yule kaka. na si vinginevyo.
Mateka wa ibilisi huwa anatengenezewa kiu ya kufanya dhambi kama vile wewe unavyosikia kiu ya kunywa maji, kwa maana hiyo basi huwa hawezi kuwa na amani mpaka amefanya hiyo dhambi.
Mateka wakati wote hufanya anacho shurutishwa kufanya na pia huwa hana maamuzi yake mwenyewe na ndio sababu sehemu nyingine Biblia ikasema "wana macho lakini hawaoni wana masikio lakini hawasikii," sasa basi sababu kubwa huwa inatokana na kuwa mateka wa Ibilisi, maana wakati huo mtu huwa haoni ubaya wa kitu anachokifanya. Isipokuwa anapokuja kukombolewa ndio anaanza kujutia na kuona alikuwa anatenda dhambi, na anaanza kutambua madhara.
Nakumbuka baada ya kufundisha somo hili la ukombozi kwenye mji Fulani, Dada mmoja alikuja mbele akapiga magoti akalia sana kiasi kwamba ilinibidi kufuatilia nini kilikuwa tatizo, nilipopata nafasi ya kuongea na yule Dada akanieleza kwa machozi huku akilia sana kuwa alikuwa ametoka kutoa mimba mda si mrefu, na jinsi ambavyo haikuwa inamsumbua kiasi kwamba aliweza kuwa na ujasiri hata wa kuongoza baadhi ya vipindi kanisani kama kusifu na kuabudu kwa kiingereza tunaita {praise and worship}
Akaniambia, ulipokuwa unaendelea kufundisha nimesikia kuhukumiwa isivyo kawaida naona dhambi yangu inakuja mbele yangu naomba Yesu anisamehe akaendelea kulia sana, na akanieleza jinsi ambavyo kesho yake alikuwa anatakiwa akaongoze {praise and worship} kusifu na kuabudu kanisani kwao na jinsi ambavyo isingemletea shida.kama asingekuwa amekutana na Bwana Yesu saa hiyo, maana siku hiyo ilikuwa ni jumamosi.
Kitu nataka uone kwenye ushuhuda huu ni hiki kuwa unaweza ukawa mateka wa ibilisi na bado uko kanisani, na bado unafanya baadhi ya huduma.
Hebu tuangalie mstari huu "Na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao"
Ndugu msomaji, Biblia inapoelezea watu kufungwa, na juu ya ukombozi unaopatikana kwa njia ya Yesu kristo, hii ina maana vifungo hivyo ni vya ibilisi, na kama ni vya ibilisi basi viko chini ya utawala wa nguvu za giza, majeshi ya pepo wabaya ikiwa ni pamoja na mambo ya uchawi na ushirikina,
Hivyo basi Biblia inapozungumza habari ya watu waliofungwa wapate kufunguliwa, hii Ina maana wako watu wamefungwa chini ya utawala wa nguvu za giza katika ulimwengu wa Roho. Sasa ukifuatilia tafsiri ya kiingereza ule mstari unao sema na hao waliofungwa habari za kufunguliwa kwao utakuta anasema "and openining of the prison to those who are bound" maana yake ni kuwafungua vifungoni waliofungwa au kuwatoa magerezani waliofungwa, {wamefungwa wapi?} Kwenye magereza ya ulimwengu wa roho.{wamefungwa na nani} na Ibilisi.
Nini maana ya maisha ya vifungo au maisha ya kuwa gerezani
Maisha ya vifungo au maisha ya kuwa gerezani ni maisha ambayo mtu huwa anaishi kinyume cha neno la Bwana, ni rahisi kuishi maisha ya dhambi hata kama wakati mwingine huwa hapendi, hakuna kufanikiwa katika kila unalolifanya, ukifanikiwa hakuna amani, maisha yaliyotawaliwa na huzuni, ikiwa ni pamoja na mateso makali hakuna kusonga mbele kila siku kuwa kwenye eneo moja la maisha, kuwa na maisha yasiyo na tumaini, maisha yasiyo na furaha,
Hivyo basi maana halisi ya vifungo vya nguvu za giza ni kuwa huwa kunakuwa na roho za giza ambazo zinakuwa zimeshikilia maeneo fulani ya maisha yako, na kila siku hizi roho huwa zinakuwa ziko kazini kuhakikisha zinakuweka katika hali ya shida kutofanikiwa kiuchumi, kutokufanikiwa kiafya, wala katika jambo lolote unalohitaji kulifanikisha.
Wako watu ambao kila anapokaribia mafanikio Fulani ndio tatizo linakuja kutokea na kukwamisha mpango mzima wa mafanikio uliokuwa mbele yake lakini pia wapo watu ambao wakipata pesa tu. Au kazi Fulani ambayo ingemuingizia kipato, ndio matatizo yanatokea kwa mfululizo kiasi kwamba hawezi kufurahia tena mafanikio aliyoyapata sasa haya yote husababishwa na Roho za giza ambazo zinakuwepo kwa ajili ya kuhakikisha huyu mtu hufanikiwi.
Unaweza ukajiuliza swali hili,{Je ninaweza nikaamua leo kuondokana na vifungo hivi ?} Jibu Ndio; inawezekana kabisa maana hii ndiyo sababu iliyomfanya Bwana Yesu kuja hapa Duniani atuokoe na kutukomboa. Endelea kufuatana nami katika mfululizo huu}







Je nguvu za giza zipo?
wapo watu wachache ambao huwa hawaamini habari za utendaji wa nguvu za giza,. na wengine huamini kuwa wakisha okoka hawahusiki tena, na mambo yanayohusu nguvu za giza kitu ambacho si kweli, Je umeshawahi kujiuliza kwa nini Bwana Yesu kabla hajaondoka alituombea maombi haya Yoh 17 : 15 ‘Mimi siombi kwamba uwatoe ulimwenguni bali uwalinde na yule mwovu’ ikiwa Bwana Yesu aliomba tulindwe na yule mwovu, hii inamaana kuwa alijua fika utendaji wa ibilisi na jinsi amabavyo maisha yetu yalihitaji ulinzi wa Mungu usiku na mchana. Na ndio sababu ukisoma ule mstari wa 12 ‘a’ anasema ‘nilipokuwapo pamoja nao, mimi naliwalinda kwa jina lako ulilonipa nikawatunza,,,,,’ unaweza ukaona jinsi ambavyo Bwana Yesu aliona umuhimu wa sisi kutunzwa, au kulindwa na ndio sababu alipokuwa akiondoka akaomba kwamba tulindwe na yule mwovu, hii ina maana kuwa alikuwa akitambua fika vifungo na manyanyaso ya Adui ambayo yalikuwepo ulimwenguni na ukiendelea kusoma ule mstari wa ‘20’ utakuta akiwaombea na wengine watakao amini au watakao okoka baadae yaani wewe na mimi tulioamini leo hii.na wengine wanao endelea kuamini anaseama ‘Wala si hao tu ninao waombea ;lakini na wale watakao amini kwa sababu ya neno lao’
Ukisoma katika ‘ Waefeso 6 :12’ anasema ‘kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama ;bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya wakuu wa giza hili, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa Roho’ Mtume paulo alipokuwa akiandika walaka huu alitaka tufahamu kuwa kushindana kwatu, au kwa tafsiri nyingine tungeweza kusema kupambana kwetu si kwa vita za mwilini isipokuwa ni juu ya falme na mamlaka za giza, moja ya tafsiri za kiingereza imetafsili hivi ‘against powers’ maana yake dhidi ya nguvu mbalimbali za kuzimu falme za nguvu za giza inaweza kuwa na maana {Utawala wa ibilisi ambao chini yake kuna mapepo, majini pamoja na na vinyamukela vya kuzimu } huko ndiko tunakotakiwa kupeleka mashambulizi yatu, tena akaendelea kusema juu ya wakuu wa giza hili maana yake watawala wa giza { ambao ni wachawi, washirikina, na waganga wa kienyeji } akaendelea kuelezea jinsi amabvyo tunatakiwa kupambana dhidi ya majeshi ya pepo wabaya katika ulimwengu wa roho. Sasa akisema majeshi ya pepo wabaya uelewe hivyo hivyo majeshi maana kuna maelfu na maelfu ya mapepo ambayo yanafanya kazi usiku na mchana kuhakikisha yanavuruga mipango mizuri ya Mungu kwenye maisha ya watu
Sasa hii inaweza kukupa kuwa na hakika kuwa nguvu za giza zipo na kuwa unahitaji kujipanga kwa maombi kila wakati ili kukabiliana nazo.
`
Hivyo basi ni muhimu kuamini tu kuwa nguvu za giza zipo na zina nguvu na kuwa zinatenda kazi Duniani mchana na usiku na hii sasa ndio sababu kuna vitu vinaitwa [vifungo vya nguvu za giza} {maagano ya mizimu} mambo ya uchawi na ushirikina, watu kuhangaika na mambo ya kuagua ,kutambika mizimu, ibada za wafu, na mengineyo mengi
Na mambo haya ndiy’o yanayosababisha maisha ya vifungo kwenye maisha ya watu wengi
Nakumbuka nikiwa na fanya huduma ya ukombozi katika mkoa fulani na Dada mmoja aliyekuwa amepagawa na roho za giza, tukiwa katika maombi zile roho za giza zilianza kupiga kelele zikieleza ‘Mama yake alitukabidhi huyu tumtunze alipozaliwa , tumemuoa, ni mke wetu, huwa tunakuja saa nane usiku tunafanya nae tendo la ndoa, hatuwezi kumuacha tumetoka nae mbali {yaani hujawahi kuona roho za giza zikilia kwa uchungu na kumngangania mtu,} haikuwa rahisi sana maana huyu Dada alikuwa chini ya mikataba mikubwa ya nguvu za giza, alikabidhiwa na mama yake pasipo ya mama yake kujua, Asante kwa Yesu aliyetupa mamlaka yote Mbinguni na Duniani maana kwa jina lake yule binti alifunguliwa, ndugu unayefuatilia mafundisho haya tunapoendelea na mafundisho haya utazidi kujua namna watu wanavyoingia kwenye vifungo na jinsi unavyoweza kumuingiza mwingine pasipo ya wao kujua.
----Siku moja mara baada ya kufundisha somo hili katika kongamano la wanafunzi wa sekondari na vyuo Dada mmoja alinieleza jinsi alivyoanza kumpenda sana kaka fulani bila hata ya yeye kujua kwa nini alimpenda kiasi kile, anasema gafra alikuwa hawezi tena kusoma na kuelewa darasani, kiasi kwamba angekuwa teyari kufanya jambo lolote ambalo yule kaka angeamua walifanye, nikamuuliza kama aliwahi kuwa na urafi wowote na yule kaka akasema hapana isipokuwa siku moja walikutana kwenye kongamano fulani la vijana yule kaka alimsalimia yule Dada, na aliposalimiwa anasema hakukuwa na kitu chochote kilichotokea na kuwa hakuwahi kumfikili huyu kaka ila anasema, siku moja kuna nguvu ilimshukia gafra, akajikuta anamkumbuka sana na kumpenda isivyo kawaida ndipo nikamuuliza kama baada ya pale kuna kitu chocho aliwahi kupokea kwa yule kaka ndipo makasema kuna siku tu nilisha ngaa maana aliniletea picha yangu ambayo inaonyesha alinipiga ila sikumbuki alinipiga wapi nilipoipokea tu ndipo hali ilipozidi kuwa mabaya zaidi na baada kuichukua ile picha nilianza kuumwa na kitovu kwa nguvu, hii ni sehemu tu ya ushuhuda kitu nilitamani ukifahamu ni kuwa kama hutatambua kujifunika katiaka ulinzi wa Bwana Yesu kila wakati na kila mahali ni rahisi tu kukamatwa, baadae tukatambua kuwa huyu kaka alipiga hii picha bila huyu Dada kujua na kuipeleka kwa wakuu wa giza ili aweze kumpata kwa kutumia madawa maana yule bint alionekana kuwa na misimamo Ashukuliwe yesu aliye mfungua binti huyu
Kumbuka hili siku zote jitahidi kukaa mkao wa kujilinda kila wakati maana unahitaji msaada wa Mungu siku zote usiku na mchana Biblia imesema wazi kabisa 1yoh 5 :18 ‘twajua ya kuwa kila aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, bali yeye aliyezaliwa na Mungu hujilinda’ wala yule mwovu hamgusi.
Ni muhimu ukafahamu kuwa unahitaji kujilinda kwa maombi kwa kulisoma neno kwa kukaa makao wa kumuhofu Mungu kila wakati hii itamfanya adui asipate nafasi kwenye maisha yako na ndio sababu Biblia ikasema Yakobo 4 :7 ‘Basi mtiini Mungu. mpingeni Shetani, nae atawakimbia ninyi’ sasa basi kule kumtii Mungu, kutembea na hofu ya Mungu ndiko kunakokutengenezea imani na ujasiri wa kumpinga shetani kwenye eneo lolote la maisha yako nae akukimbie, maana watu wengi leo wameishi maisha ya vifungo tu kwa sababu ya utumwa wa dhambi, na ndio sababu Biblia ikasema 1yoh 5 :14 ‘Na huu ndio ujasiri tulionao kwake ya kuwa tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake,atusikia,,,,,,’ sasa waweza kujiuliza swali kuwa ni kwa nini akaanza na huu ndio ujasiri tulionao kwake, hii ina maana ya kuwa huwezi ukawa na ujasiri wa kusimamia Nguvu za Mungu katika kumpinga ibilisi kama hauja kaa kwa Mungu kwa miguu yote miwili



JE MTU ALIYEOKOKA ANAWEZA AKAVAMIWA NA ROHO ZA GIZA ??? NA HATA KUWA CHINI YA VIFUNGO, NA INAWEZEKANAJE NA HALI YESU ALIMALIZA YOTE MSALABANI.
Ndugu mpendwa unayefuatilia mafundisho haya, kila mahali ambako Mungu amenipa neema ya kufundisha masomo haya ya ukombozi nimekuwa nikiulizwa hili swali.na inawezekana hata wewe unashauku ya kujua mengi kuhusiana na hili,
Mpendwa unayefuatilia mafundisho haya, ni kweli kabisa kuwa hata mtu aliyeokoka anaweza akavamiwa na roho za giza.
Na zika athiri mambo yake, kama biashara yake, uchumi wake, ndoa yake na hata maisha yake kwa ujumla na bado akawa anaenda kanisani, anaomba, anaimba, na kufanya baadhi ya mambo,
Kumbuka adui mkubwa wa ibilisi ni yule aliyempokea kristo, na ndio maana wakati mwingine kuokoka kumetamkwa kama kutangaza vita, mtu aliyeokoka anafananishwa na mtu ambae yuko vitani na kuwa amezungukwa na maadui kila mahali, na kila adui anatamani kama angelimmaliza yeye maana anasababisha matatizo makubwa kwenye ufalme wa adui bila ya yeye kujua.
Watu wengi kwa sababu ya kutokuyasoma maandiko hudhani ya kwamba kuokoka ni kumaliza kila kitu ikiwa ni pamoja na uhakika wa kufika mbinguni na kumbe kuokoka ni kuanza safari ya maisha mapya katika ulimwengu wa mapambano, na ndio sababu Biblia ikasema katika 2kor 10 :12 kwamba ‘kwa hiyo anayejidhania kuwa amesimama na aangalie asianguke, sasa ukiufuatilia huu mstari utagundua Biblia inatutaka tuwe waangalifu, maana Adui ni kama simba aungurumae anaye tafuta mtu apate kummeza, wakati huo huo ukisoma Yakob 4 :7 utakuta anasema ‘basi mtiini Mungu mpingeni shetani nae atawakimbia’ sasa kwa nini Biblia inakutaka umpinge shetani ndipo nakukimbie, hii ina maana usipompinga atakukimbilia wewe.
Ulinzi wa Mungu unakuwa juu ya mtu, tu pale anapokuwa Hodari katika Bwana huku akiutafuta uweza na nguvu zake, Efeso 6 :10 ‘Hatimae mpate kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake’
Nini maana ya kuwa hodari katika Bwana, huku ni kukaa kwenye maombi, kuwa na neno la Mungu ndani yako, kujifunza kuutafuta uso wa Mungu kwenye maeneo Mbalimbali ya maisha yako, kwa kadiri utakavyokuwa ukiendelea katika hali hii ndivyo utakavyo kuwa ukiuona uweza na nguvu za Mungu kwenye maisha yako ukiendelea mstari wa 11 utakuta anasema ‘vaeni siraha zote za Mungu mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani’ sasa hii inakupa kujua kuwa unatakiwa kupingana na hila za shetani kila siku maishani mwako na hauwezi ukazipinga tu hivi hivi ni mpaka umevaa siraha zote za Mungu, ikiwa ni pamoja na neno la Mungu kujaa kwa wingi ndani yako, kuwa muombaji, na kweli ya Mungu kuwa kwenye maisha yako,



Hii inaweza kuwa moja ya mirango ya adui kwa mtu aliye okoka
Fitina, kule kumfitini mtu au kumsengenya mtu na hauoni shida kufanya hayo, na kule kushindwa kabisa kumtoa mtu moyoni mwako,kushindwa kuachilia,kusamehe, kuendeleza kinyongo, kuacha uchungu uendelee kujaa ndani yako inaweza ikampa ibilisi mrango na ukavamiwa na roho za giza, maana ukiwa kwenye hali hii huna mda wa kuomba, ila unamda wa kulaumu na kunungunika, ikiwa ni pamoja na kujisemea vibaya au kumsemea mwingine.
Kiburi, kule kujaa kiburi na ukaidi, kutokutaka kusikiliza ushauri, kuwaona wengine wote hawana kitu isipokuwa wewe au fulani, na hivyo kutokunyenyekea, wala kushuka kitu ambacho kimesababisha roho za ukengeufu kwa watu wengi leo{uasi} hii imesababisha mirango kwa nguvu za giza.
Tendo la ndoa kabla ya ndoa, au nje ya ndoa kumbuka mtu anapoamua kutoa nguo zake kwa mtu amabaye si mke wake halali, kwa tafsiri ya rohoni anautoa utukufu wa Mungu, au anauvua, hivyo basi anauvua ulinzi, na kwa sababu hiyo Roho za giza zinakuwa na nafasi kubwa ya kuweza kumvaa mtu huyu
Na ndio sababu watoto wa kuhani heli Hofsini na Finehasi walipofanya uzinzi na wanawake waliokuwa wakitumika malangoni pa hema ya kukutania, utukufu wa Mungu uliondoka, na ulinzi wa Bwana ukaondoka na lile sanduku la agano likatekwa, habari hizi utazipata vizuri samweli wa kwanza na kuanzia sura ya pili, kitu nilitaka uone ni jinsi ambavyo utukufu wa Mungu ukiondoka juu ya mtu na ulinzi wa Mungu ukiondoka kwa sababu ya dhambi uwezekano wa mtu kuvamiwa na aroho za giza unakuwa ni mkubwa zaidi.
Kukata tamaa ile hali ya kujikatia tamaa, kuvunjika moyo, kupoteza kabisa matumaini hata kujisemea maneno ya laana, inafungua mirango kwa roho za giza kuvamia maisha yako. Ndio sababu Biblia ikasema Filip 4 :6 msijisumbue kwa neno lolote ; Bali katika kila neno kwa kusali na kuomba, pamoja na kushukuru, haja zenu na zijulikane na Mungu. sasa kule kulaumu kulalamika, kujilaani haja zako zinajulikana na mapepo na sio Mungu. Iyo ndio inayompa adui nafasi kwenye maisha ya watu wengi leo.
MOJA YA MAMBO YALIYO SABABISHA MAELFU YA WATU WA AINA MBALIMBALI KUINGIA KWENYE VIFUNGO VYA NGUVU ZA GIZA

