Monday, June 9, 2008

PICHA

Mwl.Tuntufye Andrew mwakyembe

KUFUNGULIWA

Mwl.Tuntufye akiwa katika huduma ya kufunguliwa na kuwekwa huru

VITA VYA KIROHO

VITA VYA KIROHO
Efeso 6:12 kupigana kwetu si juu ya damu na nyama bali juu ya falme
Isaya 57:14 kila siraha itakayoinuka juu yako haitafanikiwa
2timoth 2:4 hakuna apigae vita ajitiae katiaka shughuli za dunia 7 Mungu hakutupa roho ya woga bali ya nguvu
Isaya 49:24 je aliye hodari aweza kupokonywa mateka yake?
Luka 10:19 nimewapa amri ya kukanyaga inge na nyoka na nguvu zote za yule adui
Efeso 3:20 kwa kadri ya nguvu itendayo kazi {neno li hai tena lina nguvu}
Ezekieli 22:30 nami nikatafuta mtu miongoni mwao {atakayepigana atakaye fight sikuona}
Zab 91:13 utawakanyaga samba na nyoka, mwanasimba na joka utawaseta chini ya miguu
Mith 24:10 ukizimia siku ya t

Aabu nguvu zako ni kidogo
Ayubu 22:28 nawe utakusudia neno nalo litathibitka kwako
2kor 10:3 ingawa tunaenenda katika mwili hatufanyi vita kwa jinsi ya mwili
1petro 5:8 mshitaki wenu kama samba anazunguka akitafuta mtu ammeze
Yoh 10:10 mwivi haji ila aibe na kuharibu mimi nalikuja ili wawe na uzima kasha wawe nao tele
Yer 11:10 nimekuweka juu ya mataifa na juu ya falme ili kungoa na kuharibu kujenga na kupanda
Yakobo 4:7mpingeni shetani nae atawakimbia
Efeso 4:27 msimpe ibilisi nafasi
Huwezi kuingingi akwa mwenye nguvu pasipo kuviteka vitu vyake

USHINDI DHIDI YA MAPAMBANO TULIYONAYO KATIKA ULIMWENGU WA ROHO
{VITAVYA KIROHO}
Ndugu yangu mpendwa ambaye Mungu kwa neema yake amekupa nafasi ya kufuatilia masomo haya yajulikanayo kama vita vya kiroho ninakusalimu kwa Jina la Yesu. Ni matumaini yangu kuwa Mungu kwa neema yake ameendelea kukutoa hatua kwa hatua, mara ulipoendelea kufuatilia masomo mbalimbali ambayo Roho mtakatifu amekuwa akitufundisha ni matumaini yangu kuwa Mungu kwa neema yake anakwenda kukufungua macho kwa namna nyingine tena utakapokuwa ukifuatilia ujumbe huu.
Ninapozungumza vita ya kiroho ninazungumzia suala la mapambano waliyonayo wateule dhidi ya roho za giza, Biblia inasema “Efeso 6:11 Vaeni silaha zote za Mungu mpate kuweza kuzipinga hila za shetani,” hiki ni kitu muhimu sana mimi na wewe tunahitaji kukifahamu, kuwa maisha yetu yamezungukwa na hila za Adui, kwa masaa 24 kila siku, na Biblia imeweka wazi kabisa kuwa anatushitaki mbele za Mungu mchana na usiku, yaani wewe unapolala yeye alali maana ana kazi ya uharibifu yakufanya kwenye maisha yako “Ufunuo 12:10b kwa maana ametupwa chini mshitaki wa ndugu zetu yeye awashitakie mbele za Mungu mchana na usiku”unapoendelea kusoma sura ya 12:12b Biblia inasema “Ole wa nchi na bahari! Kwa maana yule Ibilisi ameshuka kwenu akijua ana wakati mchahche tu”
Neno Ole maana yake inaweza kuwa onyo/angalizo, analopewa mtu ili aweze kuwa makini sana. Na mala nyingi huwa hili neno linatumika pale ambapo mbele huwa kunakuwa na hatari kubwa inayomkabali endapo hatakuwa muangalifu au endapo hatafuata kanuni fulani.
Na kwa sababu adui anatutafuta usiku na mchana apate kutuangamiza, hii ndio inayotulazimu kuvaa siraha zote za Mungu ili kila wakati tuweze kuzipinga hila za muovu. Kwenye maisha yetu, kwenye masomo yetu, kwenye ndoa zetu, kwa watoto wetu, wachungaji wetu, kwa wazazi wetu, kwenye safari zetu, na kila mahali tunapohitaji kuzipinga.
Ndugu mpendwa ni kitu cha kawaida kabisa kuwa, majumbani mwetu ama maofisini, au kwenye michezo, mahali popote tunapokuwepo, huwa tuanakuwa tumezungukwa na watu wenye misingi ya imani tofauti, tunakuwa tumezungukwa na wapagani, wachawi, wanaotumia na kumiliki Nguvu za giza, na wakati mwingine huwa tunakuwa tuna marafiki, Ndugu au watu wa jirani sana na sisi, wanaotegemea utatuzi wa matatizo yao yote kwenye uchawi, au kwa waganga wa kienyeji. Na wakati mwingine tunasafiri kwenye mabasi na Si rahisi kabisa kuwatambua watu wa mamna hii kwa macho ya nyama,
Hii ni muhimu sana kufahamu kuwa usipojua kuwa unahitaji kujipanga kila wakati kwenye maombi utaishi maisha ya hatari kila siku. Biblia inasema katika Efeso 6:10 hatimaye, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu zake.