Kwa kurithi watoto wengi wanao zaliwa kwenye familia ambazo kuna mambo ya uchawi au wanaabudu mizimu na kufanya mambo ya matambiko huwa wanatolewa kwa pepo au mizimu wangali bado wadogo kadri wanavyoendelea kukua ndivyo wanavyoendelea kuona kama mambo yanayo fanyika ni sahemu halali kwa maisha yao. Nakumbuka safari moja tukiwa kilimanjaro tulifanya huduma na kijana mmoja wa kidato cha pili aliyekuwa amefungwa na nguvu za giza , na tukiwa tunafanya nae maombi alitapika vitu fulani vyeupe vya kushangaza sana. Baada ya kufunguliwa na Bwana Yesu na yale mapepo kumuachia tukapata nafasi ya kukaa nae na kuzungumza nae, alitueleza kuwa yeye ni mtoto wa kwanza kuzaliwa kwenye familia yao na kuwa amekuwa akipelekwa kwenye makaburi na kufanya matambiko na wazazi wake kuanzia akiwa mdogo na akaeleza kuwa alikuwa akilishwa vyakula kama nyama za aina fulani kila alipofika makaburini kwa tambiko, sasa hii ina maana kama Bwana Yesu asinge mfungua angeendelea kuishi maisha ya ushirikina chini ya utawala wa nguvu za giza.namna watoto wanavyoingizwa kwenye vifungowazazi wengi wasio amini huwaingiza watoto wao kwenye vifungo vya ushirikina bila ya wao kujua. watoto wengi wakizaliwa hupelekwa kuchanjwa chale, kwa waganga wa kienyeji au wengine hupelekwa kwa Bibi zao kwa ajili ya mambo fulani ya kimira kama kuzika kitovu, kwa taratibu za kimila, kupewa jina chini ya taratibu za kiganga, z po sara mtoto anaombewa kwa babu zake waliokufa wakati mwingine hizi sara hufanyika makaburini ‘mfano wa sara inayoombwa { mtoto wenu amekuja, mumkumbuke, mumsaidie, tunawakabidhi ni wa kwenu, maneno mengi sana yanatamkwa mara nyngi nkuwa kwa kiluga bila hata ya wao kujua ni nini wanafanya katika ulimwengu wa roho, kumbe katika ulimwengu wa roho yule mtoto anakabidhiwa chini ya falme na mamlaka za giza}Na ndio sababu ukisoma Kumb 18 :10 utakuta anasema Asionekane kwako mtu ampitishaye mwanawe au Binti yake kati ya moto’ ukiendelea mbele kidogo utakuta anasema ‘wala asionekane mtu aombae wafu sasa u mstari 12a utakuta anasema ‘kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa Bwana’Wakati fulani tukiwa na huduma mkoa wa Tanga nilipata nafasi ya kupita mitaani watu wanako ishi asilimia kubwa ya watoto nilio waona walikuwa wamevishwa Hirizi, na vitambaa vyeusi mikononi, shingoni,kwenye miguu wengine walikuwa wamevishwa shanga viunoni, japo hii aina maana mambo haya yako huko tu isipokuwa niliguswa sana nikiwa huko cha kushangaza leo hii hata wakristo wengi wamevalisha watoto wao hivyo vitu, wengine ukiwauliza hata yeye mzazi hajui kwa nini kamvalisha mtoto hicho kitambaa cheusi wengine ukiwauliza atakuambia Bibi yake alimvalisha .
kwa kushiriki mambo ya uchawi na ushirikina wapo wakristo wengi leo hii ambao kwa namna moja ama nyingine wamekuwa wakijihusisha na mambo ya uchawi na ushirikina bila ya wao kujua mfano kuchangia tambiko, kuhudhuria ibada za wafu, kula nyama za kusongolewa, kunyoa nywele kwa ajili ya aliyekufa, kunywa dawa za kimila, kwenye misiba mingi ambayo watu huamini mambo ya ushirikina huwa wanakunywa Dawa wanafamilia au ukoo mara baada ya mazishi au msiba kuisha . lakini
Biblia imesema wazi kabisa kuwa ‘msishiriki ibada zao’ na ukisoma katika Kumb 14 :1 utakuta anasema ‘msifanye upaa kwa ajili ya aliye kufa.’ Sasa ni muhimu ukafahamu kuwa haya ni moja ya mambo yanayoingiza maelfu ya watu kwenye vifungo
3. wapo waliopata watoto kwa njia za ushirikina
Wapo wanawake ambao baada ya kutafuta watoto kwa mda mrefu bila mafanikio wakaamua kutafuta kwa njia za ushirikina, wengine walilishwa madawa ya kienyeji ili apate mimba, wengine walilazimika kufanya tendo la ndoa na waganga wa kienyeji, wengine walienda kulala juu ya makaburi, na mambo mengine mengi hakuna hata muda wa kutosha kuelezea kila kitu, kitu nataka ufahamu ni hiki kuwa huyo mtoto aliyepatikana kwa namna ya uchawi na ushirikina ni lazima tu awe chini ya utawala wa Nguvu za giza {kwenye vifungo} {maana agano la kupatikana kwake lilifanyioka wakati wa kutungwa mimba} yaani mimba ilipokuwa inatafutwa. Na mara zote mtoto wa namna hii kuwa na tabia za tofauti huwa na uwezo wa kuona vitu vya tofauti, maana roho za giza zina hati miliki juu yake,
4. Kukubari huduma za kishirikina
Wapo watu ambao walipoibiwa tu wakashauliwa kwenda kuagua kitu ambacho ni chukizo mbele za Bwana Kumb 18:10b ‘Wala asionekane mtu atazamae bao,,,,’ ukiendelea mbele kidogo utakuta
anasema ‘wala mwenye kubashiri, wala mshihiri, Wala mtu alogae kwa kupiga ufundo shida ni hii kuwa wapo wakristo wengi sana leo wanao muhuzunisha Bwana kwa kushiriki au kukubariana na huduma za kishirikina na wakati huo huo wanamuabudu Mungu, wakristo wengi leo wamependa mambo ya Unajimu kwa mfano Unajimu wa Nyota, matumizi ya vitu mbalimbali kama karata, kubashiria bahati kupiga ramli, kutegua tego,
5. kuzindika nyumba
Wapo watu wengi leo walio danganywa kuwa kuna kuweka ulinzi kwenye nyumba zao Hivyo wakaruhusu waganga kuja kuchimbia vitu Fulani kwenye Nyumba zao na matokeo yake huwa inakuwa ni kupuputika kwa familia ikiwa ni pamoja na kukaribisha magonjwa na mikosi kwenye familia, ikiwa ni pamoja na vilio visivyoisha, maana mnaikabidhi ardi yenu chini ya utawala wa nguvu za giza, sasa kwenye kitabu changu cha kwanza kijulikanacho kama {PAMBAMBANA DHIDI YA NGUVU ZA GIZA}nilipokuwa natoa utangulizi wa masomo haya nilitoa ushuhuda jinsi tulivyo fanya huduma ya kufukua mazindiko kwenye familia Fulani maana familia iligeuka maali pa maombolezo, mtoto wa kwanza na wa pili walikufa katika hali ya kutatanisha mtoto wa tatu akawa yuko taabani, ukimtazama mama yake hajiwezi kwa ugonjwa ndipo mzee mwenye nyumba akakumbuka agano la ardi yake na mapepo, nakumbuka
Tulipomaliza kufukua mahali palipo chimbiwa tulikuta vitu vya ajabu kweli,lakini ninachotaka ujue ni kuwa mara baada ya kufukua vitu vilivyo chimbiwa zaidi ya miaka kumi iliyopita tulivichoma moto, na familia yote wakaamua kumpa Bwana maisha kuanzia pale, yule mgonjwa waliyekuwa wakitegemea angekufa mda wowote na kukamilisha idadi ya watoto watatu kufa maana alikuwa mahututi, alipokea uzima toka kwa Bwana Yesu, mpaka leo hii nikienda kwenye ule mkoa namkuta akiimba kwaya ya vijana kanisani kwao. mateso na vilio vikaondoka.kitu nilitamani uone ni hiki kuwa Bwana asipoulinda mji yeye alindae akesha bure,
USICHANGANYE NGUVU ZA MUNGU NA SHETANI NI HATARI
acha kumchanganya Mungu kabisa, maana utakufa. ukiamua kumtegemea Bwana Yesu, mtegemee yeye kwa asilimia mia moja na si vinginevyo maana wapo wanaopenda kuchanganya nguvu za Mungu na za Ibilisi kumbuka hilo ni kosa kubwa na Nyuma yake kuna laana na mauti utaishia kufa kifo kibaya na aibu yako itajulikana..maana ukisoma Kumbukumbu la torati 28:4 -13 utaona Mungu akitoa Baraka ikiwa watu watamtegemea na kumuamini yeye peke yake, anaanza na kuzungumza habari za uzao wa tombo lako utakavyobarikiwa, anazungunza habari za adui zako kupigwa na kuanguka mbele yako, na jinsi ambavyo kila utakalo lifanya litabarikiwa, ameeleza mambo mengi sana ambayo anatamani yafanyike Baraka kwenye maisha yako, endapo utatii na kufuata maagizo yake, Lakini ukisoma ule mstari wa 14 anasema "msipogeuka katika maneno niwaamuruyo leo kwa lolote, kwenda mkono wa kuume wala wa kushoto, kwa kuifuata miungu mingine na kuitumikia." Sasa lile neno msipogeuka kwa tafsiri nyingine msiponiacha na kufuata mambo ya ushirikina{miungu mingine} maana ni rahisi sana kudanganywa kuwa uko msaada kwenye uchawi, na mambo ya ushirikina lakini nataka ujue wazi leo hii kuwa, huko ni kijitafutia laana na mauti yako mwenyewe. Maana hakuna kitu Mungu anapingana nacho kama sisi kumchanganya yeye na miungu mingine.
Na ndio sababu ukisoma ule mtari wa 15 anasema ‘lakini itakuwa usipotaka kuisikiliza ile sauti ya BWANA, Mungu wako, usiyaangalie kufanya maagizo yake yote na amri zake, nikuagizazo hivi leo, ndipo zitakapokujia laana hizi zote na kukupata’. Ukiendelea mbele kidogo anaelezea hizo laana mstari wa 16 utalaaniwa mjini, utalaaniwa na mashambani. litalaaniwa kapu lako na chombo cha kukandia {kapu lako : {kwa tafsiri nyingine utalaaniwa uchumi wako}anaendelea ‘BWANA atakuletea laana na mashaka, na kukemewa katika yote utakayotia mkono wako kufanya, hata uangamie na kupotea upesi’ {kumbuka sio mapepo, ila Bwana atafanya } na ndio sababu kuna wakati shida yako inaweza ikaombewa na kila mtumishi na isipatiwe ufumbuzi isipokuwa ni mpaka Mungu atakapokuja kumpa mtumishi mwingine neno la maarifa juu ya dhambi yako na kwamba uondoke kwenye maagano ya ushirikina uliko ndipo uvumbuzi wa shida yako utakapotokea, na ndio sababu ni bora uwe na uadui na shetani Mungu atakusaidia, kuliko ukawa na uadui na Mungu hii ni hatari kubwa maana hatakuwepo wa kukusaidia.
Ukisoma ule mstsri wa 28 anasema ‘BWANA atakupiga kwa wazimu, na kwa upofu na kwa bumbuazi la moyoni utakwenda kwa kupapasa papasa mchana,kama apapasavyo kipofu gizani wala hufanikiwi katika njia zako ; nawe siku zote utaonewa na kutekwa nyara, wala hapatakuwa na mtu wa kukuokoa.’ Sasa ukiendelea mbele kidogo utaona jinsi ambavyo utachumbia mke na mtu mwingine atalala nae {watamchukuwa} na mambo mengine mengi ambayo yatakupata tu kwa sababu umeabudu miungu mingine. Na kama hayo mambo hayajakupata wewe hata ikiwa yamekupata kwa sehemu, basi uwe na uhakika watoto wako watarithi mateso ya dhambi yako. Maana Mungu hupatiliza maovu, alihaidi kupatiliza maovu ya Baba kwa mwana, ukisoma { Kutoka 20 :4 anasema ‘usijifanyie sanamu ya kuchonga, wala mfano wa kitu kilicho juu mbinguni, wala kilicho majini chini ya Dunia ; Usivisujudie wala kuvitumikia kwa kuwa mimi, BWANA, Mungu wako, ni Mungu mwenye wivu ; nawapatiliza wana maovu ya baba zao, hata kizazi cha tatu na cha nne cha wanichukiao,’
Sasa Mungu ameshasema kuwa wana watapatilizwa maovu ya Baba zao tu kwa sababu Baba zao waliabudu miungu mingine. Ili kuepuka mambo haya yote usimchanganye Mungu maana kuna watu leo wanaenda makanisani na bado wanairizi, bado wanashiriki mambo ya giza, bado wanashiriki mambo ya jadi na mila, hivyo basi ni muhimu sana ukawa na maamuzi ya kumtumikia Mungu peke yake na si vinginevyo

Mambo yanayotokea nyumba inapokuwa imezindikwa
Nyumba ikizikilicndikwa maana yake imekabidhiwa kwa pepo kwa tafsiri nyingine watoto wanakuwa wamekabidhiwa pia maana ni sehemu ya familia, miradi inakuwa imekabidhiwa pia biashara, ndoa, pamoja na kazi, hii ni hatari sana, na watu wengi sana wanaoishi kwenye Nyumba za kupanga zilizozindikwa huwa wanapata shida sana ya mapambano na roho za giza mara kwa mara wachache huwa wanapewa macho ya rohoni kujua kuwa ziko falme mbili zinapambana mahali hapo.Biblia inaposema katika {Yoshua 1:3 } kila mahali zitakapo kanyaga nyayo za miguu yenu nimewapa,
haina maana ufike tu hotelini au nyumba ya wageni na kulala tu, au uamie tu kwenye Nyumba na kuanza kuishi bila kufanya chochote au uinmgie kwenye basi na kustare kama abiria wengine hiyo naifananisha na imani pasipo matendo maana kwa tafsiri halisi wewe mtoto wa Mungu kupewa kila mahali nyayo za miguu yako zinapokanyaga ni kupateka mahali hapo na kuvuinja falme zingine zilizokuwa zinatawala na kuupanda ufalme wa Mungu na ndio sababu Mungu alimwambia Yeremia kitu alichotakiwa kufanya ukisoma Yeremia 1:10 anasema ‘Angalia nimekuweka leo juu ya mataifa na juu ya falme’ kwa tafsiri nyingine nimekupa mataifa nimekupa na falme utawale ukiendelea pale mbele utakuta anasema ili….. sasa neno ili linatafsiliwa kama sababu, sasa ni sababu ipi ya M ungu kumuweka Yeremia juu ya mataifa na juu ya falme utakuta Mungu alikuwa na lengo la kungoa, na kubomoa, na kuharibu kazi za ibilisi alafu aujenge na kuupanda ufalme wa kwake. Hivyo basi mambo haya ambayo mungu aliyatarajia yalitegemea sana uelewa wa Yeremia kwa habari ya yeye kuwekwa juu ya mataifa na juu ya falme.

6. matumizi ya hirizi na baadhi ya vifaa vya ushirikina
Maelfu ya watu leo wameingia kwenye vifungo kwa sababu walikubari kupokea hirizi na wengi wao wanazitumia kwa siri wakifikili kuna ulinzi na usalama kumbe ni kujiingiza kwenye mikataba ya nguvu za giza,wako wengine ambao wameziweka kwenye Magari yao, wengine kwenye vitanda vyao, wengine wameshonea kwenye nguo zao, ilimradi tuu isionekane, ni muhimu kufahamu kuwa Mungu wetu yu kinyume cha Irizi ukisoma Ezekiel 13:20 anasema ‘ Basi Bwana Mungu asema hivi mimi ni kinyume cha Irizi zenu…….’ Sasa ukianzia pale mwanzo kidogo utakuta anatoa ole, kwa wanawake wanao shona irizi.. na utaona jinsi ambavyo matumizi ya irizi ni kwa ajiri ya kuondoa Roho za watu kishirikina. Na ndio sababu Biblia ikasema watu wangu wanaangamia kwa kukosa maarifa. Maana yake ni kuwa hawana ufahamu,juu ya mambo wanayoyafanya na ndio sababu maelfu ya watu wameingia au wameingizwa kwenye vifungo vya ibilisi wakidhani wanatafuta ulinzi,usalama,amani,furaha,maisha mema, na matokeo yake kuwa vilio na majuto.

Je kuhusu shanga bangili na mikufu

Ni kweli kabisa kuwa wapo watu wengi leo wanaopenda kutumia vitu vya ulembo kama Shanga, maana zipo zinazotengenezwa kwa mfumo wa kuvaa hata wanaume pia, mfano ni zile za mikononi, na wapo wanawake wanaopenda kuvaa zile za kiunoni, mikufu, bangiri, pete, mapambo ya ndani kama vinyago na vibuyu, ni muhimu sana kuwa makini hapa maana kwenye ulimwengu huu wa utandawazi kila kitu huonekana kuwa ni cha muhimu na chenye thamani kwa Binadam.
Ni katika ulimwengu huu tunaoishi tunapotakiwa kuwa makini sana na kila chaguo la jambo tunalotaka kufanya kama wacha Mungu, na si tu kufanya kwa sababu wengine wamefanya, tunahitaji kuwa na macho ya rohoni hasa tunapofanya maamuzi ya maisha na mambo ambayo tungetamani yaambatane na maisha yetu, kuna kitu kiaitwa macho ya rohoni tunahitaji kuwa na macho ya rohoni ili kuepukana na vitu amabavyo miili yetu inaweza ikavutiwa navyo pasipo ufahamu wa mambo ya rohoni ikawa ndio tunapelekwa kwenye vifungo

Biblia inaposema katika {Kor 3 :15} kuwa ‘na amani ya kristo iamue mioyoni mwenu….’ Maana yake ni hii kuwa anayeleta amani ya kristo mioyoni mwetu ni roho mtakatifu peke yake , sasa kwa nini akasema amani inayotakiwa iamue mioyoni mwenu ni ya kristo hii ina maana zipo amani nyingine zinazoweza zikaamua moyoni mwako na matokeo yake zikasababisha mambo magumu sana kwenye maisha yako, ikiwa ni pamoja na milango kwa adui,
Sasa ni muhimu kutambua kuwa ni wajibu wa Roho mtakatifu kuamua kwa niaba yetu, kwani ndie kiongozi wetu, msaidizi na mwalimu wetu. lakini asipopewa nafasi kwenye maisha yetu hukaa pembeni akihuzunika kwani hawezi kukulazimisha kufanya jambo, ‘Efeso 4:30 wala msimuhuzunishe yule Roho mtakatifu wa Mungu,ambaye kwa yeye mlitiwa mihuri hata siku ya ukombozi’ na sehemu nyingine ya Biblia inaonyesha jinsi ambavyo Roho hututamani kiasi cha kuona wivu yaani huwa anatamani kama angeamua kwa niaba yetu, angefanya kila kitu kwa niaba yetu, sasa kwa sababu maisha yetu hayana nafasi ya Roho mtakatifu kufanya kwa niaba yetu ndio sababu tunashindwa kuyafahamu mambo ya rohoni, na mipango ya Adui iliyo katika siri kubwa kuharibu maisha Yetu. na ndio sababu pia ukisoma Rumi 8 :26a anasema ‘kadharika Roho nae hutusaidia udhaifu wetu, miili yetu ina madhaifu mengi sana, mfano tamaa, tunatamani kila kitu hata bila kujiuliza maswali wakati mwingine, wala kutafuta maana ya hicho kitu ni nini, hata kuna baadhi ya vitu tumejiingiza kwavyo tu kwa sababu labda ukifanya ndio unaonekana wa kisasa zaidi, sio vibaya kuonekana wa kisasa isipokuwa swali la kujiuliza ni je ninaliolifanya au ninalotaka kulifanya linampa Mungu utukufu ? na je Adui hawezi akapata nafasi kwa njia hii ? korosai 3 :17 ‘Na kila mfanyalo kwa neno au kwa tendo fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu’ maana yake ni hii kila unalolitamka kinywani mwako au muonekano wako au unalolitenda, limtangaze kristo, limdhihilishe kristo, limfanye kristo apate utukufu. Kitu ambacho si rahisi kama Roho mtakatifu ajapata nafasi ya kwanza kwenye maisha yako,
Sasa ukiunganisha na mapungufu tuliyo nayo inampa ibilisi milango ya uvamizi kwenye maisha
yetu
Yapo mambo mengi ambayo kwa hayo tunakuwa tumejiingiza kwenye vifungo bila ya sisi kujua ukielewa kitu cha namna hii hautaacha kumpa Roho mtakatifu nafasi ya kwanza katika kuamua mambo yako na kuhakikisha kuwa inayoamua ndani yako ni amani ya kristo.
mambo mengine yanayokupa ulazima wa kuhakikisha anayeamua moyoni mwako ni ni Roho mtakatifu
kujua fikra za ibilisi 2korinto 2 :11 ‘shetani asije akapata kutushinda kwa maana hatukosi kuzijua fikra zake’ fikra zake ni mipango yake ya uharibifu juu ya maisha yako sasa ili asikushinde ni lazima uzijue kwanza fikra zake, mbinu zake za uharibifu,na jinsi anavyotaka kukuingiza kwenye vifungo upo msemo wa kiswahili usemao { kumjua adui ni nusu ya kumshinda} sasa basi ile tu kujua kuwa kwa kufanya hili nitakuwa nimempa ibilisi nafasi na hivyo kutokufanya ni kumshida Adui teyariUshuhudanikiwa nafanya huduma hii ya kufunguliwa katika mkoa fulani yupo binti ambae alikuwa amepagawa na Roho za giza, sasa Baada ya kufunguliwa na bwana yesu nilipata nafasi ya kuzungumza naye na kutaka kujua iyo shida ilianzaje, alieleza kuwa siku moja ya jumamosi alipewa rifti na watu asiowajua lakini walidai kuelekea alikokuwa akielekea yeye,Anasema akiwa kwenye gari alipewa Biskuti na hakuona haja ya kukataa, kwa sababu ilikuwa ni biskuti tu, anasema walipo mshusha tu alipotakiwa kushuka gafra akasikia kutapika na alipotapika zilikuwa ni nywele za binadamu, alic`hanganyikiwa hakuelewa nini. Na kuanzia hapoalianza kujisikia vibaya mwilini na vitu vya ajabua vikaanza kutokea kwenye maisha yake,Anasema kuna wakati akawa anajikuta anatamani tu kukaa uchi, bila nguo watu wote wakiondoka ndania anafunga milango yote anavua nguo zote, alinieleza mambo mengi sana ya ajabu, kitu nilitaka uone ni hiki kuwa milango ya adui ilikuwa ni kwenye ile Taxi na zile biskuti, sasa sisemi usipande taxi wala usipokee vitu isipokuwa Roho mtakatiifu aamue kwa niaba yako,Shida ni hii kuwa kama Roho wa Mungu hachukui nafasi ya kwanza kwenye maisha yako hutaweza kabisa kuzijua fikra za Ibilisi kwenye maisha yako na hatimae kujikuta uko katikati ya vifungo vya adui.
Miitego ya ibilisiZab 91 :3 ‘Maana yeye atakuokoa na mtego wa mwindaji na katika tauni iharibuyo’ ndugu unayefuatilia mafundisho haya ni muhimu ukatambua kuwa kuna mitego mingi sana ya ibilisi kila siku kwenye maisha yetu, mitego ambayo unatakiwa kuitegua kwa neno la Mungu ,maombi na kwa kuongozwa na Roho mtakatifu katika kila unalolifanya.na ndio sababu Biblia ikasema msimpe ibilisi nafasi maana yake ni kuwa jambo lolote utalolifanya bila msaada wa Roho mtakatifu linaweza likampa ibilisi mlango wa kukuingiza kwenye vifungo maana anatutafuta usiku na mchana Biblia inaonyesha wazi kabisa kuwa anawashitaki wateule wa Mungu mchana na usiku, na pia ni kama Simba aungurumae anawatafuta wateule awameze, Hebu fikiria kama katika kila masaa 24 kwenye kila sekunde inayopita kuna mtego wa ibilisi unakutafuta, wewe unajipangaje au umejipangaje.Na mitego yote ya ibilisi ina lengo la kuwaingiza watu kwenye vifungo vya nguvu za giza na kuwabana mahali ambapo watendelea kunyanyasika,.na hii ndio sababu unatakiwa kujifunza kuwa mtu wa rohoni maana Roho wa Bwana atakuongoza katika kila unalolifanya, na kukuepusha na mitego ya ibilisi.na kukupa macho ya rohoni kujua nini upokee na nini usipokee, nini ufanye na nini usifanye, wapi uende wapi usiende, je kuna ulazima wa kushiriki hayo mazungumzo au hakuna ulazima, je ununue iyo bidhaa ya mamna iyo au usinunue, je ununue leo au kesho, je uupokee huo ushauri au usiupokee, je uvae iyo nguo kwenye hicho kikao au uvae nyingine, hii itakusaidia sana kutoishi maisha ya kawaida na kuepukana na mitego ya ibilisi.Na ndio sababu Biblia ikasema katika 1korinto 2 :15 ‘Lakini mtu wa Rohoni huyatambua yote, wala yeye atambuliwi na mtu’ mtu wa rohoni ni nani ni Yule aliyempokea Bwana Yesu na anayeongozwa na Roho mtakatifu, hivyo roho mtakatifu kumpa nafasi ya kujua mambo mbalimabali yanayoendelea katika ulimwengu wa Roho, Amosi 3:7 Hakika bwana hatafanya neno lolote bila kuwafunulia watumishi wake, manabii siri zake, hii ina maana Mungu kuna vitu hata ruhusu kwako mpaka amekujulisha na Mungu anapokujulisha kama icho kitu ni kibaya maana yake anataka ukipinge, au ukikatae, au ukiepuke, hivyo basi kama kuna mtego wa ibilisi mbele yako au mkakati wa adui, wa kukuingiza kwenye dhambi, au vifungo, Mungu anakuapa kujua. Na unapewa kuyafahamu Mambo ambayo wengine hawayajui wala hawawezi kuyatambua na ndio sababu Biblia ikasema mtu wa rohoni huyatambua yote, kwa vipi ? kwa msada wa Roho mtakatifu {ni muhimu kuelewa kuwa hatuwezi kuyajua mambo yanayoendelea katika ulimwengu wa Roho mpaka tumekuwa katika Roho}
Ukisoma Daniel 2 ;18 anasema ‘Ndipo Danieli akafunuliwa siri hiyo katika njozi ya usiku. Basi Danieli akamuhimidi Mungu wa mbinguni’
Sasa ukianza nyuma kidogo na hii habari utagundua ilikuwa ni shida iliyompata Mfalme nebukadreza, na vile ambavyo hakuna mtu mwingine angeliweza kujua jambo lolote isipokuwa ni yule tu wa rohoni, kwa sababu Danieli alikuwa ni mtu wa rohoni Bwana alisema nae rohoni jambo ambalo wenye hekima, na wachawi wote walishindwa kuliletea uvumbuzi, lakini kijana mmoja wa Rohoni aitae Danieli, akawa ana jibu na kusababisha amani kwa nchi nzima.
Ndugu msomaji isikutishe hii kuitwa mtu wa Rohoni au la, Biblia imesema wazi kabisa ‘Rumi 8 :14 kwa kuwa wote wanaongozwa na Roho wa Mungu hao ndio wana wa Mungu’ hivyo basi kama umeokoka Roho mtakatifu yuko ndani yako, maana huwa anashuka kwa ajili ya kuwaongoza maelfu ya watu wanaoingia kwenye orodha ya kuitwa wana wa Mungu, maana ndie anayetakiwa kumfundisha na kumuongoza kila anae ingia katika maisha mapya sasa shida ni kuwa watu wengi huwa tuna muhuzunisha, na wakati mwingine tunamzimisha kabisa.

Ingekuwa kama tungejua jinsi tunavyotafutwa na ibilisi usiku na mchana na hatuwezi kuona kwa sababu tunaishi mwilini na kuwa Roho mtakatifu anatakiwa kuona kwa niaba yetu kama ni balaa atuepushe, kama ni mauti atuepushe,na kuwa kama kuna jambo lolote atuajulishe kitu cha kufanya. Tungeyatambua hayo tungeudumisha uhusiano wetu na Roho mtakatifu.
maana kadri utavyoendelea kuudumisha uhusiano wako na Roho mtakatifu kwa maombi, na kwa kulisoma neno, ikiwa ni pamoja na akujiepusha na uovu unampa roho mtakatifu nafasi ya kuyafungua macho yako ya Rohoni,na masikio yako ya Rohoni hivyo basi ukianza kusikia na kuona Rohoni hakuna namna adui anaweza akakupata,
Maana kuna wakati mwingine utaambiwa usipande iyo Gari, au usichukue iyo nguo. Au usitumie iyo zawadi, au usinunue icho kinyago, au usinunue huo mdoli, au usile icho chakula,


Nakumbuka tukiwa tunafanya huduma ya ukombozi mahali fulani Dada mmoja alikuwa amevamiwa na nguvu za giza tu kwa sababu alilithi gauni la shangazi yake kumbe baada ya shangazi mtu kufariki Roho za giza zikabaki kwenye Nguo zake tulipokuwa tukiamuru zile roho za giza zimtoke zilipiga kelele na kusema tunataka gauni letu la marehemu, amechukuwa gauni letu, kwa kweli sikuelewa sana, isipokuwa mara baada ya kumaliza ile huduma nilipata nafasi ya kuzungumza nae na kumuuliza endapo kuna kitu chochote amekirithi ni cha marehemu ndipo aliponijulisha kuwa ni kweli kuna gauni la Shangazi alipokufa nikalichukuwa huwa ninalivaa ila kuanzia nilipoanza kulivaa kuna vitu niliona vimebadilika sana mwilini mwangu.
Kitu ninachotaka uwe mwangalifu ni hiki kuwa kuna wakati utatakiwa kuombea hata nguo kabla ya kuivaa, lakini anayetakiwa kukumbusha na kukuambia kama uombee au la, si mwingine isipokuwa ni roho mtakatifu. Na ndio sababu ukisoma katika Zekaria 3 :4 anasema ‘Nae huyo akajibu akawaambia wale waliosimama mbele yake akisema mvueni nguo hizi zenye uchafu, kisha akamwambia yeye tazama nimekuondolea uovu wako nami nitakuvika mavazi ya thamani nyingi,,,,,,,,’ kitu nilitaka uone ni jinsi amabavyo unaweza ukabeba matatizo,uovu,uchafu, shida tu kwa sababu ya mavazi, na ndio maana baada ya huyu ndugu kutolewa yale mavazi yake machafu uovu wake uliondolewa hii ina maana uovu ulikuwa kwenye mavazi. Na kumbuka ndugu mmoja aliniuliza swali sasa utajuaje hili vazi lina nguvu za giza na hili halina,
Ndugu msomaji ndio maana tunasisitiza uhusiano wa mtu binafsi na Roho mtakatifu maana si kweli kwamba mavazi yote yana mapepo isipokuwa kunawakati utakutana na mtego wa namna hiyo na kama hautakuwa na macho ya rohoni itakuwa rahisi sana kwa wewe kutekwa na ibilisi.
7/ kuhuzuria au kuishi maeneo yenye utawala wa kipepo
Ndugu msomaji wapo watu ambao huchukulia mambo haya kirahisi wapo watu amabao hupenda kuhuzuria maeneo ya matambiko hata kama wao wameokoka, wengine hawaoni shida huhudhuria vikao vya sadaka kwa miungu wengine huudhuria siku ambapo zile nyama zinaliwa ambabazo ni batili, wengine hudiliki hata kunywa zile dawa ambazo wao jadi na mila, wanaziita kinga ya ukoo, wengine huwa wanadai wanawasindikiza wengine kumbuka kadri unavyoendelea kuhudhuria kwenye hayo maeneo ndivyo unavyoendelea kufungua mirango kwa Adui hutajua ni saa ngapi mapepo yalikuvaa, maana ulinzi wa Mungu huondoka na kwa sababu yeye ni Mungu mwenye wivu ukijiingiza kwenye miungu mingine ulinzi wke unakuacha na laana yake inaambatana nawe, na Biblia inaonya , Kumbu 4 : 23 jihadhalini nafsi zenu msije mkalisahau agano la BWANA, Mungu wenu alilofanya nanyi mkajifanyia sanamu ya kuchonga, mfano wa umbo la kitu chochote, ulichokatazwa na BWANA, Mungu wenu, kwa kuwa BWANA, Mungu wenu, ni moto ulao Mungu mwenye wivu.’ Sasa ukiufuatilia huu mstari utakuta anasema jihadhalini nafsi zenu. Msije mkaanza kuabudu miungu maana washirikina wengi leo hawajui ni lini walianza kuamini hivyo vitu wanavyo amini pia hofu ya Mungu imewatoka na ukifuatilia kwa makini utagundua kuwa hiki ndicho kilichozaa huu mstari bandia wa biblia {jisaidie nami nitakusaidia} watu kutaka kuhalalisha kumchanganya Mungu na shetani,kuchanganya mambo ya ushirikina na Mungu. {hatari} kumbuka Mungu ni moto ulao na ni mwenye wivu.





8/ wengine majina yao yamewaingiza kwenye vifungo
Ndugu msomaji wa mafundisho haya ukifuatilia leo majina mengi sana amabayo watu wanayo kwa asilimia kubwa yamekuwa yakiendana na maisha yao, sababu ni hii kuwa jina lina sehemu kwenye maisha ya mtu, ukifuatilia malaika Gablieli wakati anamwambia Yusufu sababu za kumuita mtoto jina Yesu utagundua kuwa aliitwa Yesu kwa sababu ndie aliyekuja kuwaokoa wanadamu na dhambi zao kwa iyo jina Yesu ndani yake kulikuwa na ukombozi wa dhambi za watu, hebu soma
"basi alipokuwa akisafiri tazama malaika wa Bwana alimtokea katika ndoto akisema ‘Yusufu, mwana wa Daudi, usihofu kumchukua Mariamu mkeo, maana mimba yake ni kwa uwezo wa Roho Mtakatifu naye atamzaa mwana, nawe utamwita jina lake Yesu MAANA YEYE NDIE atakaye waokoa watu wake na dhambi zao." Sasa lile neno maana tunaweza tuka sema kwa sababu, fikilia kama Yusufu angeamua kumuuliza malaika kwa nini mtoto aitwe Yesu? Na tusimuite jina jingine, Malaika angemjibu kwa sababu ndie atakayewaokoa watu na dhambi zao. Hivyo unaweza ukaona kuwa ndani ya jina la Yesu kulikuwa na ukombozi, na ndio maana leo tukilitaja kuna mambo ya tofauti yanatokea, pia zipo sababu nyingi zinazowafanya watu waape watoto majina wanayo wapa
Yapo majina kama Taabu, Shida, Majuto, kibaya, Cha usiku, Mbutolwe hili ni la kilugha maana yake kwenye matatizo, yapo mengi yanayofanana na haya sasa sisemi majina kama haya ni mabaya isipokuwa natamani wewe unaye muamini Mungu upate uwanja mapana wa maarifa, maana asilimia kubwa ya watu waliopewa majina haya majina yao yanaendana na maisha yao, maana Jina linanafasi kwenye maisha ya mtu. Hivyo basi jina linaweza likafungua mlango kwa roho za giza kumiliki maisha ya mtu. Hebu tuangalie mfano mwingine ukisoma Mwanzo 35:16-18 anasema "wakasafiri kutoka betheli hata ukabaki mwendo wa kitambo tu kufika Efrasi Raheli akashikwa na utungu wa kuzaa na utungu wake ulikuwa mzito ikawa alipokuwa anashikwa na utungu mzalisha akamwambia usiogope maana sasa utamzaa mwanamume mwingine ikawa hapo katika kutoa Roho yake maana alikufa akamwita jina lake Beloni lakini lakini Baba yake akamwita benjamini" sasa unaweza ukaona mazingira jina lilivyo tolewa, jina lilitolewa mama akiwa anakufa na unaweza ukajiuliza swali kwa nini Yakobo alipofika akambadilisha mtoto jina? Jina a la kwanza halikutolewa kwenye mazingira ya baraka isipokuwa mazingira magumu yaliyojaa uchungu. Lakini pamoja na hayo yapo majina ambayowatoto walipewa na waganga wa kienyeji, watu wa mira, wazee wa jadi, majina mengine yalitolewa kwenye matambiko ibada za kuwaombea watoto kwa wafu majina haya huambatana moja kwa moja na roho za giza.
Jifunze kutangua maneno mabaya ya watu kwenye maisha yako. Mtu anapokuambia utakufa palepale mwambie sifu, utafeli sifeli, jifunze kutangua laana za maneno kila wakati maana maneno ya mshirikina au mchawi yanaenda kutengeneza kitu katiaka ulimwengu wa roho ambacho uanaweza ukakitangua hapohapo anapokisema.
NINI HUTOKEA KWA MTU ANAPOKWENDA KWA MGANGA WA KIENYEJI
------ Huingia kwenye laana ya kuabudu miungu mingine na kuitegemea, maana mganga wa kienyeji hutumia mizimu kutatua matatizo yake, hivyo basi mtu huyu pia anakuwa amejiingiza kwa hiari kwenye utawara wa nguvu za giza.
------mtu anapochanjwa chale kinachokuwa kinatafutwa ni Damu, kwa ajili ya kufanikisha agano Fulani na mapepo, kwa hiyo Damu inapotolewa kwa kuchanjwa wakati mwingine mganga huwa akisema maneno ambayo mtu anakuwa hajui maana yake, hivyo unapochanjwa chare unaingia kwenye mkataba wa mwili wako na mapepo, unaubinafsisha mwili kwa roho za giza. Kwamba roho za giza ziwe na maamuzi juu ya mwili wako.
------umewahi kujiuliza kwa nini mganga wa kienyeji hutoa masharti amabayo mtu asipofuata anakuwa katika hali ya Hatari, sababu ni hii, ili aendelee kuzitimizia roho za giza matakwa yao kupitia huyu mtu maana huyu mtu anakuwa umefanyika sehemu ya utendaji katika ofisi za kipepo.
-----roho za ushirikina zinamvaaa, imani yake inaamia kwenye roho za giza, kunaanza kutegenezeka urafiki kati ya mtu huyu na roho za giza hivyo basi kila gumu atakalo kutana nalo, utatuzi wa kunza utakuwa ni mganga wa kienyeji na mambo ya ushirikina, maana ufahamu mtu unakuwa umetekwa, mwenye vifungo, watu wanamshangaa lakini lakini yeye anajiona yuko huru,yuko sahii.
-----Irizi anayopewa mtu kwa mganga ni ishara ya kukubaliana na kubeba mizigo ya mapepo kwenye maisha yake ikiwa ni pamoja na Roho za mauti, na ukitaka kujua irizi ni mbaya watu huwa wanaificha. Na kila wakati ni nyeusi, Mungu amekataa matumizi ya Irizi, Ezekieli 13:18 anasema "useme hivi,Ole wao wanawake wale,washonao hirizi katika viungo vyote vya mikono"……ukiendelea mtari wa 20 anasema "Basi Bwana Mungu asema hivi, tazama mimi ni kinyume cha Irizi zenu….."
MATOKEO YA WATU KUSHIRIKI MAMBO YA USHIRIKINA.
Unaambukizwa rohoo za ushirikina.
Anaambukizwa roho za ushirikina kwa njia ya uvuvio wa kipepo, Ghafla anaanza kupenda na kuzoea mambo ya kichawi,anaanza kujitoa kwa shetani na kuwa teyari kumuabudu, unaanza kuwa muadilifu katika kutimiza yanayohitajika kama kutoa sadaka ya damu, na mambo mengine ya aibu. Nimefanya counseling {ushauri} na mabinti ambao wazazi wao waliwataka kufanya nao tendo la ndoa wengine wameshafanya tendo la ndoa na wazazi wao kwa siri nikagundua. sababu kubwa ni roho ya ushirikina ndani ya mzazi. Maana pia wako wazazi ambao hawapeleki mtoto shule mpaka wameenda kwa waganga wa kienyeji kwanza.
Sasa kitu shetani anakifanya ni kuhakikisha washirikina wamekuwepo kila mahali ili kulahisisha utendaji wake wa kazi, na moja ya kazi kubwa ya washirikina ni kuambukiza imani ya kishetani kwa watu wengine. Na ndio sababu unatakiwa kuwa muangalifu maana si wengi waliozaliwa na Roho za uchawi, wengingi wamevuviwa na pepo kwa kushiriki mambo Fulani Fulani.
Mara nyingi Mambo haya huambatana na washirikina
{a}Roho za mauti, mtu huyu anakuwa katika hali ya kufuatiliwa na Roho za mauti, wengi wao hufa vifo vya gafra, Ajari zenye utata,
{ b} Kufungwa kizazi, wapo watu ambao waliwahi kushiriki mambo ya ushirikina na wamekuwa tasa hawawezi kabisa kupata watoto mpaka yale mapepo yaliyoshikilia kizazi yatakapoachia icho kizazi.japo haina maana kila Tasa ni roho za Giza. Ikiwa uliwahi kushiriki mambo ya ushirikina na unashuhudiwa moyoni kuwa Roho za mauti zinakufuatilia Muamini yesu leo akufungue maana yeye ni mkuu kuliko hizo Roho za giza ukisoma Ebra 2:14 anasema "basi kwa kuwa watoto wameshiriki damu na mwili yeye naye vivyo hivyo alishiriki yayo hayo ili kwa njia ya mauti amuharibu
yeye aliyekuwa na nguvu za mauti, yaani, ibilisi, awaache huru wale ambao kwamba maisha yao yote kwa hofu ya mauti walikuwa katika hali ya utumwa"
{ c } kutofanikiwa watu wengi waliowahi kushiriki mambo ya kishirikina nyuma yao huwa kunakuwa na hali ya kutokufanikiwa kuna hali ya kuharibika kwa mambo anaweza akawa alinunua gari gafra inapata ajali, alikuwa na Duka linaungua, mara anaporwa mali yote, mara anafukuzwa kazi, ili mradi tu aishi maisha ya kuchanganyikiwa sababu huwa inakuwa nyuma ya mafanikio ziko roho za giza.
{d} Roho za kukataliwa watu wengi leo wanaofuatiliwa na nguvu za giza kwa sababu walishiriki mambo ya ushirikina huwa nyuma yao kunakuwa na kukataliwa, hali ya kuchukiwa, hata ukipendeza hakuna mtu anakuambia umependeza, hata ukiwa na mawazo mazuri hakuna anaye yataka mawazo yako, kwa wakaka hata ukiwa na kila kitu hakuna Dada anayetamani kuolewa na wewe, kwa akina dada hata kama kuna kaka alisha kuchumbia anakuja kukuacha gafra na hataki tena kukuoa, kwa wafanyakazi inawezekana ofisini mtu ni mchapa kazi lakini hakuna mtu anajali hata kuna wakati mtu huyu huwa anajisikia vibaya.sehemu kubwa ya mambo haya huwa inakuwa ni Roho za kukataliwa.na mambo mengine mengi ambayo yanafanana na haya
Hivyo basi ikiwa unakabiliana na hali za namna hii uwe na hakika siyo mapenzi ya Mungu japokuwa yapo mambo mengine ya kawaida kabisa yanayoweza yakasababisha mtu akaonekana amekataliwa, mfano kutokujijari {usafi} hasa mabinti, kutokuwa mtii, kutokuwa mnynyekevu, kutokokujizuia,kutokujikubali,kutokujiamini, na maengine mengi yanayofanana na haya
Unavyoweza ukayatambua moja ya matendo ya Uchawi na Ushirikina
Ibada za wafu, kuagua, kuzindika, kuongea na wafu, Ibada za mapepo,unajimu wa nyota,sadaka ya damu, Ngoma za matambiko, kuamini waganga wa kienyeji, uwezo wa kuona mambo yasiyoonekana, na kujua mambo kabla hayajatokea, pasipo Nguvu ya Yesu, uwezo wa kusafiri mbali nje ya mwili wako, wengine huona kama anapaa hewani, utumiaji wa vifaa vyovyote vya kichawi, kushiriki ibada za kimila, hivyo kuna umuhimu wa kuwa muangalifu sana kama kuna baadhi ya haya mambo umekuwa ukihusika nayo.
LAANA
Ukisoma kamusi ya Kiswahili ijulikananyo kama ‘oxford kamusi ya kiwahili sanifu’ utakuta wameelezea neno Laana kuwa ni ukosefu wa radhi za mwenyezi Mungu; hasira ya Mungu. Au apizo atoalo mtu kwa mtu mwingine ili afikwe na ubaya, uovu,msiba, au hasira ya Mungu.
LAANI neno laani limetafsiliwa kama, shtakia kwa Mungu, au ombea uovu.
Ndugu msomaji yapo mambo mengi sana amabayo yanaweza yakasababisha hasira ya Mungu kwa mtu , na kusababisha mtu ashindwe kabisa kupokea Baraka kutoka kwa Mungu. Kwenye maisha yake.
Hivyo basi hasira ya Mungu {laana} inaweza ikampata mtu yeyote ambae atahusika na haya yafuatayo.
{a} Laana ya kuabudu miungu mingine,
Kumb 27:15 anasema "na alaaniwe mtu afanyae sanamu ya kuchonga, au ya kusubu, machukizo kwa BWANA, kazi ya mikono ya fundi, akaisimamisha kwa siri. na watu wote wajibu waseme Amina" Sasa kule kuabudu miungu mingine,au kuchonga kitu na kuanza kukisujudia, kunasababisha laana ya Mungu juu ya maisha yako.
{ b} Laana ya kuwadharau wazazi,
Wapo watu wanao wadharau wazazi wao, hawataki kufuata ushauri wa wazazi, na mbaya zaidi ni kule kuwadharau tu kwa sababu wao hawajaokoka, kumbuka Bado ni wazazi wako na bado wana baraka zako maana Mungu aliamuru waheshimiwe, Isipokuwa kama laana itatoka kwao bila sababu haitakupata wewe. Kutoka 20:12 waheshimu Baba yako na Mama yako; bila kujalisha wameokoka au hawajaokoka, matajiri au maskini, Mungu aliamuru waheshimiwe, sasa ukiendelea kidogo anasema "siku zako zipate kuwa nyingi katika nchi upewayo na Bwana, Mungu wako." Sasa hii inaweza ikakusaidia kujua kuwa wako vijana wengi sana leo ambao hawakukubali kufunzwa na wazazi wao, kuwaheshimu wala kuwatii, wengi wao leo wameshapoteza maisha, isipokuwa wazazi, wakikutaka ufanye uovu, maana wapo pia, Mungu atakupa hekima ya namna ya kutokukubaliana nao. Na hata wakitaka kukulaani Biblia inasema laana isiyo sababu haimpati mtu.
{ c } Laana ya kufanya tendo la ndoa na dada yako au kaka yako
Kuna mambo mengine sio rahisi hata kuelezea lakini yapo na yanafanyika mtu amelala na Dada yake, mwingine na kaka yake, laana ya Mungu imeagizwa juu yao Kumb 27 :22 ‘na alaaniwe alalaye na Umbu lake, binti ya babaye au Binti ya mamae. Na watu wote waseme Amina .’
{d} Laana ya kutembea na mama yako au mke wa Baba yako.
Unaweza usielewe kuwa haya mambo yanafanyika sasa iyo ni laana ya Mungu juu ya mtu Kumb 27 :20 na alaaniwe alalaye na mke wa Baba yake,kwa kuwa amefunua mavazi ya babaye na watu wote waseme Amina.
{e} Laana ya kumtegemea mwanadamu na sio Mungu
Wapo watu ambao wanawaheshimu Binadamu zaidi na kuwaogopa kwa kiwango cha kumpa Mungu nafasi ya pili kwenye maisha yao, Yeremia 17 :5 Bwana asema hivi, Amelaaniwa amtegemeae mwanadamu kuwa kinga yake, na moyoni mwake amwemwacha Bwana. Mtu yoyote anaye mfanya mwanadamu kuwa kinga yake huwa anahesabiwa kuwa amemwacha Bwana, sasa ukiusoma ule mstali wa 6 anasema ‘maana atakuwa kama fukala nyikani, hataona yatakapotokea mema. Laana ya kumtegemea Binadamu zaidi na sio Mungu inakupa upofu ushindwe kuona tena baraka za Mungu kwenye maisha yako, maana tumaini lako limehamia kwa Mwanadamu.
{f} Laana ya udhulumaji
Kuna watu amabao wamewazulumu wengine, wamechukua sehemu ya ardhi ya wengine, pia wamechukua, sehemu ya mpaka wa nyumba ya mwingine na kudai sehemu hiyo ni yake na yuko teyeri hata kwenda mahakamani, lakini rohoni anashuhudiwa iyo sehemu si yake iko laana inaambatana na mtu huyu Kumbu 27 :17 ‘Na alaaniwe aondoae mpaka wa jirani yake’ Na watu wote waseme Amina, Na udhulumaji mwingine wowote mtu anao ufanya huwa unakuwa na laana nyumayake.
{g} Laana ya kuwakosesha walemavu
Wapo watu ambao hawawezi kabisa kusaidia vipofu hata akiona anakwenda kwenye miba, au mahali kusiko, wengine wanaona ni unajisi kuwasaidia vilema na wenye ukoma, sisemi ni lazima kuwasaidia isipo kuwa unapokuwa kwenye mazingira ya kumsaidia na ukamwacha katika hali ya kuhangaika inaleta shida Kumb 27 : 28 anasema ‘na alaaniwe ampotezae kipofu kukosa njia, na watu wote waseme Amina,’ anaposema ampotezae kipofu kukosa njia maana yake aliweza kumsaidia lakini akamwacha.
{h} Laana ya kumuibia Mungu zaka {fungu la kumi}
Watu wengi leo wamepandwa uongo na Ibilisi kuwa anapotoa sadaka inakwenda mahali fulani, fulani, na hivyo wanaacha kutoa fungu la kumi dhaka, ikiwa ni pamoja na sadaka zingine, kumbuka hapa sifundishi utoaji isipokuwa nataka tu ufahamu kuwa iko laana kwa wasiotoa, Maana Mungu anawahesabu kama wanao muibia, Maana ni bora ukatoa usijue unakokwenda maana nataka nikuambie Mungu ataipigania na kuifuatilia pesa yake, maana ni sadaka yake ambayo wewe umetoa, kulikoni kukoseshwa baraka zako,na hivyo kupata laana Malaki 3 :8 je mwanadamu atamwibia Mungu ? Lakini ninyi mnaniibia mimi. lakini ninyi mwasema, Tumemuibia kwa namna gani ? Mmeniibia dhaka na dhabihu. Sasa ukiusoma mstali wa 9 anasema ‘Ninyi mmelaaniwa kwa laana ; maana mnaniibia mimi….’
{i} Laana ya kupindisha injili
Wapo watu leo wangetamani hata kuibadilisha Biblia kama wangeweza, maana wanataka Biblia iwafuate wao wanavyotaka badala ya wao kulifuata neno la Mungu na kulitii, na ndio sababu kuna kitu kinaitwa manabii wa uongo, na wapotoaji wa maandiko, sasa kitu natamani ujue ni kuwa iko laana ya Mungu itakufuatilia tu endapo utapotoa maandiko na kuwapotosha wengine ukisoma Garatia 1 :6 anasema ‘Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya kristo, na kuigeukia injili ya namna nyingine, wala si nyigine lakini wapo watu wawatabishao na kutaka kuigeuza injiri ya kristo sasa mstali wa 8 anasema ‘Lakini ijapokuwa sisi au malaika wa mbinguni atawahubili ninyi injili yoyote isipokuwa iyo tuliyowahubiri na alaaniwe !’kitu nilitaka uone ni laana inayomkabili mtu yoyote anapopotoa injili ya kristo,
{j}Laana ya kuilaani Izraeli
Ndugu msomaji wapo watu wengi leo huisema vibaya Izraeli, bila kujua madhara yake, kwenye maisha yao, na matokeo yake laana kuwafuatilia bila ya wao kujua, ukisoma Mwanzo 12 :2 utakuta Mungu akimbariki Ibrahimu, na kumbuka kuwa katika ibrahimu alitokea Yakobo, ambaye baadae akaitwa Izraeli, na kwa Yakobo{Izraeli} tukapata kabira kumi na mbili za Izraeli, Taifa teule la Mungu ambalo ndilo tulilonalo mpaka sasa hivyo basi kama unataka kubarikiwa jifunze kuwabariki maana ukisoma Mwanzo 12 : 2 utaona Mungu akimwambia Ibrahimu anasema ‘nami nitakufanya wewe kuwa taifa kubwa, na kukubariki, na kulikuza jina lako ; nawe uwe baraka ; mstari wa pili nami nitawabariki wakubarikio, naye akulaanie nitamlaani ; na katika wewe jamaa zote za Dunia watabarikiwa. Sasa basi na wewe uko kwenye jamaa zote za dunia wanaotakiwa kubarikiwa endapo tu wataibariki Izraeli.