MAFUNDISHO YA NENO LA MUNGU

It is evident that the present dispensation under which we are is the dispensation of the Spirit, or of the Third Person of the Holy Trinity. To Him in the Divine economy has been committed the office of applying the redemption of the Son to the souls of men and women by the vocation, justification, and salvation of the elect. We are, therefore, under the personal guidance of the Third Person as truly as the apostles were under the guidance of the Second." (Edward Manning)

Friday, June 6, 2008

HUDUMA ZA MAOMBEZI

Mwalimu Tuntufye akiwa katika moja ya makongamano ambayo huwa anayaendesha.

Saturday, May 31, 2008

WIKI HII

Youth Christian organization fellowship, which conduct prayer as youth Christian prayer network
Mtandao huu wa maombi ya vijana walio dhamilia kudhihilisha Nguvu za Mungu duniani

Hata ikawa mwisho wa siku saba neno la bwana likanijia kusema mwanadam nimekuweka kuwa mlinzi juu ya nyumba ya izraeli [eze 3:16 ]
Mambo ya kuombea

v Ombea watumishi wa Mungu ambao mungu anawatumia juu ya Taifa , Mungu awape mafunuo juu ya Taifa utulivu na unyenyekevu mkubwa, kataa roho za kujiona bora kuliko wengine , ombea familia zao , ndoa zao ,mafanikio ya kiuchumi, hata kama wametenda dhambi omba toba juu yao , hawa ni maaskofu , wachungaji ,na wainjilsti,
v Ombea huduma ya mana ,mtumishi Mwakasege, ombea huduma ya agape,mtumishi fenandusi, ombea huduma ya mama lwakatale, Nabii mwingila,pastor hiza ,newlife oustrich under egon falk,huduma ya ukwata, huduma ya new life band, new life ministry , scripture union na huduma zingine nyingi Mungu ametumia huduma hizi kuvuna maelfu ya watu zikabidhi mikononi mwa Mungu

Kwa sara zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatiu [ waefeso 6:18]