MOJA YA VITU VINAVYOWEZA KUKUASHIRIA MTU YUKO CHINI YA LAANA,VIFUNGO AU UNAFUATILIWA NA ROHO ZA GIZA:
Kuishi maisha ya kutokufanikiwa, kutokuvuka daraja fulani, kila unalojitahidi kulifanyia jitihada unaishia kuwa mtu wa kushindwa tu. Ziko familia amabazo hakuna mtu aliyewahi kuvuka level Fulani ya kimaisha. kama ni elim inaweza ikawa mwisho form four hakuna aliye wahi kuvuka hapo.hata kama mtu alikuwa anaakili vipi, anaishia kuvuta Bangi, na kupata mimba.
Kwa wengine mafanikio Fulani yanapotaka kutokea tu, ndipo linapotokea jambo la kurudisha nyuma, na anabaki kwenye ilo eneo siku zote. Misiba, magonjwa, ajali, na kutapeliwa
Maumivu yasiyo na sababu maalumu Mwili mzima, au Magonjwa ya ghafra na vipimo vya Hospitari kushindwa kuonyesha kitu chochote,
Wapo watu amabao huwa wanaota waliokufa mara kwa mara, wakati mwingine kuona unapaa hewani.
Kuota unakula au unalazimishwa kula nyama Fulani, wakati mwingine kuhisi kabisa ni za watu.au kuota unakimbizwa na majoka,wanyama wakali, mara kwa mara.
Tulifanya huduma na Binti mmoja Sumbawanga ambae Baba yake aliltaka alithi mikoba ya uchawi na yeye alikuwa hajui hilo, isipokuwa mara nyingi alimuona Bibi kizee katika ndoto aliyemtaka apokee mkoba wenye fifaa vya ushirikina, wakati mwingine alilazimishwa kula vitu Fulani.katika ndoto. Siku moja Baba yake akaja akamwambia wewe peke yako ndie uliyependwa na Bibi zako utatakiwa kushikilia mambo yetu ya mila na ntakufundisha namna ya kufanya. Ndipo yule binti akaelewa alichokuwa anakiona.
Wengine huwa wanaona wanadumbukizwa shimoni, analia kwa uchungu ukitafuta msaada.
Kupoteza ujasili, kuwa muoga kupita kiasi siku zote, kushindwa hata kukaa ndani peke yako, hasa wakati wa usiku.
Kuota unafukuzwa na waliokufa, au mnafanya nao vikao.
Kuota au kuona kwenye maono umevaa vifaa vya ushirikina kama Irizi,nguo za matambiko, na vikapu vyenye madawa ya kienyeji.
Wengine huona kama maono, au kuota kuwa wamelala juu ya Jeneza au makaburi .
Wapo wanao ota wamevaa mavazi ya kimila, wengine huota mara kwa mara wanaagua, au wapo kwa waganga wa kienyeji hata kama hajawahi kwenda.
Kusikia hisia Fulani Fulani ambazo si za kawaida mwilini kwa kipindi na kipindi, Wengine hupata mishtuko ya mara kwa mara na hawajui sababu, wengine huona mwili mzima unachomachoma, Vipindi Fulani Fulani.
Kutokushika kwa mimba, Au mimba kuharibika. Mara kwa mara.
Wengine huota wanafukua makaburi wakati mwingine wamebeba maiti za watu, na wakati mwingine umwagikaji wa Damu.na hivi vitu kutokea mara kwa mara, wakati mwingine unaona umebeba maiti na unashurutishwa kwenda nayo mahali Fulani. Hizo ni roho za giza
Kuishi maisha ya kukata tamaa siku zote, na kila wakati kufikilia ni bora kufa kuliko kuishi. Hizo ni roho za giza. Yesu alikataza kabisa kukata tamaa ila alitutaka tuishi maisha ya kuomba siku zote. "Luka 18:1 akawaambia mfano ya kwamba imewapasa kumuomba Mungu siku zote wala msikate tamaa."
Kuvunjika kwa ndoa na matengano kwenye familia.
Kusikia uchovu wakati wa ibada, miayo isiyo ya kawaida wakati wa maombi,
Kuwachukia watumishi wa Mungu bila sababu na kuwasema vibaya.
Kusikia sauti zisizo za kawaida zinazo ashiria hatari, {strange voices} vipindi Fulani, wengi husikia wakiwa kwenye ndoto. Wakati mwingine zinakuwa za watu waliokufa. Hizo zote ni roho za giza.
Uwezo wa kuona mambo ya kishirikina, kuona wachawi, kutoa unabii, kujua mambo ya watu wengine nje ya nguvu za Bwana Yesu. Mate 16:16 ikawa tulipokuwa tukienda mahali pale pa kusali kijakazi mmoja aliyekuwa na pepo wa uaguzi akatukuta, aliyewapatia Bwana zake faida nyingi kwa kuagua. Akamfuata Paulo na sisi akipiga kelele, akasema watu hawa ni watumishi wa Mungu aliye juu, wenye kuwahubiria njia ya wokovu. Akafanya hayo siku nyingi. Kitu nataka uone ni kuwa huyu kijakazi hakuwa na nguvu za Mungu isipokuwa za pepo na ilikuwa ni ngumu kujulikana ni mpaka Mungu alipomfunulia Paulo matari wa 18b Lakini Paulo akasikitika, akageuka akamwambia yule Pepo sio kujakazi tena Nakuamuru kwa jina la Yesu kristo, mtoke huyu, Akamtoka saa ileile. Lengo ni kukusaidia kuwa muangalifu maana si kila mtu anamuabudu Mungu aliyehai leo, na kutembea kwenye uweza na nguvu zake. Nakumbuka nikifanya huduma mahali Fulani nilikutana na mtu wa namna hii na watu wa eneo lile wote waliamini anatumia Nguvu za Mungu na kumbe ndani yake alikuwa na pepo lililo muwezesha kufanya mambo hayo yote lakini hata yeye alikuwa hajui, kwa Neema ya Mungu nilipata ufunuo juu ya ilo mara nilipomuona tu. Tulipofanya nae maombi tu nguvu za Giza zilimuachilia.kila mtu alishangaa.
Kuona unatembea kama nyoka kwenye ndoto, kuota ndoto za majoka, na mambo ya kishetani, pia mara kwa mara kuongea peke yako wakati uwapo usingizini, tena kwa mda mrefu.Ndugu msomaji nguvu za giza huweza kuwasiliana na mtu kwa njia ya sauti, ndoto na hisia. Na ndio maana unaweza kuhisi kwa kuongozwa na Roho mtakatifu kwa habari za uwepo wa nguvu za giza mahali, wakati mwingine hata zikiwa ndani ya mtu.Inawezekana haya yakawa yakitokea kwenye maisha yako lakini usiogope, Kumbuka kuwa kazi zote Yesu alimaliza pale msalabani Biblia inasema wazi kabisa kuwa udhihilisho wa Yesu Duniani ulikuwa ni kwa ajili ya kuzivunja kazi za Ibilisi. Ukisoma Yoh 3:8b "kwa kusudi hili mwana wa Mungu alidhihilishwa azivunje kazi za Ibilisi. pia ukisoma {Kolosai 1:13} anasema "naye alituokoa katika nguvu za giza akatuamisha na kutuingiza katika ufalme wa mwana wa pendo lake."
Ili mtu aweze kufunguliwa
Anahitaji utayari wa kuelezea mambo uliyowahi kufanya au kufanyiwa {making comfetional} hii ni kwa sababu uwazi unampa huyu mtumishi kujua namna ya kukupeleka mbele za Mungu.
Anahitaji kuwa na utayari wa kuviachia vitu ulivyovishikilia vile vya ushirikina inaweza ikawa ni mikoba ya uchawi au vitu vya aina yoyote ile, kutoka kwa waganga. Mfano wa vitu Irizi, vibuyu, mavazi ya aina Fulani, vitu vya kutambikia mizimu,Shanga za kuvaa, na kila aina ya kitu ulichopewa kwa ajili ya ushirikina, Ule utayari wa kuviachilia unafungua mirango ya uponyaji wako. Maana wapo watu wangependa kufunguliwa lakini bado wanataka kuendelea kushikilia hivyo vitu pia, wawe na uhakika hawata funguliwa maana Mungu awezi akamfungua mtu na kutaka aendelee na miungu mingine.
Vitu vya ushirikina amabvyo mtu hupewa vinamuunganisha yeye na falme za Adui {kuzimu} bila yeye kujua. Sasa basi mtu anapo amua kuachilia anakuwa ameamua kujitoa kwenye hicho kifungo kwa iyali yake mwenyewe,
Lengo ni kumsaidia mtu aifahamu kweli ya Mungu ili asiendelee kukubali manyanyaso ya Ibilisi Yoh 8:32 Nanyi mtaifahamu kweli na hiyo kweli itawaweka huru shida ni kuwa wapo watu wengi leo hata baada ya kuifahamu kweli bado wameendelea kuficha uovu wao na vitu vyao vya ushirikina japokuwa wanasali na Mungu wanampenda sana, wengine hufikili kuwa watu watanielewaje wakijuwa nilikuwa ninafanya haya, kumbuka ni kwa ajili ya ukombozi wako mwenyewe, ukishindwa kabisa fanya kama nikodemu utafanyiwa hata huduma ya ukombozi kwa siri.
Biblia imesema wazi kabisa "Mith 28:13 Afichae dhambi zake hatafanikiwa bali yeye aziungamae na kuziacha atapata rehema" Maana halisi ni kuwa mtu akificha kinachomtatiza hawezi kufunguliwa isipokuwa akiwa wazi zipo rehema za Mungu juu yake kwa ajili ya ukombozi wake.
WATU WALIOISHI CHINI YA VIFUNGO VYA NGUVU ZA GIZA NA KUFUNGULIWA NA BWANA YESU
Yesu anamfungua mgerasi
Marko 5:1 wakafika ngambo ya bahari mpaka nchi ya wagerasi waliposhuka chomboni walikutana na mtu ambaye ametoka makaburini wala hakuna mtu yeyote aliyeweza kumfunga tena kwa minyororo, kitu nataka uone ni ni mateso na manyanyaso aliyokuwa nayo huyu mtu tu sababu tu ya nguvu za giza ukisoma mstari wa 5 utaona kitu kingine "na siku zote usiku na mchana alikuwako makaburini na milimani akipiga kelele na kujikata kata kwa mawe", sasa ukisoma kitabu cha Luka 8:27 utaona utaona huyu mtu akielezewa kwa kitu kingine, Biblia inasema " naye aliposhuka pwani yaani Yesu alikutana na mtu mmoja wa mji ule mwenye Pepo hakuvaa nguo siku nyingi wala hakukaa nyumbani" mapepo yalimshurutisha huyu mtu pia kutokuvaa nguo hapo nyuma kidogo tumeona yalimfanya asikae nyumbani,apige kelele, apende makaburini, ajikate kate kwa mawe.
Roho za giza zinatesa zichukie na kuzikataa kabisa kwa kuishi maisha ya kujilinda na maombi, nakumbuka tulifanya huduma na binti mmoja wa aina hii mkoa Fulani baada ya kufunguliwa alitupa ushuhuda jinsi amabvyo Roho za giza zilikuwa zikimuamuru kukaa uchi, watu walikuwa wakiondoka nyumbani anafunga mirango na kubaki uchi, wakirudi anajifungia chimbani kwake alieleza mambo mengi sana yaliyoambatana na hilo.
Yesu alipomfungua mwenye pepo kifafa
Math 17:14 "Nao walipoufikia mkutano mtu mmoja alimjia akapiga magoti akasema Bwana umreemu mwanangu kwa kuwa ana kifafa na kuteswa vibaya maana mara nyingi huanguka motoni na mara nyingi huanguka majini mstari wa 18 Yesu akamkemea pepo, naye akamtoka; Yule kijana akapona tangu saa ile,"
Nataka uone jinsi ambavyo yale mapepo yalikuwa yanamtesa huyu mtoto, hakuwa na amani wala furaha, maisha ya huyu mtoto yalijaa huzuni na mateso Biblia inaonyesha wazi jinsi amabavyo huyu mtoto alivyo angushwa motoni na majini,
Mi sijui kama ummewahi ona mtu wa hali hii tulipofanya huduma na mtu wa hali hii wkati Fulani nakumbuka alikuwa amejaa makovu, tulipouliza ni makovu ya nini walituambia jinsi amabavyo alikuwa akianguka motoni, na kwenye maeneo mengine mababaya, kumbuka sio mapenzi ya Mungu uishi hivyo hata kidogo. ELEWA WAZI KUWA MWANA WA MUNGU YESU ALIDHIHILISHWA APATE KUZIVUNJA KAZI ZA IBILISI, kwako binafsi,kwa mme wako,kwa watoto wako, kwa mke wako, na hata kwa wazazi wako.
Yesu alipo mfungua mwenye pepo la udhaifu
"uka 13:10 siku ya sabato alikuwa akifundisha katika sinagogi mojawapo. Na tazama, palikuwa na mwanamke aliyekuwa na pepo wa udhaifu mda wa miaka kumi na minane, naye amepindana, hawezi kujinyosha kabisa. Yesu alipomuona alimwita, akamwambia, Mama umefunguliwa katika udhaifu wako, akaweka mkono juu yake naye akanyoka saa iyo, akamtukuza mngu. unaweza kuona kifungo cha huyu mama ilikuwa ni mgongo kupinda kwa mda wa miaka 18 japo sijui mamepo haya yalitaka yakae humo kwa mda gani, maana kama isingekuwa ni Yesu kumfungua huyu mama ni wazi kuwa yangeendea kukaa na kuendelea kumtesa huyu mama. Unapoendelea kufuatilia mafundisho haya endelea kutafakari ni kifungo gani kimekuwa kikikutesa kwa mda mrefu alafu amini Yesu yuleyule aliyeponya kipindi kile yuko teyari kukuponya na wewe leo, ukisoma Rumi 10:11 anasema " kwa maana andiko lanena kila amwaminiye hata tahayarika,…"
KWA MTU ALIYEOKOKA MAOMBI YA VITA NI MUHIMU KATIKA KUPINGANA NA HILA ZA ADUI.
Mtumishi wa Mungu mmoja nchini Marekani alizungumza hivi kwa lugha ya kiingereza ni maneno muhimu sana akasemaif thdevil has declared the war, we to declare the war against the devil" ikiwa na maana ikiwa shetani ametangaza vita, sisi nasi tunatangaza vita dhidi ya shetani, iko hivi kama Adui yako ametangaza vita dhidi yako hii ina maana amejiandaa, sasa wewe usipojipanga kukabiliana naye hii ina maana atakumaliza tu, lakini kama ukijipanga kwa vita, hata kama yeye ndiye aliye tangaza vita utamshinda tu. Ni muhimu ukafahamu kuwa shetani kila wakati anafanya vita na watoto wa Mungu. Lakini pamoja na hayo sisi ni washindi tunashinda na zaidi ya kushinda, "saya 42:13 Bwana atatokea kama shujaa ataamsha ataamsha wivu kama mtu wa vita,,,,,,,,,,,Atawatenda adui zake mambo makuu," Adui wa Bwana ni roho za giza zinazotesa na kusumbua maisha yako leo.
Maombi ya vita yakoje??
Ndugu mpendwa unayefuatilia mafundisho haya Maombi ya vita ni maombi ya kupambana katika ulimwengu war oho ukipambana na roho za giza, mapepo, na falme zote za giza
Aina hii ya maombi si aina ya tofauti na maombi mengine isipokuwa tu saa hii unakuwa katika hali ya vita ukikataa manyanyaso ya adui kwenye maeneo mbalimbali ya maisha yako, ukiamuru roho za giza kuachia maisha yako, watoto wako, mme wako, na hata biashara yako
Watu wengi waliokoka leo wangependa sana kuombewa, kitu amabacho ni chema isipokuwa unahakika gani kuwa unaombewa? Fikilia uko katikati ya maadaui na unategemea mtu mwingine awapige maadui kwa niaba yako na kwa sababu hajui uko kwenye hatari ya namna gani anaamua kufanya uzembe uwe na hakika utaangamia, hii ndio sababu ulipewa mamlaka dhidi ya nguvu zote za yule adui Math 10:1 Akawaita wanafunzi wake kumi na wawili, akawapa amri juu ya pepo wachafu , wawatoe, na kupoza magonjwa yote na udhaifu wa kila aina,
Ndani ya kila mtu aliyeokoka na anaye ishi maisha ya uaminifu mbele za Mungu, iko mamlaka na nguvu ya utiisho dhidi ya ibilisi na ndio sababu Biblia pia ikasema tutakayoyafunga Duniani yatakuwa yamefungwa na mbinguni, na tutayo yafungua duniani yatakuwa yamefunguliwa na Mbinguni hii ina maana ndani ya mtu aliyeokoka kuna ufunguo wa kufungua mambo kwenye ulimwengu war oho,
Sasa watu wengi waliokoka leo hawana mda wa kukaa kwenye maombi na kupingana na na hila za adui kwenye maisha yao.
Na ndio sababu tunahamasisha mtu binafsi aliyeokoka kuwa na mda wa kupinga hila za shetani kwenye maisha yake kila inapoitwa siku, ukisoma katika Waefeso 6:10 anasema hatimae mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake. Sasa huwezi kuwa hodari katika Bwana kama huna mda wa maombi na kama huna mda wa maombi hii ina maana hauna ulinzi kwenye maisha yako maana ulinzi wa Mungu juu yako unategemea namna unavyopingana na adui kwenye maisha yako.na ukisoma mstari wa 11 utakuta anasema " vaeni siraha zote za Mungu mpate kuweza kuzipinga hila za shetani" sasa hii inakupa kujua kuwa kuna umuhimu wa kukaa kwenye maombi tena si kwa namna ya kawaida ili uweze kuzipinga hila za adui kwenye maisha yako,
Ukisoma mstari wa 12 utakuta anasema "maana kushindana kwetu si juu ya damu na nyama bali ni juu ya falme na mamlaka juu ya wakuu wa giza hili juu ya majeshi ya pepo wababaya katika ulimwengu wa roho"
Sasa unapoingia kwenye maombi ya vita ni kama askari anayeingia vitani, maana ni kwenye maombi haya ndiko ambako kuna kuamuru vitu Fulani vitokee au vizitokee, Yoeli 3:9-10 anasema " tangazeni haya kati ya mataifa takaseni vita, waamsheni mashujaa, watu wa vita na wakalibie na wapande juu yafueni majembe yenu iwe mikuki, aliye dhaifu na aseme, mimi hodari,
Maadamu umeokoka usijidharau amini tu kuwa kila unachokiamulu katika ulimwengu wa roho kwa mamlaka ya jina la Bwana kinatokea na ndia sabubu Biblia ikasema aliye dhaifu na aseme mimi hodari,
Maombi ya vita ni maombi ya kuvuruga mipango ya shetani kwenye maisha yako na familia yako hata taifa lako haya si maombi ya siku moja ni maombi ambayo unahitaji kufanya kila siku, maana ndani yake kuna ulinzi wa familia, kuna uponyaji wa ndoa, kuna ulinzi wa biashara yako na mambo mengine ambayo adui anayatafuta kwenye maisha yako kila siku.
Anayeomba maombi haya ni lazima awe ni yule anayeishi maisha matakatifu mbele za Mungu
Efeso 6:14 anasema Basi simameni hali mmejifunga kweli viunoni, na kuvaa diriiya haki kifuani, jitahidi kuwa mtu wa kweli na mwenye haki mbele mbele za mungu sasa endelea na kufungiwa miguu utayari upatikanao kwa injiri ya amani zaidi ya yote mkitwaa ngao ya imani amabayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu
Hili ni jambo la muhimu kulielewa kuwa kila siku kuwa kunakuwa na mishale yenye moto toka kwa mwovu inayotumwa kwenye maisha yetu hivyo basi ni maombi tu ya kupingana na Adui kwenye maisha yetu ndio yaletayo msaadamstari wa 18 " kwa sara zote na maombi mkisali kila wakati katika roho, mkikesha kwa jambo hilo,,,,,,,"
Hivyo basi jifunze kuwa na muda maarumu wa kusogea mbele za Mungu kama askali wa vita kuhani na mfalme,ukijiweka wakfu kwa Bwana ukiweka wakfu nyumba yako,familia yako, na hata kazi yako.
Uwapo kwenye maombi haya amabayo ni mapambano kati yako na nguvu za giza tumia JINA LA YESU, DAMU YA YESU,
Ni muhimu kufanya yafuatayo kabla ya kufanya maaombi haya
Omba toba kwa Bwana ili kusiwe na ushitaki wowote wa adui juu yako, pata mda wa kujitakasa Isaya 1:16 jiosheni jitakaseni ondoeni uovu wa matendo yenu usiwe mbele ya macho yangu.
Usiingie kwenye maombi haya na hali unakinyongo na mtu moyoni hakikisha unasamehe "marko 11:26 lakini kama ninyi hamsamehee,wala baba yenu aliye mbinguni hata wasamehe ninyi makosa yenu."
Kumbuka haya ni maombi ya imani, amini tu kuwa unachokiamuru kwenye ulimwengu wa roho ndicho kinacho fanyika hata kama hauoni kwa macho Ebran 11:6 lakini pasipo imani haiwezekani kumpendeza;yoyote amwendeae Mungu yapasa aamini ya kwamba Mungu yuko na kwamba huwapa thawabu wale wamtafutao
Pia imeandikwa katika kumbu 28:7 "Bwana atawafanya adui zako wainukao juu yako kupigwa mbele yakowatakutokea kwa njia moja lakini watakimbia mbele yako kwa njia saba"
Hivyo basi iko namna maadui watakuwa wakishigulikiwa katika ulimwengu wa roho mara utapokuwa ukifanya maombi haya.
Futa kwa damu ua Yesu maneno mabaya uliyotamkiwa
Ni katika maombi haya unakotakiwa kufuta kwa damu ya Yesu kila aina ya maneno uliyotamkiwa futa maneno ya laana, mikosi, mabalaa, futa maneno mabaya kwa watoto wako kwa mke wako, kwa mme wako,
Futa kwa damu ya Yesu mambo mabaya ambayo hayataki kuiachilia nafsi yako, kunavitu uliwahi kuvisikia vikafanyika mzigo kwako, kunapicha uliwahi kuona, mapicha ya uchawi,mapicha mauti, mapicha ya uzinzi, futa kila kila kitu uwapo katika maombi haya.
Ni katika haya maombi unakoweza kukataa aina yoyote ya udhaifu iliyoko ndani yako bila msaada wa mtu mwingine ukaomba mwenyewe, ukapambana mwenyewe.
Mfano wako watu wanasumbuliwa na hofu ya mauti yaani kila wakati anaona yeye atakufa mda wowote ni roho tu ya adui ambayo ukijipanga kwenye maombi haya inakuachia, kataa kwa jina la Yesu tumia na damu ya Yesu zisomee roho za giza zab 118:17 "sintakufa bali nitaishi nami nitayasimulia matendo ya Bwana" kumbuka kibiblia siku zako za kuishi ni miaka 70 ukiwa na nguvu 80.
Ni katika maombi haya unaweza ukakataa magonjwa yanayoonekana kuutesa mwili wako wako tulifanya huduma na binti aliyekuwa akitokwa na damu maeneo ya siri kwa mda mrefu baadae tukagundua ilikuwa ni Roho za giza tu, badae tukagundua roho za giza zinasababisha mabinti wengine wasione siku zao, sasa yapo magonjwa mengine ni ya kawaida mengine sio ya kawaida ni katika maombi haya kila kitu kitu kinafanyika maana unapambana kwenye ulimwengu wa roho.Ni katika maombi haya unaweza ukakataa roho ya uchungu na hali ya kukataliwa
Ni katika maombi haya unaweza ukatakasa mavazi yako, vifaa vyako maana si kila tunachonunua Dukani au kwenye mtumba ni salama,
Pia maombi haya huzuia mapepo ya kulushiwa, Maana hakuna pepo litakalotumwa kwako na kufanikiwa.
Maisha ya maombi husababisha ulinzi na amani hata kama kuna roho za adui zinatenda kazi, Mambo ya walawi 26:6 nami nitawapa amani katika nchi tena mtalala wala hapana atakaye watia hofu……"
Hii ni mifano ya maombi ya vita
Jipangie muda inaweza kuwa Dakika 15 ukiwa na nguvu dakika 30 wapo wanaoweza kukaa kwa saa nzima, endapo unanena kwa lugha ni vizuri ukaomba pia kwa kunena kwa lugha.
Katika jina la Yesu, ninakataa kila aina ya mipango ya uharibifu wa shetani kwenye maisha yangu, manyanyaso na mateso,laana, mikosi, mabalaa, katika jina la Yesu, achieni maisha yangu, kwa Moto wa Roho mtakatifu, Nawaamuru ninyi roho za giza achieni baraka zangu, achieni uponyaji wangu, kwa Damu ya Yesu achieni maisha yangu, kila aina za roho za giza mnaosababisha mwili wangu ushindwe kutulia kwenye uwepo wa Mungu niachieni sasa, kwa kinywa changu ninawakana, hata kama mliwai kupata nafasi kwenye maisha yangu, leo ninawakana, na ninawasaliti, kwa jina la Yesu,
Kwa Damu ya Yesu ninajifunika, kwa mamlaka niliyopewa na Bwana Yesu, ninajitangazia baraka, kwa jina la Yesu nakataa hali yoyote ya kushindwa, kutokufanikiwa, najitangazia maisha marefu kwa jina la Yesu, najitangazia utajiri badala ya umasikini, kwa Jina la Yesu, maana neno la Bwana limesema aliyachukuwa masikitiko yetu, alifanyika masikini ili sisi tuwe matajili, na kwa kupigwa kwake sisi tumepona kwa jina la Yesu ninajitangazia mafanikio na uwepo wa nguvu za Mungu maishani mwangu. Lihimidiwe jina la Bwana kwa sababu Bwana ameyatenda haya. Ameni
Wewe unaweza ukaomba mambo mengi zaidi hayo kwa kadri ya kiu yako na uhitaji wako omba mpaka uone kiu yako inaisha kulingana na muda wako uliojipangia.
Baada ya maombi haya amini, omba maombi ya aina hii kila siku, sasa aina hii ya maombi inaweza ikawa ni sehemu tu ya maombi yako unayoomba kila siku, aina maana uombe hivi tu kila siku, maana unahitaji kuombea mambo mengine.

FAIDA ZINAZOTOKANA NA MAOMBI YA VITA
Maombi haya yanazima mishale yenye moto toka kwa adui ambayo ingeelekezwa kwenye maisha yako, mishale yenye moto ni kama kusingiziwa, kuibiwa, kusimamishwa kazi bila sababu, kuchukiwa ofisini bila sababu yoyote, kuachwa na mchumba au arusi kuvurugika, ndoa kuvunjika, na yafananayo, hii yote ni mishale ya mwovu kwenye maisha yako sasa maombi ya vita huwa yanakwenda kwenye ulimwengu wa roho na kuizima hii mishale ya mwovu.
Roho za giza kushindwa kuvamia hata kama ziliamriwa kufanya hivyo, maombi haya hufunga ajali, huzuia mauti, ukisoma Mtend 12:5 basi Petro akalindwa gerezani, nalo kanisa likamuomba Mungu kwa juhudi kwa ajili yake" haya hayakuwa maombi ya kawaida maana herode alikuwa amekwisha kumuua yakobo kwa upanga, kanisa likajua yamkini petro angefuata ndipo walipoamua kuingia kwenye maombi ya kuzima ile hila juu ya petro.Biblia inaonyesha wazi kuwa usiku ule ule malaika wa Bwana akashuka gerezani.
Ni kwa maombi haya vifungo mbalimbali vya adui huwa vinamwachia mtu na minyororo kufunguka kwenye maeneo mbali mbali ya maisha ikiwa anapata mda wa kuomba maombi haya.
Ni maombi haya amabayo yakielekezwa mahali yanasababisha watu waache pombe, sigara, ukahaba maana kuna watu walisimama kwenye ulimwengu wa roho kupingana na zile hila za adui kwenye maisha yao, na kungoa mizizi ya tamaa ikiwa ni pamoja na kuikata ile kiu ya pombe, sigara, ikiwa ni pamoja na tamaa mbaya.
Mara baada ya maombi haya watu hujisikia wepesi mwilini na hata katika ulimwengu waro pia Amani moyoni ikiashiria vifungo vimefunguka.

Naamini mpaka sasa Bwana atakuwa amefanya kitu kikubwa sana kwenye maisha yako, ikiwa ni ukombozi kwenye maeneo mbalimbali ya maisha, hivyo basi ingia kwenye maombi ya kumshukuru Mungu ukimwambia asente kwa ajili ya ufunuo aliokupa kupitia mafundisho haya,
Ndugu msomaji itakuwa ni vema endapo utapata nafasi ya kuniombea ukimsii Mungu anipe mafunuo zaidi, katika wito huu, anilinde na kunipa uzima ikiwa ni pamoja na kunifungulia mirango ya baraka.
Ombea mfululizo unaofuata wa masomo haya ujulikanao kama: Unavyoweza kuwa Mshindi dhidi ya mapambano tuliyonayo katika ulimwengu wa Roho.
Usisite kutuma ushuhuda wako
Kupitia mawasiliano yafuatayo
Mwl: Tuntufye Andew mwakyembe

Email tumsifu_Andrew@yahoo.com simu 0784 629562 na kwa uhitaji wa maombezi youth_ prayernet@yahoo.com pia C/o S.L.P 55 USA RIVER ARUSHA
ENDAPO UMEGUSWA NA HUDUMA HII NA UNGEPENDA KUPANDA MBEGU KWA KUSAIDIA KULIPIA SEHEMU YA GHARAMA
usisite kuwasiliana nasi.au waweza kutumia account No.016201033820 NBC.MBEYA BRANCH.
Kwa maelezo zaidi tumia Email ifuatayo yagotm28@yahoo.com

SHUHUDA

Bwana asifiwe Mwl Tuntufye, pole na huduma, kitabu chako cha "SABABU 12 WATU KUKATA TAMAA KUIJERUHIKA NA KUPOTEZA MATUMAINI" kimenifanya nijione ninanafasi kubwa sana hapa duniani sikuwahi kujua hayo.
Nimefurahi sana najisikia huru mno Mungu akulinde na akufanikishe katika yote.

Napenda kutoa shukrani zangu za dhati kwa kwa Mungu kwa kazi unayoifanya maneno ya Mungu unayofundisha yamekuwa faraja kubwa sana kwangu kwangu.
Nikiwa nasoma kitabu ulichoandika kiitwacho "PAMBANA DHIDI YA NGUVU ZA GIZA" gafla nguvu za Mungu zilinishukia nikajikuta naanza kunena kwa Lugha, na kujaa nguvu za Mungu kwa mara ya kwanza, mpaka leo nafanya huduma za kuwaombea wenye nguvu za giza na nimesimama kiroho.

Mungu asifiwe ubarikiwe kwa ujumbe unaoutoa kwenye gazeti juu ya majaribu na kukata tamaa maana mara nyingi nilikuwa nikiwa katika hali hiyo naomba mniombee

Baada ya kusoma mafundisho mbalimbali aliandika hivi.
Nimefika hatua ya kuchoka natamani kulala katika kristo kwani nilianza na kristo toka utoto kila hatua nimemtegemea yeye amenionyesha baraka kubwa sana rohoni lakini mwilini sivioni ninampenda sana Yesu sasa ni zaidi ya miaka kumi kumi Moyo umechoka, nataka kuona mwilini la nilale nimechoka. Lakini Yesu alimsaidia.

Baada ya kusoma makala zenu kwenye gazeti na mafundisho kwenye vitabu nimepata nguvu za kusoma neno na kuomba Mungu awababriki sana
KARIBU NAWE UTUTUMIE USHUHUDA WAKO. KUPITIA MAWASILIANO YETU.

KIONGOZI WA KANISA LA FULL GOSPEL BIBLE FELLOWSHIP


Askofu Zakaria Kakobe.

KONGAMANO LA WANAFUNZI MJINI TANGA

Moja ya kongamano la wanafunzi alilolifanya Tanga Mwl.Tuntufye

SOMO LA LEO

ITAMBUE MILANGO YA KUTOKEA

UWAPO KATIKATI YA MAJARIBU NA HALI YA KUKATA TAMAA
Habari yako ndugu msomaji wa mafundisho haya, naamini ni kwa neema na huruma za Mungu kuwa leo tena tumepata nafasi ya kusogea mbele zake mungu ili tuweze kujifunza kitu kutoka kwake ambacho naamini kitakuwa na nafasi kubwa sana katika kubadilisha mifumo ya imani zetu na kujifunza kumuamini na kumtegemea Yesu peke yake bila kujalisha tunakutana na hali ya namna gani katika maisha yetu ya kila siku,
Kwako mpendwa msomaji
Majaribu na magumu tunayokutana nayo siku kwa siku si kwa ajili ya kutufadhaisha, kutuumiza, kutuvunja moyo, na hata kutuondoa kwenye mpango wa Mungu na hatimae kutupeleka jehanamu .Nivizuri ukaelewa hili siku zote kuwa, huo si mpango wa Mungu hata kidogo; lengo la Mungu, wakati mwingine anaporuhusu tujaribiwe ni kutaka kuimarisha imani zetu, kujitwalia utukufu, kujitukuza, kuwafanya wengine wamuamini na kumtegemea yeye tu kwa sababu ya muujiza uliofanyika kwako au utakao fanyika kwako maana upo muujiza utakaofanyika kwako mara baada ya kusoma mafundisho haya.

HIZI NI MOJA YA SABABU ZINAZOWEZA KUKUFANYA UPITIE KATIKA MAMBO MAGUMU

Ili ukue kiroho,Kiimani na uje kuwa msaada kwa wengine na hatimae kuyafikia yale Mungu aliyoyakusudia kwenye maisha yako, Ni vizuri ukafahamu kuwa kiwango chako cha kumuamini na kumtegemea Mungu kinategemea mambo yafuatayo, kama umemuona Mungu akikutetea katika madogo utamuamini katika hayo hayo madogo na utamtia moyo mtu mwingine katika hayo hayo madogo unayo yafahamu kuhusu Mungu na uweza wake.
Lakini kama Mungu amekuwa akionekana kwako katika makubwa na yaliyo onekana kuwa mazito kwako na yakukatisha tamaa kisha ukavuka salama, hutaacha kumuamini Mungu hata katika hilo lingine linaloonekana kuwa kubwa zaidi kwako, na kuwa na ujasiri wa kumtia moyo mwingine anaye pitia hayo, ndio sababu mtume Paulo alikuwa na ujasiri wa kumwambia Timotheo kuhusu magumu aliyokutana nayo na jinsi Mungu alivyo mtetea. Ukisoma 2Timoth 4:14-18 anaeleza, "Iskanda, mfua shaba,alionyesha ubaya mwingi kwangu;Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake nawe ujihadhari na huyo, kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu". Tunaona Paulo akiendelea kumueleza Timotheo kilicho tokea na hali ilivyokuwa na kitu anachotakiwa kujifunza katiaka hayo ukiendelea mstari wa 16 anaendelea "katika jawabu langu la kwanza hakuna mtu aliye simama upande wangu,bali wote waliniacha; naomba wasiesabiwe hatia kwa jambo hilo. Lakini Bwana alisimama pamoja nami akanitia nguvu,ili kwa kazi yangu ule ujumbe utangazwe kwa utimilifu,hata wasikie mataifa yote; nami nikaokolewa katika kinywa cha simba Bwana ataniokoa na kila neno baya,na kunihifadhi hata nifike ufalme wake wa mbinguni.utukufu una yeye milele na milele Amina" .Fikiria Kama Paulo asingekuwa ameyapitia hayo magumu, Kama angekuwa na kitu cha kumwambia Timotheo, anazungumzia habari ya Iskanda alivyoonyesha ubaya mwingi, anaendelea kumueleza jinsi alivyotegemea baadhi ya watu wangeweza kumtia moyo na kusimama pamoja nae na vile amabavyo hakuna mtu aliye simama upande wake. Kwa tafsiri nyingine inawezekana kabisa aliowategemea ndio waliomsaliti, tu kwa sababu ya kulisimamia kusudi la Mungu, na inafika mahari anaelezea kuwa aliokolewa na kinywa cha Simba ukiona anelezea haya yote uelewe wazi kuwa hayakuwa mapito ya kawaida, lakini pamoja na hayo tunaona Paulo akimtia moyo Timotheo kwa kumwambia kuwa pamoja na hayo yote Bwana alisimama pamoja nami akanitia Nguvu, akaniokoa na kinywa cha simba, ukiufuatilia ule mstari wa 18 anasema, "Bwana ataniokoa na kila neno baya." Kitu Paulo alichokuwa anasisitiza hapa kwa Timotheo ni kama Bwana alinipigania katika yote hayo hataacha kuniokoa na kila neno baya, hii inaonyesha alikuwa bado anaendelea na huduma na bado kulikuwa na magumu yanamkabili lakini alimtia Moyo Timotheo kuwa kama Mungu aliniwezesha huko nyuma hataacha kuniokoa na kila neno lililo baya. Leo hii wewe ni shahidi jinsi ambavyo watumishi Mbali mbali wamekuwa wakieleza jinsi walivyo pita katika magumu na hatimae Mungu akawasaidia. Kumbuka, kama wasingekuwa wamepitia hayo magumu, leo wasingalikuwa na kitu cha kukutia moyo na hata kukusaidia wewe kuvuka.
Wakati mwingine magumu hutokea ili kupanda Daraja kutoka imani uliyopo kwenda nyingine, kutoka utakatifu kwenda utakatifu na pia ili Mungu akuamini, Ni muhimu kufahamu kuwa hata wewe mwenyewe unapotaka kumuamini mtu ungependa kumpa mtihani japo tu kumpima uwezo wake, au kufanya jambo ambalo litapima endapo unachokiona kwake ndivyo kilivyo au ni cha kuigiza tu ili usije kumuamini kabisa na kumbe sivyo alivyo. Walimu wanaofundisha madarasani wanaelewa jinsi ambavyo kipimo cha kujua watu walielewa au la ni mtihani tu, na si vinginevyo, na mwanafunzi asiyetaka mtihani maana yake hataki Shule na hayuko tayari kwenda darasa lingine.Sasa ukisoma Yakobo 1:12 utakuta anasema "Heri mtu yule astahimilie majaribu; kwa sababu akisha kukubaliwa ataipokea taji ya uzima,Bwana aliyowaahidia wampendao."Nilipenda uone huu mstari unaosema akiisha kukubaliwa, hii ina maana kuwa ili Mungu akuinue, akuamini na akukubali unahitajika kushinda majaribu na sio kuishia tu kusema shetani alijiinua., Sasa ukisoma Warumi 5:3 utakuta anasema ,"wala si hivyo tu,ila na tufurahi katika dhiki pia;tukijua kuwa dhiki kazi yake ni kuleta saburi;na kazi ya saburi ni uthabiti wa moyo; na kazi ya uthabiti wa Moyo ni tumaini ,,,,,,,,,," ukiufuatilia huu mstari kwa makini utakuta unakutaka ufurahie jaribu,shida,au tabu yoyote unayokutana nayo, Nini sababu hasa? Sababu ni kuwa baada ya kushinda hilo jaribu, liko Tumaini, ipo faraja,na hatimae kukua kiroho, nakumbuka jinsi ambavyo tulipokuwa chuoni nikifanya masomo yangu ya awali, hakuna mtu alipenda kurudia mtihani{suplimentary} kama kuna kitu wanafunzi waliopo vyuoni huwa wanaomba usiku na mchana ni kutokuwa na sup maana wanaona inawapotezea muda lakini wale wanaorudia mtihani fulani wakisha kuufaulu vizuri huwa wanakuwa na uwezo mkubwa wa kumsaidia mwingine kwenye lile somo kuliko hata wale ambao hawakurudia mtihani. Hivyo unaweza ukapitia gumu fulani ili uwe na uwezo mkubwa wa kuwasaidia wengine.
Wakati mwingine majaribu huja, ili upate kuwa mkamilifu.
Ukisoma katika Yakobo 1:4 anasema "Saburi iwe na kazi kamilifu,mpate kuwa wakamilifu na watimilifu bila kupungukiwa na neno." Ni wazi kabisa kuwa baada ya kupita kwenye majaribu na mambo fulani yaliyoonekana kuwa magumu kabisa kwako halafu ukatoka salama, huwi tena kama ulivyokuwa hapo awali, maana ndani yako kunakuwa kumejengeka imani juu ya Mungu aliye kufanikisha, na walio wengi sana huanza kusimama kiroho baada ya kushinda vikwazo alivyokutana navyo. Mara nyingi imetokea watu wanapotoka kuokoka, wengine walipotengwa na marafiki,wazazi, kuchekwa ,kuchukiwa, kupewa majina Fulani Fulani ya dhihaka, hii ndio iliwasababisha kukaa kwenye maombi na kulisoma neno, na kwa sababu tu umeokoka kila unachofanya wanataka wachunguze kama ndivyo walokole huwa wanafanya au la,lakini ukifuatilia kwa umakini wengi hii ndio imewasaidia kusimama maana kila wakati wanajua kuna watu wanamtazama, hii inamsaidia kusimama kwenye maombi na kuwa mkamilifu mbele za Mungu, baadae nae anakuwa na ujasiri wa kumshauri mwingine. Nini kimemsaidia? Ni kuwa yale Magumu aliyokutana nayo awali yalisaidia kuujenga msingi wa utimilifu. Mtume Paulo alifika mahali akasema "nimevipiga vita vilivyo vizuri vya imani mwendo nimeumaliza imani nimeilinda." Ni kitu gani kilimpa ujasiri wa kusema amevipiga vita vilivyo vizuri vya imani na kwamba mwendo ameumaliza alafu imani ameilinda?Ujasiri huu ulikuwa ni kutokana na magumu mengi ambayo alikuwa amekutana nayo, na kuwa pamoja na hayo hakumuacha Yesu isipokuwa yakamfanya amtafute Mungu zaidi na kukaa zaidi katika hali ya kutaka kumuona Mungu akijidhihirisha kwake.Hivyo basi ni vizuri ukafahamu kuwa hatuwezi tukawa wakamilifu kama hatuta kabiliana wakati mwingine na vitu vya kutuvunja Moyo na vya kutukatisha tamaa kabisa kuna msemo mmoja husema kuwa"ili dhahabu ihakikiwe kuwa ni dhahabu safi hupitishwa kwenye Moto" kwa hiyo Moto ni kipimo cha kujua kama hiyo dhahabu ni ile safi au la. Ukisoma katika Isaya 43:1 anasema, "Lakini sasa, Bwana aliyekuhuluku,e Yakobo yeye aliyekuumba,e Israeli asema hivi, "Usiogope,maana nimekukomboa;nimekuita kwa jina lako wewe u wangu.".Sasa ukiufuatilia ule mstari wa pili utakuta anasema, "Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe na katika mito haitakugharikisha;uendapo katika moto hutateketea wala mwali wa moto hautakuunguza."Kitu ninachotaka ukione hapa ni hiki, Mungu anapoanza kujitambulisha kwako na kukuambia Usiogope maana nimekuita, tafsiri nyingine ya neno nimekuita inaweza ikawa nimekuchagua, sasa anapokuambia Usiogope maana yake ni kuwa anakutaadharisha, maana viko vitu utakutana navyo vitakuogopesha na anaposema upitapo katika maji mengi, maji mengi tunaweza tukayafananisha na misukosuko ya maisha. Mambo magumu kwenye maisha na vitu vya kukatisha tamaa .