Basi kabla ya mambo yote nataka dua na sala na maombezi na shukrani zifanyike kwa ajili ya watu wote [1timoth 2:1]
· Msogeze mbele za Mungu huyu dada aitwae mary ni mwanafunzi anaye soma kwa mateso makali kwa sababu ya kuathilika na ukimwi omba uponyaji na rehema za Mungu juu ya maisha yake anaishi mkoani Tanga fanya dua sara na maombi kwa ajili yake
· Msogeze mbele za Mungu huyu kaka aitwaye hebron anasoma chuo cha usafilishaji Dar Mungu afungue mrango wa ada kabla ya tar16 january si chini ya 2laki kw semister ya kwanza
· Ombea ndoa za watu walio okoka , kataa vurugu,mikosi ,omba hali nzuri za kiuchumi,kataa Roho ya matengano, panda upendo mpya , panda amani, utulivu, na hofu ya Mungu kwenye ndoa hizo
· Ombea vijana walioingia kwenye uchumba,Mungu awafanikishe, watunze utakatifu, mmoja asiwe jeraha kwa mwingine, omba safari njema mpaka siku ya ndoa,kataa mahusiano yanayosababisha vijana wengi watoke kwenye mpango wa Mungu
· Ombea mabinti waliojiingiza kwenye ukahaba tu kwa sababu ya kukosa msaada yaani ni yatima , au mafukara , hana msaada wowote , au vijana wakiume waliojiingiza kwenye uvutaji wa bangi , madawa ya kulevya, upolaji, ujambazi, na mambo mengineyo ambayo si ya haki mbele za Mungu, hawakupenda kufanya haya ila ni kwa sababu tu ya kukosa msaada wakafikili njia rahisi ni hiyo omba rehema za Mungu juu yao·

Kwa kusudi hili mwana wa Mungu alidhihilishwa apate kuzivunja kazi za ibilisi [1yoh 3:8b]
kataa Roho za mauti juu ya nchi na juu ya afrika mashaliki ikiwa ni pamoja na makafara, roho za ajali , miripuko ya magonjwa,umwagaji wa Damu na matambiko yanayoendelezwa na baadhi ya makabila nchini kitu ambacho kinapelekea laana juu ya nchi amuru hizo kazi za adui kuvunjika
kumbuka na huu ndio ujasiri tulio nao kwake ya kuwa tukiomba kitu sawa sawa na mapenzi yake atusikia [2 yoh 5;14]

Baada ya maombi haya unaweza kutuambia nini Mungu kafanya ukiwa na ushuhuda mistari ya kututia Moyo, au vitu fulai umevipata toka kwaMungu, ombea huduma hii mikoa yote ya Tanzania na Afrika mashariki, ombea waombaji wote wa huduma hii kumbuka kumuombea coordinator Tuntufye Andrew.

TAMASHA LA INJILI KWA NAMNA YA PEKEE ARUSHA

Kuwashirikisha Christina Shusho, Frola Mbasha, Jackson Bent pamoja na Kwaya nyingine.

Waimbaji wa muziki wa injili Christina shusho na Frola mbasha toka Dar es Salaam wanatarajiwa
kuhudhuria katika tamasha la injili linaloandaliwa na IRPAYAN O’ NGERA ORGANIZATION ambalo ni shirika la dini linalohudumia watoto yatima mkoani Arusha.

Akizungumza na afu hii ya MAONI NA SALA, Muandaaji wa Tamasha hilo Bw.Jemsi Losioky alisema kuwa tamasha hilo litakuwa maalum kwa ajili ya kuwasaidia watoto wanaoishi kwa matumaini wa kituo hicho.

Tamasha hilo linalotarajiwa kufanyika jumapili ya tarehe 8/06/2008 kuanzia saa nane mchana katika Hotel ya Gorden Rose jijini Arusha litapambwa na wakali wa injili hapa nchini ambaye ni Frola Mbasha na Christina Shusho kutoka Dar es Salaam.

Wengine ni Jackson Bent wa Arusha, Marther J. mushi, Sauti ya Nyikani Band wote kutoka Kilimanjaro pamoja na waimbaji wengine ambao hawakutajwa kwa sasa.

Tiketi za tamasha hilo kwa sasa zinapatikana kituo cha Radio ya Kikristo ya Safina FM iliyoko Arsuaha, Kimahama Bookshop pamoja na Golden Roze Hoteli (Arcade Comference Centre)

Tamasha hili linategemewa kuwa ni la aina yake kutokana na matamasha ya aina hii kutofanyika mara kwa mara.

Kwa mawasiliano zaidi 0754202623 au 0715 629562