japo pamoja na hayo alisha kuambia usiogope, na pia anaposema mito haitakugharikisha anamaana matatizo utayokumbana nayo hayata kufanya umuache Mungu kwa sababu yeye yu pamoja nawe,na anaposema uendapo katika moto hauta teketea ina maana kuna wakati utatakiwa kupita katika moto na mambo yatakayo kusababishia uchungu kabisa katika nafsi yako, lakini alisha kuambia kabisa, Usiogope maana yeye yu pamoja nawe katika vipindi vyote hivyo. Ndugu mpendwa unayefuatilia somo hili ni muhimu ukatambua kuwa mambo magumu ni sehemu katika maisha yetu Ili tukamilike, tuimarike na hatimae kukifikia kimo cha kristo.
Wakati mwingine magumu huja ili umtambue Mungu kwa sura nyingine, ambayo hujawahi kumuona akijidhihirisha kwako na hasa baada ya kufika mahali umekata tamaa kabisa.Sehemu nyingi Mungu alipotaka kujidhihirisha Kwa wale wasomaji wa Biblia watakubaliana nami kuwa kulitokea tatizo ambalo liliwafanya watu walie, wafikirie,wachanganyikiwe,watumie mda mwingi kuwaza tena bila kupata majibu, ukikumbuka habari za Esta baada ya chukuliwa mateka kutoka Yerusalemu wakiwa huko shushani ngomeni tena kama wakimbizi maana haikuwa nchi yao, Mungu anampa Esta kuwa malkia kwenye nchi ya watu akiwa yeye na kundi zima la Wayaudi walioingia huko kama mateka, baada ya kujisahau na kufurahi kuwa hata kama ni mateka bado wanaishi kwa amani kama vile wako kwao, na mtu wa kwao ndio amepewa umalkia, sasa wakiwa katika hali hii gafla inatokea kuwa wanatakiwa kuuwawa wayaudi wote mimi sijui kama kuna jaribu gumu kama lile la kutakiwa kuuwawa ukisoma Esta 3:8-11 anasema "Basi Haamani akamwambia mfalme Ahasuero, kuna taifa moja waliotawanyika na kukaa mahali mahali katikati ya mataifa walioko katika majimbo yote ya ufalme wako.na sheria zao zimefarakana na sheria za kila Taifa wala hawazishiki amri za mfalme ;kwa hiyo aimpasi mfalme kuchukuliana nao. Tunaona jinsi ambavyo Haamani haikumsumbua Esta kuwa malikia wa mfalme alichotaka hapa ni kutimiza hazma yake ya wayahudi kuuwawa tu, ukiendelea mbele kidogo inaonyesha wazi kuwa alikuwa ni Adui wa wayahudi hivyo akatengeneza maneno ya uchochezi ili tu wayaudi wauwawe, ukiendelea mstari wa tisa anasema basi mfalme akiona vema na iandikwe kwamba waangamizwe; nami nitalipa talanta kumi elfu za fedha mikononi mwao watakao simamia shughuli hiyo,waziweke katika hazina ya mfalme .ndipo mfalme alipoivua pete yake mkononi akampa hamani bin Hamedatha,mwagagi adui ya wayahudi. Kisha mfalme akamwambia hamani, hiyo fedha umepewa, na watu pia, fanya uonavyo vema. Sasa ukisoma ile sura ya 4 mstari wa 3 anasema "na katika kila jimbo ambako amri ya mfalme na mbiu yake imewasili palikuwako na msiba mkuu kwa wayahudi na kufunga na kulia na kuomboleza hata na wengi wakalala juu ya magunia na majivu" hii mistari inaonyesha walichanganyikiwa kabisa maana imeshatangazwa wanasubiri kifo na mfalme akisha pitisha amepitisha. Biblia inaposema "palikuwako na msiba mkuu", ujue haikuwa kilio cha kawaida wengine walijuta kuzaliwa,wengine lazima walitamka maneno magumu,maana hawakuona kingine isipokuwa mauti mbele yao, lakini hapa ndipo Mungu alipotaka kujidhihilisha kwao. Baadae ukiendelea kusoma utaona jinsi Mungu alivyowatendea miujiza wakaendelea kutawala na kumilki na hali waliingia kama mateka. Hivyo basi wakati mambo ya kukukatisha tamaa yanapo tokea na wakati mwingine utatuzi wa kibinadamu unapokataa ni vizuri ukamtumaini Mungu na kumfanya ajidhihirishe kwako. Yohana 14:21 anasema, "Yeye aliye na Amri zangu na kuzishika yeye ndie anipendae; nae anipendae atapendwa na baba yangu nami nitampenda na kujidhihirisha kwake." Ni muhimu kutambua kuwa Mungu amehaidi kujidhihrlisha kwako.Hivyo basi lolote unalo kutana nalo ni vizuri ukakaa mkao wa kuona Mungu akijidhihirisha kwako.USHUHUDABinti mmoja aliyemtumaini Mungu kuanzia utoto wake na kumuona Mungu akimfanikisha katika masomo yake kuanzia kidato cha kwanza mpaka alipokuwa akiingia kwenye mtihani wa kidato cha sita hakuna siku alitegemea yale yaliyotokea yangempata hakuamini kuwa kwa jinsi ambavyo Mungu amekuwa akimfanikisha kuna siku angekuja kukutana na mambo magumu namna hii, maana mpaka anafanya mtihani wa kidato cha sita hakukua na tatizo lolote, sasa baada ya matokeo kutoka ikaonekana hajapata daraja la kwanza la pili wala la tatu na la nne, kwa lugha ya leo ya wanafunzi wangesema alizungusha maana yake alipata sifuri, hakuna mtu aliamini au kuelewa kilichotokea,wazazi pia hawakuelewa , binti huyu alikuwa katika wakati mgumu sana hakuelewa kitu cha kufanya akaanza kuwa kama anaugua maono yake yalikuwa ni kuja kusomea Udaktari, sasa anaendelea vipi na amepata sifuri? Wakati mwingine inasemekana alikuwa anajikuta tu ana vidonge vingi mkononi na anasikia kabisa sauti ikimwambia "Si ujiue tu kuna haja gani ya wewe kuwepo Duniani, kwanza ndoto zako ndio zimekufa, hata mchumba gani atakaye kupenda wewe na hiyo sifuri yako?" Mara nyingi alisikia kukatishwa tama. Sasa mama mmoja aliyeokoka ambaye pia ni Muombaji, alikuwa ni ndugu yake huyu binti ndipo aliposikia hayo yaliyokuwa yakitokea akaenda kumchukua na kuishi naeAkaanza kumpa matumaini huku akimwambia Mungu anaweza, bado suala lako la kuwa Dactari lipo palepale njia za Mungu si njia zetu, Mungu atakufanikisha tu usiogope. Yule Mama aliendelea kumtia moyo huyu binti siku hadi siku, alipokuwa akiendelea kuishi nae akamshauri akachukue fomu za kurudia mitihani huku yeye akimlipia kila kitu na wakati huo akamtafutia mahali ambapo huyu binti alikuwa akifanya nursing kwa kipindi alichokuwa akisubiri kufanya mtihani.
Haikuwa jambo Rahisi kwa huyu binti maana hata wale wenzake aliokuwa akiwashinda Darasani walikuwa wamepata alama nzuri wengine wameshapata vyuo vizuri lakini yeye aliendelea kujitia moyo kwa Bwana na kuendelea kumtumaini Mungu peke yake. Baada ya mwaka kupita yule binti akawa amefanikiwa kufauru ile mitihani aliyo irudia kwa arama za juu sana na pale alipokuwa akifanya nursing palitokea watu kutoka nje ya nchi ambao walikuwa wanahitaji watu wakawasomeshe udaktari Nchi za ulaya kutoka kwa wale manesi ambao na yeye ni mmoja wao walipohitajika watu watatu yeye alipita bila kipingamizi maana kwanza alikuwa amefauru vizuri ile mitihani aliyokuwa ameirudia na akawa anaelimu nzuri kwa pale, baadae akaenda kusomea udaktari tena nchi za Ulaya aliporudi akawa ni moja ya madaktari wachache wanaoaminika hapa Nchini. Hivyo basi Mungu anapokuwa ameruhusu jambo fulani litokee huwa anataka kujitukuza ni wazi kabisa kuwa huyu Dada inawezekana alipenda kusomea udaktari lakini hakutegemea ingekuwa ni Ulaya, ninachotaka ujue ni kuwa muujiza wako upo, usijali ni hali ya namna gani unayopitia Muamini Mungu.
Mtume Paulo alipokuja kugundua kuwa magumu aliyokuwa akipitia ni kwa ajili ya udhihirisho wa nguvu za Mungu kwenye maisha yake alifika mahali akafurahi hata alipopita kwenye matatizo ukisoma 2korinto 12:9 anasema "Nae akaniambia,Neema yangu yakutosha;basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi,ili uweza wa kristo ukae juu yangu.kwa hiyo napendezwa na udhaifu,na ufidhuli,na msiba,na adha,na shida,kwa ajili ya kristo.maana niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu." Sasa kwanini mtume Paulo akasema niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu maana yake ni hii, kila udhaifu uliokuwa ukija kwenye maisha yake ulikuwa na nafasi ya kumfanya aone nguvu za Mungu kwa namna ya tofauti,au aone miujiza totauti, au amtambue Mungu kwa sura tofauti. kila Mungu alipomsaidia katika mambo ya kukatisha tamaa aliyokutana nayo alipata nguvu kubwa ya kusonga mbele na kutojali magumu ambayo yamkini yangekuwa mbele yake, ndipo sasa akatambua na kusema "niwapo dhaifu ndipo nilipo na nguvu." Mungu alivyo jidhihirisha kwa Paulo
Saa hii Paulo na Sila wakiwa wamekamatwa na kupigwa sana kisha kufungwa kwa mikatale na wamewekwa gerezani hakuna mtu angeweza kukubaliana nami kwa kipindi kile kuwa Mungu aliruhusu yale yatokee kwaajili ya utukufu wake, yaani kwa ajili ya kujidhihirisha, maana kwa wasomaji wa Biblia ni lazima wataungana nami kuwa haikuwa mara ya kwanza kwa Paulo kuwekwa gerezani na Biblia inasema wazi kabisa kuwa kwa safari hii walikuwa wamepigwa sana na pia walikuwa wamefungwa kwa mikatale na si hivyo tu hebu soma hii uone Mat 16:22 anasema, "makutano yote wakaondoka wakawaendea makadhi wakawavua nguo zao kwa nguvu wakatoa amri wapigwe kwa bakora."Sasa sio rahisi sana kuelewa kuwa pamoja na hayo yote bado Mungu alikuwa pamoja nao inawezekana kabisa ungekuwa wewe au mimi tungesema kama ni kazi ya Mungu basi iache maana ni rahisi kufanyiwa mambo mengine na si kutolewa Nguo hadharani,yaani jana umemuongoza mtu sala ya toba hapo na una watoto wa kiroho, leo wanaona ukidhalilishwa tena kwa kutolewa nguo na kuchapwa bakora inaweza isiingie sana akilini ni ngumu kuelewa, mstari wa 23 anasema na "Walipokwisha kuwapiga mapigo mengi,wakawatupa gerezani,wakaamuru walinzi wa gereza wawalinde sana nae akisha kupata amri hii akawatupa katika chumba cha ndani,akawafunga miguu kwa mikatale.’Sasa kwa nini nasema muda wote huu Mungu alikuwa pamoja nao na aliacha tu yote hayo yatokee ili ajidhihilishe kwao na kwa wale waliowakamata. Ukisoma mstari wa 25 anasema "Lakini panapo usiku wa manane Paulo na sila walikuwa wakimuomba Mungu na kumuimbia nyimbo za kumsifu na wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza." Sijui kama unaona kama mimi ninavyoona kwamba kama wafungwa wengine walikuwa wakiwasikiliza inamaana Mungu alitaka hata hawa wafungwa waipate ile injili, Na je wangeipataje kama Paulo na Sila wasingekaa nao mle gerezani na wangekaeje gerezani kama yaliyotukia hayakutukia? Sasa ukiangalia ule mstari wa 26 anasema "Ghafla pakawa tetemeko kuu la nchi" kumbuka ni baada ya Paulo na Sila kumuomba Mungu na kumuimbia nyimbo za sifa na baada ya wafungwa wengine kuipata injili yao endelea"hata misingi ya gereza ikatikisika,na mara hiyo milango ikafunguka,vifungo vya wote vikalegezwa,"Hebu nikuulize swali, inamaana walipokuwa wakipita katika misukosuko Mungu alikuwa haoni na unafikiri hawakuomba wakiwa wanapigwa bakora? Sasa kwa nini Mungu alinyamaza halafu anakuja kufanya miujiza mikubwa huku mbele ya safari? Hii ni lazima Mungu alitaka kujidhihiriisha kwa nanmna ya tofauti, tena si kwao tu, isipokuwa na kwa maaskari na wafungwa wengine. Hebu tuendelee mstari wa 27 anasema "Yule mlinzi wa gereza akaamka,nae alipoona yakuwa milango ya gereza imefunguka,alitafuta upanga,akataka kujiua akidhani ya kuwa wafungwa wamekimbia ila Paulo akapaza sauti yake akasema, usijidhuru,kwa maana sisi sote tupo hapa." Sasa kwa nini nilisema Mungu alikuwa na kusudi pia maaskari na wafungwa wapate injili ili pia waokoke. Mstari wa 26 anasema "akataka taa ziletwe yule polisi sasa akirukia ndani, akitetemeka kwa hofu,akawaangukia Paulo Sila, kisha akawaleta nje akasema Bwana zangu,yanipasa nifanye nini nipate kuokoka?wakamwambia mwamini Bwana Yesu nawe utaokoka pamoja na nyumba yako." Sasa ukiendelea kusoma yaliyotokea hapo mbele utaona jinsi ambavyo usiku uleule Yule mlinzi wa gereza akawapeleka nyumbani kwake Paulo na sila, na Biblia inasema watu wote wa nyumbani mwake yule Askari waliokoka na yeye mwenyewe Askari ndie akawahudumia kuwaosha mapigo yao akina Paulo na nyumba nzima wakabatizwa siku hiyo hiyo na Biblia inasema akawaandalia chakula. Sasa sitaki kuelezea zaidi kilichoendelea kutokea isipokuwa Mungu alifanya maajabu na ishara nyingi sana kwa Paulo na Sila baada ya tukio hili.
Kitu ambacho ninatamani ukifahamu ni hiki, kuwa wakati mwingine unapokabiliana na magumu tena ambayo hujawahi kuyategemea kabisa sio rahisi kufikiri kuwa eti Mungu anaweza akawa anataka ajidhihirishe katika hilo na kuwa bado Mungu yupo pamoja nawe. Wengi huona Mungu yupo mbali kabisa na amewaacha lakini Mungu anasema katika Yeremia 23:23, "Mimi ni Mungu aliye karibu mimi si Mungu aliye mbali." Na wengine huanza kutafuta ni wapi wamekosea, hii ni nzuri lakini wakati mwingine Mungu huwa anaruhusu kwa ajili ya kusudi lake alilonalo kwako mbele ya safari, na hasa katika kukudhihirishia wewe na wengine uweza wake.Mungu alitaka kujidhihirisha kwa wana wa Izraeli
Ni rahisi sana kufikiri kuwa Mungu alikuwa hajui kuwa Mbele yao kuna Bahari ya shamu, wakaendelea tu kwenda pia kumbuka yeye ndie alikuwa anawaongoza lakini utajiuliza kwa nini Bado aliwaacha waende kwenye bahari ya shamu lengo lake lilikuwa ni kwenda kujidhihirisha kwao na wengi wetu tunafahamu kabisa kuwa Mungu alikwenda na kuigawanya bahari, kitu ambacho hakuna mtu mwenye akili za kibinadamu angefikiri kingeweza kutokea lakini baada ya kutendewa muujiza huu walimuamini Mungu kwa kiwango cha juu sana na kuwa na hakika kuwa hakuna lisilowezekana kwake, hivyo basi wakati mwingine Mungu huwa anataka ufike mahali pa kumuamini kwa kiwango cha tofauti ili usimuonee mashaka tena.
Wakati mwingine magumu hutokea ili ufike mahali Mungu alikotaka ufike .Si wengi sana huwa wanaamini kuwa wakati mwingine Mungu huwa anaruhusu jambo fulani litokee ili yeye afike pale Mungu alipomkusudia, ni wazi kabisa kuwa unaweza kukutana na kashikashi nyingi sana za kimaisha na mambo ya kukuvunja Moyo lakini ikawa ndio njia yako ya kuyaendea mafanikio yako, wakati mwingine inaweza ikawa ni kwa maumivu na machozi lakini ikawa ndio muujiza wako.Ukifuatilia vizuri kwenye Biblia utamkuta kijana Yusufu ambaye Mungu alimkusudia kwenda kuwa mtawala kule Misri ili afike Misri na kuwa waziri mkuu kama Bwana alivyomkusudia ilimbidi kwanza achukiwe na ndugu zake,maana kama wasingelimchukia wasingelimtupa shimoni na baadae kumuuza, maana kule kumuuza ndiko kulikokuwa kunalitimiza kusudi la Mungu kwa ajili ya yeye kwenda Misri, japo yeye pamoja na nduguze wote walikuwa hawajui kitu ambacho Mungu alikuwa anafanya. Ukisoma Mwanzo 39 mstari wa kwanza anaanza kukuonyesha maisha ya Yusufu baada ya kufika Misri kama mtumwa.Ukifuatilia kwa namna ya kawaida inawezekana lazima Yusufu alilia sana,aliumia, na pia kujeruhika kwa kuwa nduguzake walimchukia kiasi cha kumuuza, lakini kama hayo yasingelitokea kusudi la Mungu lisingelitimia,
Na pia tunaona wazi kuwa alipofika Misri si kuwa mambo yake ndio yalikuwa shwari moja kwa moja, isipokuwa ndio akasingiziwa kuwa alitaka kubaka na kutiwa gerezani sasa kwa wale wanaofuatilia Biblia watagundua wazi kuwa ulikuwa ni mpango wa Mungu kwa Yusufu kwenda gerezani ili atokee gerezani kwenda kwa mfalme{ikulu} na ndipo litimie lile Mungu alilolikusudia kwa yeye kuwa waziri mkuu, hili ni jambo la kukutia moyo sana maana inawezekana kabisa unapitia mambo magumu kumbuka utakaposhinda ndipo utakapogundua kuwa Mungu alikuwa na makusudi kwa wewe kuyapitia hayo. Ili kufika pale alipopakusudia kwa ajili ya maisha yako.
Nakumbuka jinsi ambavyo kaka mmoja alinipa ushuhuda baada ya kusoma moja ya vitabu nilivyo andika na hiki kilikuwa na kichwa SABABU 12 ZA WATU KUKATA TAMAA, KUJERUHIKA, KUVUNJIKA MOYO, NA KUPOTEZA MATUMAINI.Alisema nilikuwa nimemuomba Mungu kwa ajili ya kwenda chuo na hatimae nikapata chuo kilichoko Dar es salaamu,lakini Ada yake ilikuwa ni kubwa maana nilitakiwa kujilipia mwenyewe, nikaendelea kujiandaa kuelekea huko, huku nikiendelea kumuomba Mungu anisaidie kujua kama hapo ndipo mahali hasa nilipotakiwa kwenda, na siku ya kuripoti ilipofika nilikuwa tayari nina pesa taslim zaidi ya laki tatu mkononi kwa ajili tu ya kuripoti, anasema nilipofika Dar tayari kwa kuripoti mara nikaibiwa pesa yote na matumaini yangu ya kusoma yakaishia pale, maana sikujua nitapata wapi pesa nyingine na mda ndio unapita siwezi tena kuja kwenye hicho chuo,ikanibidi nirudi kwetu Dodoma nikiwa na uchungu mwingi Rohoni kwa sababu nimeibiwa pesa ambayo ndio niliitegemea, na chuo pia nikawa nimekikosa.Anasema alikuwa katika hali mbaya sana akiwa katika hali hiyo akaendelea kumuomba Mungu pasipo kukata tamaa, ndipo baada ya miezi kadhaa kupita akapata nafasi ya kwenda kwenye mkoa Fulani ambako alienda tu kutembea na kupumzika baada ya yaliyomkuta kutokea anasema nikakuta chuo wanachofundisha mambo ambayo hasa ndio niliyokuwa nikiyataka na Ada yake ni kama Robo ya ile niliyotakiwa kulipa kule Dar es salaam pia nikawakuta watu niliowahi kusoma nao kwenye chuo changu cha awali,anasema nilifurahi sana kwani nikaona pale hasa ndipo Mungu aliponikusudia yaani ninaamani na ninaziona ndoto zangu zikitimia.Ushuhuda huu ni kwa ajili ya kutusaidia kujua kuwa wakati mwingine mambo yako yanaweza yakakwama tu kwa sababu njia uliyoipitia sio uliyotakiwa kuipita au njia unayotaka kupita si sahihi sasa ili urudi kwenye mstari huwa ni lazima ulipe gharama.
Na mfano mwingine ni huu, kuwa vijana wengi leo wanao chumbia au kuchumbiwa na watu ambao sio wale Mungu alio wakusudia kwenye maisha yao. Huwa wanapata shida sana Mungu anapokuwa kazini kuwatoa huko ambako sio sahihi wao kuwa au kuelekea , kumbuka neno lake limehaidi utafundishwa na utaongozwa mahali ambaoko ni sahihi Zab 32:8 Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea;nitakushauri,jicho langu likikutazama" Maana kama Mungu ameona unaelekea kwenye,majuto, kukosa amani,kwenye vilio, kwenye kuacha wokovu, au kufa kwa huduma yako mara nyingi huwa anaruhusu mazingira ya kukukatisha tamaa kabisa juu ya mpango huo,ili baada ya hapo akupitishe kwenye mpango wake ulio sahihi, sasa kwako inaweza ikaja kama mapito au jaribu jitie Moyo kwa Bwana ukiamini kuwa Mungu anao mpango kamili juu ya maisha yako.Maana kama unamtegemea Mungu huwa hawezi akaruhusu mabaya yatokee kwenye maisha yako, sasa mfano huyu Dada hakutakiwa kuwa na huyu kaka aliyenae anaweza tu kushitukia ameachwa , au Mungu anaweza akatumia watu kukushauri, maana neno lake limesema atakushauri, pia jambo lolote laweza kutokea tu mradi msiwe pamoja, nirahisi sana kuumia maana tayari ulikuwa umempa nafasi ndani ya moyo wako,kulia,kujeruhika, hata kuona una bahati mbaya, na kuona Mungu amekuacha na hali Mungu anasema sitakuacha wala sitakupungukia ni wachache sana ambao huwa wanaangalia na upande ule wa pili kuwa inawezekana Mungu ameniepusha na jambo baya au inawezekana huyu hakutakiwa kuwa nami kwenye maisha, wengi huwa wakuja kuelewa baadae sana baada ya kukutana na mtu amabae Mungu alikuwa hasa ndio amemkusudia kwenye maisha yake, mtu atakae inua huduma yake,atakae saidia familia yake, na atakae mfanya aishi maisha ya amani na furaha.
Wakati mwingine majaribu ni kwa ajili ya kuufanya uhusiano wako na Mungu uendelee kukua siku hadi siku au ubadilike kabisa. Ni muhimu sana ndugu msomaji ukafahamu hili, kuwa kila unaposhinda vikwazo na majaribu uhusiano wako na Mungu huwa unakuwa, maana Mungu anaporuhusu jaribu kwako huwa kunakitu anataka kuona kwenye maisha yako na wakati mwingine si tu kuwa Mungu anaruhusu majaribu na kuyazuia isipokuwa kuna wakati yeye mwenyewe anaweza akakujaribu ukisoma Mwanzo 22:1 anasema "Ikawa baada ya mambo hayo Mungu alimjaribu Ibrahimu,,,,,,,,,"nilichotaka hapa uone ni kuwa Mungu alimjaribu Ibrahimu na wala si shetani, hivyo basi si kila jaribu ni shetani, Mungu alimjaribu Ibrahim kwa kumtaka amtoe Isaka, kumbuka halikuwa ni jaribu la kawaida kama unavyoweza kufikiri kwa haraka haraka, uelewe wazi Isaka ndie aliyetakiwa kuwa mrithi, na wakati huo Ismaili alikuwa amesha ondoka, na Ibrahimu amehaidiwa uzao kama nyota za Mbinguni hakikuwa kitu cha kueleweka kabisa maana huo uzao unatokea wapi ikiwa Isaka anakufa, sasa ukisoma ule mstari wa 15 unasema, "malaika wa Bwana akamwita Ibrahimu mara ya pili kutoka mbinguni akasema nimeapa kwa nafsi yangu asema Bwana kwa kuwa umetenda neno hili wala ukunizuilia mwanao,mwanao wa pekee,katika kubariki nitakubariki na katika kuzidisha nitakuzidisha uzao wako kama nyota za mbinguni na kama mchanga uliopo pwani;na uzao wako utamiliki mlango wa adui zao ukiusoma ule mstari wa 18 anasema na katika uzao wako maaifa yote a dunia watajibarikia; kwa kuwa umeitii sauti yangu" kitu nilitaka uone ni kuwa, uhusiano wa Mungu na Ibrahimu ulibadilika kabisa baada ya kukubali kwenda kumtoa Isaka, kwa tafsiri nyingine baada ya kulishinda jaribu maana Mungu alikuwa anasubiri aone kama atashinda au la na ndio maana mwishoni akamaliza kwa kusema, kwa kuwa umeitii sauti yangu tungeweza kutafsiri kama kwa kuwa umelishinda jaribu. Akisema kwa kuwa umeitii sauti yangu maana yake ni kuwa kama usinge itii au kama usinge lishinda jaribu haya ninayo kubarikia na kukuahidi yasingelitokea kwako,
Ndio sababu ni muhimu kujitahidi kuhakikisha unashinda Majaribu au mapito unayokutana nayo maana saa hii, huwezi kujua kuna muujiza gani utatokea mara baada ya wewe kulishinda hilo jaribu, ukisoma katika "Ufunuo 2:17 anasema Yeye aliye na sikio, na alisikie neno hili ambalo Roho ayaambia makanisa: Yeye ashindae nitampa baadhi ya ile mana iliyofichwa,nami nitampa jiwe jeupe, na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya asilolijua mtu ila yeye anayelipokea" anasema yeye ashindae nitampa, hii inamaana kuwa si kila mtu isipokuwa ni yeye ashindae tu, sasa ukifuatilia pale chini anasema nitampa jiwe jeupe na juu ya jiwe hilo limeandikwa jina jipya,maana yake ni hii utakaposhinda tegemea jambo jipya kwenye maisha yako.
Wakati mwingine lile unaloliona jaribu linaweza kuwa ni mpango wa Mungu katika kukuepusha na hatari Fulani,Mfano huu utakusaidia, Kaka mmoja aliachwa na mke wake tena kwa hila kabisa, na yule Dada akasema hamtaki na hampendi kabisa yule kaka. Wanandugu wakajaribu kuingilia kati ikashindikana kabisa yule Dada aligoma kabisa kurudiana na huyu kaka na hali alikuwa ni mume wake, kitu kilichofanya watu waanze kutafuta kujua ni kosa gani kubwa hasa alilolifanya huyu kaka, lakini wakimuuliza huyu kaka anasema anashangaa hata yeye aelewi na walikuwa wamezaa watoto wawili tu, siku moja huyu Dada akamwambia rafiki yake wa karibu sana{kwa tafsiri ya leo tunaweza sema msiri wake} akasema hivi si kwamba simpendi Mme wangu isipokuwa nilitembea nje ya ndoa, Mume wangu alipokuwa masomoni hivyo nimeathirika na sipo tayari yeye ajue na wala sitaki kumuambukiza ukimwi,maana ni nani atalea watoto wangu nikifa na endapo na yeye atakuwa ambukizwa, niliposikia ushuhuda huu nilishangaa sana. Sasa kwa upande wa huyu kaka inakuwa ni huzuni na kuona ameachwa pia kuona Mungu hamuoni kuona amedharaulika kumbe Mungu aonae sirini anamuepusha na Hatari ya kuambukizwa virusi viliyokuwa vinakuja mbele yake, japo haina maana kila anayepitia haya iko namna hii, kwanza Biblia imekataa kuachana, nilitaka tu ujue kuwa wakati mwingine Mungu anakuwa anakuepusha na jambo Fulani baya zaidi, mara nyingi inakuwa si rahisi kwa wakati huu kuelewa ila ukimtumaini Bwana kwa Moyo wako wote hata hali ingeonekana kuwa mbaya kwa kiwango gani Biblia imesema tumaini la mwenye haki halitabatilika. Pia ukisoma Isaya 60:2 anasema "Maana tazama giza litaifunika dunia, na giza kuu litazifunika kabila za watu; bali Bwana atakuzukia wewe na utukufu wake utaonekana juu yako." Hivyo basi inawezekana kabisa mambo yote yakaonekana kuwa ni giza tupu kwako maana mambo unayokutana nayo hujawahi kuyategemea, kumbuka utukufu wa Bwana utaenda kuonekana juu yako endapo utaendelea kumtegemea na kumuamini hata katika hali hiyo unayokutana nayo sasa.
Nimekuwa nikijiuliza maswali mengi sana huku nikindelea kumuomba Mungu baada ya kufanya ushauri na baadhi ya watu ambao wao waliniambia walimuacha Yesu kwa sababu walikutana na majaribu mazito,na wengine wameacha huduma walizokuwa wakifanya kwa sababu ya majaribu na magumu wanayopitia wengine waliniambia wameanguka kwenye uzinzi baada ya majaribu makali, wengine hunijulisha jinsi ambavyo wapo katika hali ya kukata tamaa hivyo wanahitaji maombi ndipo Mungu alipoendelea kunifundisha hili somo.
Hii ni moja ya mifano ya watu wanao pita kwenye majaribu na hali za kukatisha tamaa
Wapo wanawake ambao walipokuwa wanajifungua kwa mara ya kwanza watoto walikufa na kwa sababu ya matatizo yaliyotokea wakafungiwa uzazi,maana yake hawawezi kuzaa tena, sasa ebu fikria jinsi ambavyo tayari yeye na mume wake walikuwa na matumaini na mipango mingi juu ya watoto wao ambao Bwana angewapa gafla unaambiwa mtoto amekufa na kizazi kimefungwa,hili si jambo rahisi hata kidogo, nakumbuka Dada mmoja alinijulisha jinsi ambavyo alipata BP akiwa ni mjazito na baadae mtoto akafa tumboni akafungiwa uzazi.Anasema alichanganyikiwa,na anatamani sana kuzaa lakini aliambiwa na Daktari kuwa akizaa tena atakufa .Kumbuka "yaliyoshindikana kwa mwanadamu kwa Mungu yanawezekana." ushuhuda huu utakusaidia nilikuwa naongea na rafiki yangu ambae ni Daktari aliniambia jinsi ambavyo inakuwa haiwezekani kabisa wao kuamini kuwa baada ya kumfunga mtu kizazi anaweza akajifungua tena sasa anasema siku moja alishangaa kuona mama aliyemfunga tumbo la uzazi ni mjamzito na kuwa aliombewa, anasema wakati wa kujifungua walimfanyia operation na kukuta mtoto amekaa nje ya utaratibu wa kibaolojia nina maana nje ya tumbo la uzazi ila amejishikiza mahali ambapo anapata mahitaji yote muhimu kutoka kwa mama, alivyosema yeye ni kuwa kuanzia hapo alianza kuamini kuwa Mungu anaweza kufanya maajabu na alinielekeza kuwa zamani alikuwa hawezi kabisa kuamini kitu kama hicho kwa jinsi walivyo somea hayo mambo, kumbuka Yeremia 32:27 inasema "Tazama,mimi ni Bwana,Mungu wa wote wenye mwili;je kuna neno gumu lolote nisiloliweza?" Anaposema yeye ni Mungu wa wote wenye mwili maana yake ni kuwa yuko juu ya wote wenye mwili,wasomi, wanasayansi na madaktari na watu wanaofanya mambo makubwa leo Duniani,wote hawa ni kuwa wanakijisehemu tu cha maharifa aliyowapa, hebu jiulize hili swali kama Yesu alizaliwa kama mwanadamu si angetakiwa kufuata taratibu zote za kibinadamu lakini Biblia inasema mimba ilikuwa ni kwa uweza wa roho mtakatifu maana yake ni kuwa utaratibu wa kisayansi na kibaiologia haukufuatwa lakini hii haikusababisha yeye asizaliwe kwa sababu Mungu ni mungu wa wote wenye mwili na njia zake si njia zetu, watumishi wakilitambua hili hawataona shida kuwaombea watu wenye kansa, wenye ukimwi na matatizo ya uzazi, kwa sababu aponyae si wao ila ni Mungu ambae hakuna neno gumu kwake lisilowezekana, pia wanaomuamini Mungu wakilitambua hili hawataacha kuendelea kumuamini na kumtegemea yeye peke yake.na kukaa mkao wa kusubiria miujiza yao.
Wapo watu ambao walitegemea mambo makubwa sana kabla ya kuolewa au kuoa hawakuwahi kufikiri habari za mapito ya ndoa na magumu ambayo wangeweza kukutana nayo, wengine wao kwa sasa wanatamani kama ingetokea nafasi ya kuoa au kuolewa tena, hii yote ni kutokana na magumu wanayo kutana nayo, nakumbuka Mama mmoja alipokuwa akitushirikisha kwa habari za kumuinua kwenye maombi alitujulisha jinsi ambavyo Mume wake ambae hajaokoka alimvizia kumuua kila siku, na kuwa kila alipotaka kufanya hivyo alimuona., sasa Mume wake amekuwa akishindwa kutimiza azma iyo kwa muda mrefu na hali hii imemfanya huyu mama kuishi kwa mashaka makubwa sana, pia wapo wanawake walio olewa na wanaume wasiomjua Mungu kumbuka huyo ni mme wako na umeshafunga nae pingu za maisha ni kifo tu ndicho kitakachowatenganisha hata kama anakukera vipi, usikate tamaa endelea tu kumuamini Mungu kwa ajili yake. Elewa kuwa njia za Mungu si njia zetu mawazo ya Mungu si mawazo yetu ipo siku Mungu atakutana nae inawezekana unapata tabu na huyo mke, Elewa tu kuwa Mungu ajashindwa, wapo watu wengine inafika mahali anakuambia ameomba mpaka sasa amechoka ni muhimu ukatambua kuwa hakuna haja ya kuchoka, muujiza wako uko njiani unakuja hebu tuone Biblia inasema nini juu ya hilo "Luka 18:1 Akawaambia mfano ya kwamba imewapasa kumuomba Mungu siku zote wala msikate tamaa" Sasa ukifuatilia huu mstari kwenye tafsiri zingine za kiingereza utakuta lile neno {siku zote} limeandikwa {always} maana yake kila wakati hivyo basi muombe Mungu kila wakati juu ya hilo jambo linalokukera maana ujui ni wapi na sa ngapi Mungu atatenda muujiza wako.Nakumbuka tulienda kufanya huduma mkoa fulani, hivi karibuni sasa tulikuwa na mwenzetu mmoja ambae ana kaka yake na familia wamekuwa wakimuombea sana amjue Mungu hakikutokea kitu mpaka wakafika mahari wakasahau kwa Kiswahili kingine wakachoka au wakamuachia Mungu kama wengi leo wanavyopenda kusema, wakifika mahali wamekata tamaa, sasa tukiwa kwenye huo mkoa yule kaka yake alihudhuria kipindi cha usiku ambacho tulikuwa tukiwafundisha watu waliokoka namna ya kusimama kwenye wokovu, tena nakumbuka tuliwafundisha kwa njia ya kuonyesha mkanda wa video na ukumbuke yule kaka alikuja tu kwa sababu ndugu yake alikuwepo hivyo alikuja kama kumsalimia kwa sababu alijua yupo pale kwenye lile eneo la huduma, kilichotokea ni kuwa ikabidi ajumuike na wengine kuangalia ile filamu maana tulikuwa kwenye huduma, sasa ilipofika saa ya watu ambao hawajaokoka kumpa Yesu maisha wakashangaa kuona yule kaka akinyosha mkono na kumpokea Yesu, yule ndugu yake hakuamini kilichotokea ilibidi atoe ushuhuda kuwa walikatatamaa, hakuna mtu alitegemea angeokoka tena kwenye kipindi cha mafundisho ya waongofu wapya tena alikuja tu kusalimia. Natamani ufahamu kuwa maombi yako sio bure wala machozi yako sio bure muujiza wako uko njiani unakuja japo hatujui ni wapi utatokea na sa ngapi na kwa namna ipi maadamu tu iwe ni kwa utukufu wa Bwana,sasa wapo watu leo ambao wameachishwa kazi kwa hila na hali familia nzima ilikuwa inawategemea kwa hiyo kazi ,wengine wameshitakiwa kwa uongo mpaka wakawekwa magerezani, wapo wanawake ambao baada ya waume zao kufariki wakapokonywa mali zote wamebaki na uchungu moyoni na wana watoto, ni muhimu kufahamu hili siku zote kuwa Mungu amehaidi kuto kukuacha wala kukupungukia endapo utaamua kumuamini na kumtegemea, ukisoma katika Zaburi 37:5 anasema "mkabidhi Bwana njia yako,pia umtumaini nae atafanya" hivyo basi hata kama jambo limekukatisha tamaa vipi usiache kumkabidhi Bwana na si tu kumkabidhi bali pia kuamini kuwa ulicho muomba atafanya ukisoma ule mstari wa 25 utakuta anasema "Nalikuwa kijana nami sasa ni mzee,lakini sijamwona mwenye haki ameachwa,wala mzao wake akiomba chakula,"watu wengi huwa hawajui namna Mungu anavyowathamini na kuwaheshimu hata kama wanapita katika magumu Daudi alipoifahamu siri hii ya ajabu akasema hajaona mwenye haki ameachwa maana yake ni kuwa hata kama ilitaka kuonekana kama ameachwa lakini baadae ikagundulika kumbe Mungu alikuwa amemkusudia jambo,ukishalifahamu hili kule kuamini tu kuwa Mungu atakupigania au Mungu amehaidi kunitetea huwa kunavuta msaada wa Mungu wa kukusaidia na kukuondolea hali ya hofu na mashaka na kukufanya uishi kwa imani na ujasiri.zaidi.
Wapo watu ambao wameachwa na wake zao au waume zao, na wameachiwa watoto na baadae kusikia yule mwanamke au mwanaume anataka kuolewa au kuoa kwingine , maumivu haya huwa yanakuwa ni mabaya sana tena mara nyingi yenye kuambatana na uchungu mkubwa maana si kitu kinachoelezeka kiurahisi hata kidogo, nakumbuka nilipata kumsikia mama ambae baada ya kuolewa na kuzaa watoto kadhaa ile mimba iliyofuata Mme wake akaikataa na kusema hiyo si yake na kuwa huyu mama amezini nje na hivyo basi ameamua kwenda kuoa mke mwingine maana ile haikuwa mimba yake, ni kitu kigumu sana na pia hakielezeki kirahisi sasa huyu mama ameachwa ni mjamzito,alafu amesingiziwa kazini nje,alafu anaambiwa mme wake anataka kuoa amepata na mchumba wa kumuoa, ni lazima tu maumivu yatakuwa ni makali sana moyoni, lakini kumbuka Biblia imeshasema katika Mithali 23:18 kuwa "Maana bila shaka iko thawabu,na tumaini lako halitabatilika." Kibinadamu huwezi kuelewa mambo Fulani yanapo kufika, lakini Biblia ni amina na kweli ikiwa unamuamini Mungu hakuna gumu kwa Mungu na tumaini la mwenye haki haliwezi batilika
BIBLIA INASEMA NINI JUU YA MAJARIBU NA MAGUMU UNAYOKUTANA NAYO
Ni wazi kabisa kuwa watu wengi wanakutana na hali za kuvunja moyo,wengine wamekatishwa tamaa kabisa,na wengine, ni vile tu yale waliyo yategemea yangetokea hayakutokea ,lakini nataka ujue ya kuwa Yesu yu hai leo maana kama asingalifufuka imani yetu ingekuwa ni bule,lakini maadamu alifufuka basi liko tumaini, hivyo basi endelea kuliamini neno lake na kumtumaini Yeye peke yake ukisoma Ufunuo 3:10anasema "kwa kuwa umelishika neno la subira yangu,mimi nami nitakulinda utoke katika saa ya kujaribiwa,,,,,,,,,,,"Maana ya kulishika neno la subira ni kule kuishi katika hali ya kumtumaini Mungu na kuliamini Neno lake {kule kujua neno lake li hai tena lina nguvu,kule kujua kuwa analiangalia hilo neno lake apate kulitimiza, hata kama halijatimizwa kwako bado, maana .inawezekana mazingira yanayo kuzunguka yakawa yanakukatisha tamaa kabisa hivyo basi ile tu kuwa na tumaini kwa Bwana kwa wakati kama huu, kutakufanyia mlango wa wewe kuweza kutoka, sasa ukulifuatilia lile neno "kwa kuwa umelishika neno la subira yangu"tunaweza tukatafsiri kama kwa sababu umelishika neno la subira yangu, hii ina maana kuwa kule kulishika neno la subira yake katika wakati kama huu wa magumu na mambo ya kukatisha tamaa ndiko kunakomfanya yeye akulinde na akusaidie kutoka kwenye wakati mgumu ulio nao,ikiwa ni pamoja na shida zinazo kuzunguka,

ukisoma huu mstari utaelewa vizuri kitu ninachotaka ukipate "Rumi 4:18:-21 Naye aliamini yasiyoweza kutarajiwa ili apate kuwa Baba wa mataifa mengi, ninachotaka ujue ni kuwa suara la Ibrahimu kuwa Baba wa mataifa mengi lilitegemea kule kumuamini Mungu na kulishika neno la subira yake hata kama kibinadamu mambo yalikuwa yanakatisha tama, ili kujua yalikuwa yanakatisha tamaa kivipi ukiendelea mbele kidogo utaona Biblia inasema aliamini yasiyoweza kutarajiwa maana yake ni kuwa aliamini vitu ambavyo hakuna mtu mwenye akili timamu asiyemuamini Mungu angeweza kukubaliana navyo, mstari wa 19 anasema "Yeye asiyekuwa dhaifu wa imani alifikiri hali ya mwili wake uliokuwa umekwisha kufa akiwa amekwisha kupata umri wa kama miaka mia na hali ya kufa tumbo lake sara."Mstari huu unaelezea jinsi ambavyo Ibrahimu alikuwa amezeeka vya kutosha na jinsi ambavyo Sara hata tumbo lake tu lilikuwa limekufa maana yake hawezi tena kupata mtoto kwa namna ya taratibu za kibinadamu, na bado Mungu aliendelea kuwahaidi hata katika wakati huu, kwao lilikuwa ni jaribu zito na hali iliyowakatisha tamaa kabisa kwa sababu walikuwa na mali nyingi ila hazina mrithi,na bado hawaoni kama kuna kitu kinaweza kikafanyika. Nini kiliwasaidia katika wakati kama huu ukisoma ule mstari wa 20 na 21 utakuta anasema "Lakini akiiona ahadi ya Mungu akusita kwa kutokuamini bali alitiwa moyo kwa imani akimtukuza Mungu huku akijua hakika ya kuwa Mungu aweza kufanya yale aliyoahidi kama kilichomsaidia Ibrahimu ni kutosita, kwa tafsiri nyingine ni kutokuwa na mashaka na huku hakujua hakika kuwa Mungu anaweza kufanya yale aliyohaidi,ndugu yangu unayesoma mafundisho haya bila kujalisha unapita katika kipindi cha namna gani liamini neno la Mungu amini ahadi za mungu juu ya maisha yako, Ibrahimu alimtukuza Mungu huku akijua hakika kuwa anaweza kufanya yale aliyohaidi.
NAMNA YA KUITAMBUA MILANGO YA KUTOKEA UWAPO KATIKATI YA MAJARIBU.
Ukisoma katika 1korinto 10:13 anasema, "Jaribu halikuwapata ninyi, isipokuwa lililo kawaida ya wanadamu;ila Mungu ni mwaminifu; ambae hatawaacha mjaribiwe kuliko mwezavyo lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea,ili muweze kustahimili" anaposema jaribu halikuwapata ninyi isipokuwa lililo kawaida ya mwanadamu hii ina maana haijalishi tatizo unalokutana nalo limebeba vitisho vya namna gani,au watu wanasema kwa namna gani, au limekuumiza kwa kiwango kipi, cha msingi tu limekupata wewe basi hilo ni lakiwango chako, ndio hasa maana ya huu mstari unaosema jaribu halikuwapata ninyi isipokuwa lililo kawaida ya mwanadamu, hivyo basi hakuna jaribu linalo ruhusiwa kwako kinyume cha imani yako, na ndio sababu Yesu alipokuwa akiwafundisha wanafunzi wake kusali kipengele kimojawapo kilikuwa ni kumuomba Mungu asitutie majaribuni na kama kipengere hiki kilikuwa ni sehemu ya sala,hii ina maana majaribu sio mazuri, sasa basi mpaka jaribu likatokea kwako au likaruhusiwa kwako hii ni lazima kunasababu.hivyo basi kaa mkao wa kuona Mungu akikushindia na tamani kuona matokeo ya ushindi wako. Na majaribu siku zote ni sawa na mtihani na lengo la mtiani ni kukuvusha darasa hivyo basi jaribu lengo lake ni kukutoa kwenye kiwango Fulani cha imani na kukupeleka kwenye kiwango kingine, na ndio sababu Biblia ikasema tunatoka tunatoka utakatifu hadi utakatifu, pia tunatoka imani hadi imani na pia ni muhimu ukafahamu kuwa lengo la jaribu sio kukuangusha wewe,wala sio kukukatisha tamaa isipokuwa ni kuimalisha imani yako utakapokuwa umeshinda, hebu kwanza tuangalie huu mstari vizuri, anaposema "Lakini pamoja na lile jaribu atafanya na mlango wa kutokea ili muweze kustaimili" ninachotaka uone hapa ni kuwa pamoja na kwamba kila jaribu litakalo kuja kwako ni la kiwango chako bado Mungu amehaidi kufanya mlango kwa ajili ya wewe kustaimiliSasa ikiwa Mungu alihaidi kufanya mlango ili watu waweze kustaimili na bado watu wameanguka kwenye majaribu, hii haina maana majaribu yalikuwa mazito sana isipokuwa watu hawakuitambua milango ya kutokea maana yeye si mwongo alishasema atafanya mlango wa kutokea ili waweze kustaimili sasa kama amefanya mlango na mtu hakutoka basi inawezekana mtu hajatambua mlango au hakuchukua hatua ya kutoka.

Nini maana ya kutokuitambua milango ya kutokea
Wapo watu ambao katikati ya mapito na mambo magumu anayo kutana nayo anajisemea maneno ya laana, anaruhusu hali ya uchungu moyoni na si kwamba hajui anachokifanya ila ameamua tu kufanya hivyo {mara nyingi mwisho wake huwa unakuwa ni kuanguka} kwa sababu unaporuhusu maneno ya kukuvunja moyo tena unayo jitamkia mwenyewe kuna kitu kibaya kinachoumbika katika ulimwengu wa Roho {Mith 10:11}anasema "kinywa chake mwenye haki ni chemchem ya uzima bari jeuri hufunika kinywa chake mtu mpumbavu" sasa neno la Mungu limesema kinywa chako wewe mwenye haki bila kujalisha uko kwenye kipindi gani kinajulikana kama chenye chemchemu ya uzima, na sio laana japo kinao uwezo wa kutengeneza laana,Huu si wakati wa kujisemea mabaya ni wakati wa kusema najua bwana atanisaidia,najua ni kwa muda tu,Mungu ataniinua, Muujiza wangu unakuja,Bwana atafanya njia hiki ni kipindi cha kujitia Moyo Mwenyewe na usisubiri mtu mwingine,maana anaweza asitokee, maana haya maneno unayojitamkia yananafasi ya kujenga kitu au kubomoa kitu katika ulimwengu wa Roho Mithali 12:14 "Mtu atashiba mema kwa matunda ya kinywa chake na atarudishiwa matendo ya mikono yake" ikiwa hivyo ndivyo ilivyo kuwa muangalifu sana maana maneno yako na mawazo yako vinanafasi kubwa sana ya kuondoa uchungu uliotokea ndani yako. Maana kule kuendelea kuruhusu hali ya uchungu kutakuletea kukata tamaa na hatimae kumuacha Yesu na kuanguka dhambini.

MAMBO YA KUZINGATIA UWAPO KATIKATI YA MAJARIBU NA MAMBO MAGUMU
Huu si wakati wa kukaa na watu wanao kuvunja moyo na kukupandikiza roho za uasi ikiwa ni pamoja na kukata tamaa, wakikunenea maneno magumu maana wapo watu wanao ruhusu mazingira ya namna hii hata ikiwa wamejua madhara yake. {Na mara nyingi mwisho wake huwa unakuwa ni kurudi nyuma au kuanguka}ukisoma katika Mithali 12:5-6 anasema "mawazo ya mwenye haki ni adili,bali mashauri ya mtu mwovu ni hadaa", hivyo basi hiki ni kipindi cha kuwa muangalifu sana na watu wanao kushauri, sasa ukiendelea ule mstari wa sita utakuta anasema "Maneno ya waovu huotea damu,bali kinywa cha wanyofu kitawaokoa" anaposema kinywa cha wanyofu kitawaokoa hii ina maana kuwa unahitaji watu ambao ndani yao hamna hila, ili kukutia moyo maana pia ndani yao huwa kunakuwa na matumaini, na hivyo basi imani yako juu ya msaada wa Mungu kukusaidia inakuwa kubwa kabisa bila kujalisha ni magumu ya aina gani uanayo kutana nayo .
Huu si wakati wa kuwaza kulipiza kiasasi juu ya mtu aliye kutendea ubaya maana kuna watu huwa wanapita katika kipindi Fulani cha ugumu tu kwa sababu kuna mtu amemfanyia ubaya, pamoja na hayo kumbuka huu ni wakati wa kujitahidi kusamaehe,kuachilia nafsi yako maana kisasi ni juu ya Bwana ukisoma katika 2timotheo utaona Paulo akimwambia Thimotheo jinsi amabavyo Iskanda alimfanya apite katika kipindi kigumu sana maana alikuwa akimpinga sasa ukiendelea anaishia kusema Bwana atamlipa, maana anajua hatakiwi kulipiza kisasi 2Timotheo 4:14 anasema "Iskanda mfua shaba,alionyesha ubaya mwingi kwangu Bwana atamlipa sawasawa na matendo yake nawe ujihadhari na huyo,kwa sababu aliyapinga sana maneno yetu".
Huu si wakati wakumuelezea kila mtu yaliyotokea kwenye maisha yako, maana kuna wakati mwingine atavunjwa moyo kabisa na mtu uliyetegemea labda ndie angekutia Moyo pia hata kukusaidia kwa maombi kwa wakati kama huu, hivyo basi muombe Mungu akusaidie kujua ni yupi hasa atakuwa tayari kuubeba mzigo wako kwa wakati kama huu, ukisoma katika Isaya 35:3 utakuta anasema "Itieni nguvu mikono iliyo dhaifu,yafanyeni imara magoti yaliyolegea,Waambieni walio na hofu, "jipeni moyo msiogope? Unahitaji watu wa namna hii hasa upitapo katika magumu watakao kusaidia kuvuka, watakao kuambia jipe moyo na hatimae kutoka salama.
Huu si wakati wa kupokea kila ushauri maana unapokuwa unapita katika gumu Fulani ni rahisi sana kutaka kulitendea kazi kila unalolisikia,maana unafikiri ndani ya kila unalolisikia kuna uponyaji unaweza kupatikana, na wengine kipindi kama hiki huwa tayari kuombewa kila mahali au popote hata akiambiwa kuna mganga anaombea watu kwa kuagua yuko tayari kwenda bila kuhoji, kumbuka magumu ni kwa kitambo kifupi tu yasikufanye ukaharibu maisha yako na kumkosea Mungu kabisa, ukisoma Zab 23:4 anasema ,"nijapopita kati ya bonde la uvuli wa mauti sintaogopa mabaya;kwa maana wewe upo pamoja nami gongo lako na fimbo yako vyanifariji." Ni muhimu ukafahamu kuwa mfalme Daudi ni mmoja wa watumishi wa Mungu waliopitia kipindi kigumu sasa aliposema nijapopita alikuwa anamaana ya kujitia moyo kuwa sintakaa kwenye haya magumu siku zote isipokuwa ninapita tu,ndio maana akasema nijapopita sio nijapokaa,amini tu kuwa unapita,na ni kwa muda tu,
Huu si wakati wa kutumia muda mwingi sana kukifikiria kilicho tokea na jinsi kilivyo kuumiza maana utaishia tu kuwa na uchungu moyoni hata kupata vidonda vya tumbo na hata kumkosea Mungu, ipo mithali inasema yaliyopita si ndwele tugange yajayo,inawezekana yaliyotokea yamekuhaibisha,yamekutia aibu,yamekushusha hadhi, yamekuondolea heshima kwenye familia au jamii inayokuzunguka, bila kujalisha ilitokeaje cha msingi yameshatokea, wewe msii tu Mungu afanye kitu kipya kwako na si kulia tu huku ukiwa kwenye mawazo muda wote.baada ya Paulo kuamua kuyasahau yaliyo pita,kujikubali nafsi maana aliyafanya mambo mengi ya aibu kabla ya kumjua kristo,pale tu alipoamua kuutafuta uso wa Mungu kwa bidii baada ya kuamua kuyasahau yaliyo pita, Mungu alikuwa akijidhiirisha kwake siku hadi siku. Ukisoma Filipi 3:13 anasema Ndugu,sijidhanii nafsi yangu kwamba nimekwisha kushika;ila natenda neno moja tu;nikisahau yaliyo nyuma,nikiyachuchumilia yaliyo mbele nakaza mwendo,niifikilie mbele ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika kristo Yesu." Sasa basi kule kujitahidi kuyasahau yaliyopita kutakusaidia kukaza Mwendo na kujipanga upya kwa ajili ya yale yaliyo mbele yako.
Huu si wakati wa kuanza kujaribisha imani zingine, kama hujawahi tumia Dawa za kienyeji kwa sababu unaamini ni machukizo mbele za Bwana au kutambika kwa kutoa sadaka kwenye makaburi ya mababu kwa nini ufanye hivyo tu kwa sababu ya gumu Fulani tena linalopita tu? Muamini Mungu maana yote yawezekana kwake yeye aaminie kumbuka "ukiwa muaminifu kwa madogo Mungu atakufanya kuwa muaminifu na kwa makubwa pia".
Huu ni wakati wa kukaa kwenye maombi, nakumbuka Bwana Yesu alikuwa ni muombaji lakini pia baada ya kutambua kuwa anakiendea kipindi kigumu, muda mwingi aliendelea kukaa kwenye maombi zaidi na Mungu alikuwa akimtia nguvu ukisoma "Luka 22:40 anasema, "Alipofika mahali pale akawaambia "Ombeni kwamba msiingie majaribuni." Mwenyewe akajitenga nao kiasi cha kutupa jiwe,akapiga magoti akaomba akasema "Ee Baba, ikiwa ni mapenzi yako,uniondolee kikombe hiki;walakini si mapenzi yangu bali yako yatendeke." ninachotakaka uone ni kuwa alikuwa anapita katika jambo gumu sana tena la mauti ya msalaba hivyo alifika mahali pa kujihurumia nafsi yake, lakini kule kukaa kwenye maombi kwa wakati kama huu kulikuwa ni kwa muhimu sana ukisoma ule mstari wa 43 anasema "Malaika toka mbinguni akamtokea akamtia nguvu" hivyo tunaona malaika wa Bwana alimkuta Yesu kwenye maombi, pia kwa wasomaji wa biblia utakumbuka siku nyingine walikuja Musa na Elia lengo lilikuwa ni moja tu kumtia moyo BwanaYesu lakini walimkuta akiwa kwenye maombi,hivyo basi maombi huuisha, hitia nguvu, pia humtengenezea Mungu mazingira ya kujifunua kwako hata katika hilo unalolipitia wewe.
Huu si wakati wa kujilaani, kujikataa, na hata kufikiria ni bora ungekufa, ni muhimu kufahamu kuwa wewe ni wathamani sana mbele za Mungu bila kujalisha nini kimetokea kwenye maisha yako,anza kujinenea maneno yenye baraka,ushindi,mafanikio,uzima,huku ukimuamini Mungu.
Huu ni wakati wa kutafuta kujua ni mianya ipi ambayo ilimpa Adui nafasi kwenye maisha yako, na kujitahidi kutokumpa tena nafasi kwenye maisha yako huku ukilisoma neno la Mungu, na kukaa kwenye maombi ukijiepusha kabisa na mazingira yoyote yanayoweza kusababisha maumivu na uchungu moyoni.
Huu ni wakati wa kujifunza kujisamehe, Pamoja na kukubaliana na hali iliyotokea kuwa imeishatokea, kwa lengo la kuweka mikakati mipya ya maisha na si kuishia kujilaumu na kulia tu, kitu ambacho hakisaidii isipokuwa kuendelea kukutengenezea uchungu na majeraha moyoni.
Huu ni wakati wa kubadilisha mfumo wa mawazo usiendelee kukubaliana na mawazo ya kukukatisha tamaa wala kurudisha nyuma pia yale yanayokutaka ufanye kosa la pili maana wapo mabinti ambao baada ya kugundulika ana Mimba huamua kuitoa,kumbuka ni machukizo kwa Bwana maana wapo watu wanaomtafuta huyo mtoto usiku na mchana kubaliana na hali iliyotokea Rudi mbele za Mungu kwa toba, kasha anza kufikiri kwa habari ya maisha mapya na umuombe mungu akusaidie bila kujalisha jamii inakuchukuliaje maana kama umefanya kosa la kwanza ukaamua kufanya na lile la pili ni muhimu kufahamu kuwa unachokipanda utakivuna.maana Mungu adhihakiwi.
Huu ni wakati wa kujifunza kutokana na yaliyotokea, huku ukifanya tathimini kujua nini lilikuwa tatizo,au chanzo cha hilo jambo kilikuwa ni kitu gani, nani alihusika zaidi, na je yaliyofanyika yalikuwa ni mapenzi ya Mungu au la, ni Ni nini hasa neno la Mungu linasema kuhusu hilo jambo,ukishapata nafasi ya kutathmini kilichotokea ndipo sasa unaweza ukapata kitu cha kujifunza, au kuomba toba Mbele za Mungu na kufanya maamuzi yenye busara
Huu ni wakati wa kuijenga nafsi yako kwa neno la Mungu anza kujitahidi kujaza Moyo
wako neno la Mungu, Bwana Yesu siku moja alitoa sababu ya watu kupotea au kukosea kuwa ni kwa kutokulijua neno la Mungu, na hauwezi kulijua neno la mungu ikiwa haulisomi Mathayo 22:29 inasema "Yesu akajibu akawaambia "mwapotea"kwa kuwa hamyajui maandiko wala uweza wa Mungu" sasa ukisoma ile tafsiri ya kiingereza utakuta anasema your mistaken not knowing the scriptures tafsili ya moja kwa moja ya Kiswahili ni kuwa mnafanya makosa kwa sababu ya kutojua maandiko pia neno la Mungu limesisitizwa kujaa kwa wingi ndani yako kule kuendelea kulishika neno la Mungu na kulijaza kwenye nafsi yako ni kwa muhimu sana hasa kwa wakati kama huu.





MAMBO YA KUZINGATIA UNAPOKUWA UMEZUNGUKWA NA MAMBO YA KUKATISHA TAMAA
Endelea kumuamini, kumtii na kumtegemea Mungu peke yake hata uwapo katika hali ya kukatisha tamaa. Mke wa ayubu aliona ni bora Ayubu akufuru afe ili yale mateso yaishe,hii ina maana Ayubu alikuwa katika hali ya kukatisha tamaa kabisa, lakini bado aliendelea kumtegemea na kumtumaini Mungu peke yake pia ukisoma Luka 18:7anasema "na Mungu, je, hatawapatia haki wateule wake wanao mlilia mchana na usiku,nae ni mvumilivu kwao,nawaambia atawapatia haki upesi;" amini maombi yako na machozi yako mbele za Mungu sio bure na kuwa Mungu amehaidi kukupatia haki upesi endapo utamtumaini na kumtegemea yeye peke yakeJapo pia inawezekana ukawa umetishiwa mambo mabaya, wanataka kukudhulmu,kukuua, unakaliwa vikao vya hila, neno linasema katika Zaburi 125 :2 "kama milima inavyozunguka yerusalemu,ndivyo bwana anavyozunguka watu wake,tangu sasa na hata milele" ukiufuatilia ule mstari wa 3a utakuta anasema "kwa maana fimbo ya udhalimu haita kaa juu ya fungu la mwenye haki" na endapo wakawa wamekudhurumu mali umesingiziwa, mambo ambayo hujayafanya Biblia inasema Math 5:11 "Heri ninyi watakapowashutumu na kuwaudhi na kuwanenea kila neno baya kwa uongo,kwa ajili yangu. Furahini, na kushangilia,kwa kuwa thawabu yenu ni kubwa mbinguni hii isiwe kwa ajili ya kukuvunja moyo bali iwe ni gia ya kukufanya usonge mbele.
Usiache kukaa kwenye maombi uwapo katika wakati huu Biblia inasema katika "Filipi 4:6 Msijisumbue kwa neno lolote bali katika kila neno kwa kusali na kuomba,pamoja na kushukuru,haja zenu na zijulikane na Mungu"hiki ni kipindi cha kukaa kwenye uwepo wa Mungu sana maana wengi walimuacha Yesu tu kwa sababu ya uchungu na Magumu waliyowahi kukutana nayo kumbuka hujaanza wewe wengi walipita katika hayo na Mungu akawashindia..Neno la Mungu linasema katika Math 7:7 "Ombeni nanyi mtapewa;tafuteni nanyi mtaona; bisheni nanyi mtafunguliwa; kwa maana kila aombae hupokea naye atafutae huona;nae abishae atafunguliwa" ndugu msomaji endelea kuomba bila kuchoka maana neno la Mungu linasema kila aombae hupokea amini ipo siku utapokea muujiza wako, tena Bwana Yesu akitaka kusisitiza kuhusika kwake katika mambo yako akasema kwenye ule mstari wa 9 Au kuna mtu yupi kwenu, ambae mwanawe akimuomba mkate atampa jiwe au akimuomba samaki atampa nyoka? Basi ikiwa ninyi mlio waovu,mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema,je si zaidi sana Baba yenu aliye mbinguni atawapa mema wao wamuombao" Lakini pia BwanaYesu akijua kuna watu watakata tamaa kabla ya kupokea miujiza yao akawaambia mfano ukisoma Luka 18:1 anasema "Akawaambia mfano ya kwamba imewapasa kumuomba Mungu siku zote,wala msikate tamaa Yesu alijua kuna watu watakata tamaa upesi ikabidi atoe na mifano mstari wa 2 akaendelea kusema "palikwa na kadhi katika mji Fulani,hamchi Mungu, wala hajali watu na katika mji huo palikuwa na mwanamke mjane,aliyekuwa akimuendea endea,akisema,nipatie haki na adui wangu nae kwa muda alikataa;alafu akasema moyoni mwake,Ijapokuwa simchi Mungu wala sijali watu lakini kwa kuwa mjane huyu ananiudhi nitampatia haki yake asije akanichosha kwa kunijia daima."’sasa ukiendele mstari wa sita unaona msisitizo wa jambo baada ya mfano "Bwana akasema, Sikilizeni asemavyo yule kadhi dhalimu.Na Mungu je hatawapatia haki yake wateule wake wanao mlilia mchana na usiku,naye ni mvumilivu kwao nawaambia atawapatia haki upesi kwa tafsiri nyingine ni kuwa kama tu yule kadhi asiejali mtu wala Mungu bado alifika mahali akaona huyu Mama anamsumbua kiasi ambacho ni bora tu ampatie hitaji lake Si zaidi Mungu wa mbinguni na wewe ukiwa kama mtoto wake. Muamini Mungu usikate tamaa atakupatia haki yako upesi.
Jifunze kumtwika yesu fadhaa zako hii ndio ilikuwa sababu ya yeye kufa msalabani, kumbuka alipokuwa pale msalabani alisema imekwisha ukisoma Isaya 53:4a anasema "Hakika ameyachukuwa masikitiko yetu,amejitwika huzuni zetu" hivyo basi hayo masikitiko yako, hizo huzuni zako Yesu alivichukuwa msalabani, ukisoma ule mstari wa 5 anasema "bali alijeruhiwa kwa makosa yetu,alichubuliwa kwa maovu yetu.Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake na kwa kupigwa kwake sisi tumepona."ukisha kuyaona hayo muamini Mungu Lakini pia ukisoma 1petro 5:7 anasema "huku mkimtwika yeye fadhaa zenu zote maana yeye hujishugulisha sana na mambo yenu" maana ya kumtwika yeye fadhaa zako ni kumbebesha mzigo wako,na sio kubaki na mzigo wako Amini Mungu anajishugulisha sana na mambo yako na amini yuko tayari kubeba mateso yako hata kama mazingira yanaonyesha ugumu wa kila namna.
Amini tu kuwa Mungu atatenda Biblia inasema nini juu ya kuamini ukisoma Ebrania 11:6 anasema Basi imani ni kuwa na hakika juu ya mambo yatarajiwayo,ni bayana ya mambo yasiyoonekana. Kama imani ni kuwa na uhakika juu ya mambo yatarajiwayo hii inamaana hayapo, wala hayaonekani, ila unayategemea, na anaposema ni bayana ya mambo yasiyoonekana maana yake, ni ukweli juu ya kitu ambacho hakipo wala hakionekani kwa macho pia kinaweza kisiwe hata na dalili zozote kuwa kinaweza kutokea ila wewe unakiona bayana kwa kutarajia ukiamini,ndio sababu ukisoma Rumi 4:18a anasema "Naye aliamini kwa kutarajia yasiyoweza kutarajiwa" hii Ina maana kuwa, aliyaona bayana mambo ambayo hakuna mtu aliyategemea yangetokea ila yeye aliendelea kuamini huku akiyategemea yatokee anaposema aliamini kwa kutarajia maana yake aliamini kwa kusubiria
Kaa mkao wa kuepuka mabaya huku ukitarajia muujiza wako toka kwa BwanaJambo linalo sababisha watu wengi leo wasipokee miujiza yao kutoka kwa Mungu ni kutokaa mkao wa kutarajia toka kwa Bwana hata kama wamekuwa wakiomba,wengi mnafahamu mnapokua mkimtarajia mgeni Fulani nyumbani kila hodi inayogongwa huwa mnafikilia ni yeye, kwa nini? kwa sababu mnamtarajia mgeni, hebu fikiria huu mfano wa kawaida ndio Askofu wako amesema anakuja nyumbani kwako, jinsi unavyo jiandaa kuweka kila kitu safi tena kila kitu mahali pake,na hata kama kuna ratiba huwa zinaendelea hapo nyumbani siku hiyo inakuwa tofauti kwa nini kwa sababu tu unatarajia mgeni, mfano wa pili ni mama mjamzito anapotarajia kujifungua kuna baadhi ya vitu huwa anakuwa hawezi kufanya kwa sababu anajua akifanya vinaweza kuharibu tarajio lake alilo nalo juu ya ujio wa kiumbe kipya.hivyo basi kaa mkao wa kuona Mungu akikutetea acha kujilaani, na kujikatia tamaa, anza kujiamini huku ukitarajia muujiza wako toka kwa bwana.Sasa basi unapokuwa umepita kwenye magumu huu sio wakati wa kujichafua isipokuwa kujitakasa na kutegemea kumuona Mungu akikusaidia,maana kule kujichafua na kuanza kufanya mambo yasiyompendeza Mungu ndiko kunakoweza kusababisha usipokee muujiza wako toka kwa Mungu, naamini kabisa kuwa mpaka sasa Mungu ameshafanya kitu kukubwa kwenye maisha yako kupitia somo hili, endelea kumuamini na kumtegemea Bwana Yesu siku zote za maisha yako. Mungu na akubariki sana. USIACHE KUTUOMBEA.
Mwl: Tuntufye Andew mwakyembe
Email tumsifu_Andrew@yahoo.com simu 0784 629562 na kwa uhitaji wa maombezi youth_ prayernet@yahoo.com pia C/o S.L.P 55 USA RIVER ARUSHA
ENDAPO UMEGUSWA NA HUDUMA HII NA UNGEPENDA KUPANDA MBEGU KWA KUSAIDIA KULIPIA SEHEMU YA GHARAMA
usisite kuwasiliana nasi.au waweza kutumia account No.016201033820 NBC.MBEYA BRANCH.
Kwa maelezo zaidi tumia Email ifuatayo yagotm28@yahoo.com